Mzee Mwanakijiji
Platinum Member
- Mar 10, 2006
- 33,476
- 39,995
Tawala zote duniani ambazo zimeshindwa kuwajibu wakosoaji wake mara zote zimegeukia kutumia nguvu kuzima hoja dhidi yao. Hili ni kweli na tumeliona Syria, kama tulivyoliona Misri; tumeliona Georgia kama ilivyo Russia; tumeliona Libya kama tulivyoliona Uchina. Mara nyingi watawala wanaposhindwa hoja wao hutumia risasi kama siyo virungu na pingu.
Hoja za wapinga Muungano zimekuwa wazi kwa muda mrefu;hakuna jambo linalosemwa leo ambalo kwa mtu yeyote anayefuatilia siasa za Tanzania anaweza kushangazwa kwamba ni ngeni. Siyo hoja ya mafuta wala siyo hoja ya Utanganyika, siyo hoja ya kunyanyaswa wala hoja ya kubanwa zote hizi ni hoja zilizodumu kwa takribani miongo mitano sasa. Hakuna jipya.
Bahati mbaya sana, wakati wa Mwalimu hoja hizi zilijibiwa kwa kutumia nguvu ya hoja. Kwa kuzichukua hoja zinazotolewa na kuzikata vipande vipande na kuzifunua kwa kuonesha udhaifu wake. Na hii ndio sababu ya mwalimu Nyerere kuamua mara mbili kujibu hoja za wapinga Muungano bila kulazimika kuitisha matumizi ya nguvu. Ukisoma kitabu cha Uongozi Wetu na Hatima ya Tanzania utaona jinsi hoja za Muungano zilivyojibiwa; na ukirejea ile hotuba ya Juni 14, 1995 Kilimanjaro hoteli utaona kuwa Nyerere aliweza kuzichambua hoja zote hizi kwa kutumia mantiki na hadi leo hakuna mtu ambaye ameweza kujitokeza kuonesha udhaifu wa hoja hizo - isipokuwa mashambulizi binafsi (ad hominem) dhidi ya nafsi ya Nyerere.
Leo hii tunashuhudia viongozi walioshindwa - bara na visiwani - wakitumia nguvu ya risasi, pingu na vurungu kujaribu kupangua hoja za wapinga MUungano. Bahati mbaya sana hakuna risasi, kirungu au pingu iliyowahi kujibu hoja! Kwa kushindwa kusimama na kuzijibu hoja hizi moja baada ya nyingine watawala hawa wanawapa na niseme wamewapa nguvu wapinga Muungano.
Kwa muda mrefu baadhi yetu tumekuwa tukiutetea Muungano kwa kuonesha udhaifu wa hoja za wapinga Muungano lakini sasa na sisi wengine tumefikia kikomo. Kwanini sisi tusio viongozi na watawala tusimame kuutetea Muungano wakati mamia ya wabunge walioapa kuulinda Muungano huu wakila kuku na kujipepea huku wakinywa vinywaji vikali? Kwanini, sisi watu wa kawaida ambao hatulipwi hata senti moja ya Muungano kusimama na kutetea Muungano wakati wapo watu ambao walipita huku wengine wakipiga magoti kuomba uongozi wa JMT?
Inawezekana vipi leo watu wanatukuzwa ati ni "viongozi vijana" na kuwa "wamesoma" lakini wameshindwa kusimama na kujenga hoja za kuutetea Muungano huku wakipinga hoja dhaifu zinazotolewa dhidi ya Muungano? Ukweli ni kuwa Muungano ulipofika sasa hauwezi kuteteeka na hauna mtetezi. Kikwete hawezi kujenga hoja ya kuutetea wala Shein - kama alivyozungumza juzi- hana ujasiri wala uwezo wa kuutetea Muungano. Vuai hawezi wala Seif hawezi kuutetea; siyo Makinda wala Pinda na siyo Kificho wala Mkuchika wanaoweza kuutetea Muungano. Hakuna mbunge hata mmoja ambaye anaweza kusimama na kujenga hoja ya kuutetea Muungano au kuwajibu wengine zaidi ya wabunge nao kuchochea tu hoja za kwanini huu Muungano hauteteeki!
Je wakati umefika wa kuanza kusema:
Farewell Zanzibar, Goodbye Muungano?
Hoja za wapinga Muungano zimekuwa wazi kwa muda mrefu;hakuna jambo linalosemwa leo ambalo kwa mtu yeyote anayefuatilia siasa za Tanzania anaweza kushangazwa kwamba ni ngeni. Siyo hoja ya mafuta wala siyo hoja ya Utanganyika, siyo hoja ya kunyanyaswa wala hoja ya kubanwa zote hizi ni hoja zilizodumu kwa takribani miongo mitano sasa. Hakuna jipya.
Bahati mbaya sana, wakati wa Mwalimu hoja hizi zilijibiwa kwa kutumia nguvu ya hoja. Kwa kuzichukua hoja zinazotolewa na kuzikata vipande vipande na kuzifunua kwa kuonesha udhaifu wake. Na hii ndio sababu ya mwalimu Nyerere kuamua mara mbili kujibu hoja za wapinga Muungano bila kulazimika kuitisha matumizi ya nguvu. Ukisoma kitabu cha Uongozi Wetu na Hatima ya Tanzania utaona jinsi hoja za Muungano zilivyojibiwa; na ukirejea ile hotuba ya Juni 14, 1995 Kilimanjaro hoteli utaona kuwa Nyerere aliweza kuzichambua hoja zote hizi kwa kutumia mantiki na hadi leo hakuna mtu ambaye ameweza kujitokeza kuonesha udhaifu wa hoja hizo - isipokuwa mashambulizi binafsi (ad hominem) dhidi ya nafsi ya Nyerere.
Leo hii tunashuhudia viongozi walioshindwa - bara na visiwani - wakitumia nguvu ya risasi, pingu na vurungu kujaribu kupangua hoja za wapinga MUungano. Bahati mbaya sana hakuna risasi, kirungu au pingu iliyowahi kujibu hoja! Kwa kushindwa kusimama na kuzijibu hoja hizi moja baada ya nyingine watawala hawa wanawapa na niseme wamewapa nguvu wapinga Muungano.
Kwa muda mrefu baadhi yetu tumekuwa tukiutetea Muungano kwa kuonesha udhaifu wa hoja za wapinga Muungano lakini sasa na sisi wengine tumefikia kikomo. Kwanini sisi tusio viongozi na watawala tusimame kuutetea Muungano wakati mamia ya wabunge walioapa kuulinda Muungano huu wakila kuku na kujipepea huku wakinywa vinywaji vikali? Kwanini, sisi watu wa kawaida ambao hatulipwi hata senti moja ya Muungano kusimama na kutetea Muungano wakati wapo watu ambao walipita huku wengine wakipiga magoti kuomba uongozi wa JMT?
Inawezekana vipi leo watu wanatukuzwa ati ni "viongozi vijana" na kuwa "wamesoma" lakini wameshindwa kusimama na kujenga hoja za kuutetea Muungano huku wakipinga hoja dhaifu zinazotolewa dhidi ya Muungano? Ukweli ni kuwa Muungano ulipofika sasa hauwezi kuteteeka na hauna mtetezi. Kikwete hawezi kujenga hoja ya kuutetea wala Shein - kama alivyozungumza juzi- hana ujasiri wala uwezo wa kuutetea Muungano. Vuai hawezi wala Seif hawezi kuutetea; siyo Makinda wala Pinda na siyo Kificho wala Mkuchika wanaoweza kuutetea Muungano. Hakuna mbunge hata mmoja ambaye anaweza kusimama na kujenga hoja ya kuutetea Muungano au kuwajibu wengine zaidi ya wabunge nao kuchochea tu hoja za kwanini huu Muungano hauteteeki!
Je wakati umefika wa kuanza kusema:
Farewell Zanzibar, Goodbye Muungano?