Mkenazi
Senior Member
- Apr 11, 2011
- 124
- 43
Sioni jambo jipya linaloweza kufanikishwa na CCM ikiwa mambo waliyopanga wenyewe yamewashida kama nilivyoweza kukumbuka machache hapa chini:
- Chama cha Mapinduzi kilishindwa kutekeleza programu yake ya miaka 15 (1987 2002). Pamoja na mambo mengine kulikuwa na kipengele kinasema "IFIKAPO 2002 kila wilaya itakuwa na matrekta 25" Mpaka leo hakuna kitu kama hicho badala yake miaka 24 baadae bado mnaongelea kununua Power tiller tena kwa UFISADI
- Chama cha mapinduzi kilianzisha mradi wake wa SUKITA pale bonde la Tabata kikashindwa, SUWATA kikashindwa ; leo CCM wanazunguka wanatuimbia wimbo wa EL, RA na AC yaani wanatafuta huruma za wananchi wa Tanzania kupitia mazao ya mfumo wao. Tumekwisha wagundua.
- Nchi nzuri Tanzania kwa sababu ya utawala wa CCM haina hata shirika la ndege lenye ndege za uhakika. Tunazidiwa na Rwanda. Hawa wawekezaji waliojaa nchini wangekuwa wanapanda ndege zetu shirika lingekuwa kubwa sana.
- UMEME – Eti mpaka leo hatuna umeme wa kutoshereza mjini. Mawazo ya CCM ni kukodisha tu hii ni milango ya UFISADI. Iko wapi mipango ya MCHCHUMA, KIWIRA na LIGANGA coal projects ? toka miaka hiyo mpo tu halafu mnasema mnataka ridhaa ya wanachi muendelee kuwatesa.
- VIWANDA, enzi hizo za Mwalimu Tanga, Morogoro, Dar Arusha n.k kulijaa viwanda vya kila namna na kutoa ajira leo viko wapi ? bado mnataka muendelee kutawala – Nasema imeishatosha pumzikeni muone wenye akili watakavyofanya kazi.
- CCM ni nini hasa ilichokianzisha kikafika mwisho kwa mafanikio ? Ilianzisha RUBADA – Rufiji Basin Development Authority miaka ya 1975 – Hilo bonde limeendelezwa ? ikaja KOTACO – Korea Tanzania Agricultural Company kwenye mabonde ya chitah je mlifanikiwa ?, haya kuna kilmo cha kufa na kupona miaka ya 1974, kilimo ni uti wa mgongo, Kilimo kwanza, MKUKUTA, Mkurabita n.k.
- Oh CCM – mmewadhoofisha wana wa Tanzania kwa kuwajengea mawazo hasi kwa kila eneo mf. Kauli ya viongozi wote wa CCM ni kusema tanzania ni masikini – hii ni mbaya sana. Nchi isiyotaka kutumia wataalamu wake Waandisi, wakandarasi n.k hii yote ni sababu ya UFISADI. – CCM inachojua ni kuchakachua tu hata taarifa za utafiti inachakachua ili ionekane imefanya vizuri.
- ELIMU – Shule za Yebo yebo – hakuna maabara halafu mnasisitiza masomo ya sayansi au kwa kuwa viongozi wengi na watoto wenu mnasomea siasa ?. Hakuna mkakati wa Kitaifa wa kuifanya sayansi ijenge uchumi wa nchi. Ikiwa mhandisi wa kitanzania ndiye supervisor kwenye makampuni ya wakoloni tutegemee nini ? - UFISADI kila sehemu.
- CCM, CCM, CCM pamoja na wabunge wako kitendo cha kuipenda ccm ya watu milioni tano kuliko watu milioni 40 wasiokuwa CCM na ambao ni wapiga kura wenu mnatenda kosa kubwa sana na ndio maana hamtapewa ridhaa tena ya kuongoza nchi hii. Wabunge wa CCM wanashangilia kil akitu hata kama ndani yake kina ajenda ya kuwachinja ndugu zao. Wabunge wa CCM walishangilia mswada wa uundaji wa tume ya Katiba mpya ulioondolewa bungeni, lakini pia wangeupitisaha serikali ingelazimisha uende bungeni. Huu ni wendawazimu ambao ni magamba kuliko hata haya y aya juzi kwani matokeo ya katiba dhaifu ni ufisadi uliokithiri.
- CCM kimekuwa ni chama cha kijeshi kama ifutavyo
- Rais – ni mwnajeshi
- Wakuu wa mikoa wengi wanajeshi wasitaafu
- Wakuu wa wilaya – Wanajeshi
- Makamba, Kapteni Mkuchika, Nape mtoto wa mwanajeshi, January Makamba – baba yake mwanajeshi, Kinana
- SHIME Watanzania tunayo kazi moja tu nayo ni kumwondoa nduli CCM kwani NIA tunayo, Sababu tunazo na uwezo tunao.