Bumpkin Billionare
JF-Expert Member
- Jan 5, 2012
- 1,332
- 621
Mara kadhaa nimekuwa nikipigiwa simu na namba 0901901901 ambayo ni automated call. Unapopokea simu hii unapatiwa maelezo ambayo huna haja wala shida nayo jambo ambalo kwangu mimi huwa naliona usumbufu tu. Cha kushukuru angalau kidogo namba hii ni tofauti na namba zingine za simu kwa hiyo sasa naweza kui-ignore.
Leo mchana huu nikiwa maeneo ya Ruvu Darajani nikiwa naendesha gari nimepigiwa simu na namba +255684000165, kwa kuwa nilikuwa kwenye barabara inayopitiwa na magari yanayoenda kasi niliamua kupaki gari pembeni niweze ku-attend hiyo call; KICHEFUCHEFU KITUPU!
"Hallow, mimi ni 'SIJUI KITUKO GANI MWAITEGE' nafurahi kwa kuwa najua wewe ni mpenzi wa nyimbo zangu. Ili kupata nyimbo zangu......" mpk hapa niliamua kukata kwani nilishasikia hasira.
Swali langu: Hivi kusajiliwa simu zetu na TCRA nia ilikuwa ni kutusupply haya makero au ni nini?
Imagine ndio umerudi job jioni umepumzika zako huku simu iko kwenye chaji, mtu anakunyanyua kwenda kuifuata kwa ajili ya tangazo lake la kipuuzi, huyu mama mimi nimemwambia nataka matege?
Kama ni biashara jamani, si ziwekwe kwenye mabango mwenye kutaka na ajisomee tusiotaka tupite kama hatujaziona. Huu ni usumbufu kwa kweli, unless kwa watu ambao kazi zao haziwachoshi mwili na akili. Mimi binafsi haya matangazo ya lazima YANANIKERA KUPITA KIASI.
Wengine ni TIGO. Hii mimesej mnayotujazia kwenye inbox zetu ni lazima au ni sehemu ya mikataba ya huduma? Oooh ukitaka raha tuma neno utamu kwenda 56601 huu sio upumbavu jamani?!!! Siku moja unatumiwa huu ****** mara 3 mpk 5, ni nini lakini?
Leo mchana huu nikiwa maeneo ya Ruvu Darajani nikiwa naendesha gari nimepigiwa simu na namba +255684000165, kwa kuwa nilikuwa kwenye barabara inayopitiwa na magari yanayoenda kasi niliamua kupaki gari pembeni niweze ku-attend hiyo call; KICHEFUCHEFU KITUPU!
"Hallow, mimi ni 'SIJUI KITUKO GANI MWAITEGE' nafurahi kwa kuwa najua wewe ni mpenzi wa nyimbo zangu. Ili kupata nyimbo zangu......" mpk hapa niliamua kukata kwani nilishasikia hasira.
Swali langu: Hivi kusajiliwa simu zetu na TCRA nia ilikuwa ni kutusupply haya makero au ni nini?
Imagine ndio umerudi job jioni umepumzika zako huku simu iko kwenye chaji, mtu anakunyanyua kwenda kuifuata kwa ajili ya tangazo lake la kipuuzi, huyu mama mimi nimemwambia nataka matege?
Kama ni biashara jamani, si ziwekwe kwenye mabango mwenye kutaka na ajisomee tusiotaka tupite kama hatujaziona. Huu ni usumbufu kwa kweli, unless kwa watu ambao kazi zao haziwachoshi mwili na akili. Mimi binafsi haya matangazo ya lazima YANANIKERA KUPITA KIASI.
Wengine ni TIGO. Hii mimesej mnayotujazia kwenye inbox zetu ni lazima au ni sehemu ya mikataba ya huduma? Oooh ukitaka raha tuma neno utamu kwenda 56601 huu sio upumbavu jamani?!!! Siku moja unatumiwa huu ****** mara 3 mpk 5, ni nini lakini?