Nicksixyo
JF-Expert Member
- Jan 11, 2011
- 944
- 263
Kwa habari nilizozipata muda sio mrefu kuanzia jana hadi leo pamekuwa na maandamano na vurugu za wanachuo baada ya mwenzao mmoja kugongwa na gari hapo nje ya geiti ya chuo.Wamekuwa wakiomba serikali isikie kilio chao cha kuweka bansi eneo hilo baada ya kuwepo kwa matukio mengi ya ajali,bila ya mafanikio.
Hatima na machungu yao imefikia ukingoni jana baada ya mwenzao mwingine kugongwa na kufia hapohapo njia. Wachungaji maaskofu na wote waliopo katika chuo hicho kwa masomo yao wameamua kutoka kudai haki yao ya kusikiliza na serikali kwa kuzuia magari yote yapitayo njia hiyo kuu ya Moshi - Arusha.
Waliopo maeneo hayo tunaomba mfuatilie tukio hili mtuletee habari zaidi kwani bado hali ni ya kuviziana kati ya polisi na wanachuo hao. Polisi wakifika hawaoni mtu lakin wakiondoka magari yanayopita hapo yanapigwa mawe na kuwekewa vizuizi barabarani. Nchi imekuwa mtafaruku...Nawakilisha.
Hatima na machungu yao imefikia ukingoni jana baada ya mwenzao mwingine kugongwa na kufia hapohapo njia. Wachungaji maaskofu na wote waliopo katika chuo hicho kwa masomo yao wameamua kutoka kudai haki yao ya kusikiliza na serikali kwa kuzuia magari yote yapitayo njia hiyo kuu ya Moshi - Arusha.
Waliopo maeneo hayo tunaomba mfuatilie tukio hili mtuletee habari zaidi kwani bado hali ni ya kuviziana kati ya polisi na wanachuo hao. Polisi wakifika hawaoni mtu lakin wakiondoka magari yanayopita hapo yanapigwa mawe na kuwekewa vizuizi barabarani. Nchi imekuwa mtafaruku...Nawakilisha.