Hizi ndo athari za kupanda kwa bei ya umeme

Wewe mawazo yako nafikiri tulisoma shule na darasa moja maana tunaongea rugha moja lakini nashangaa mengine kwanini hayaelewi au ndio vibaraka wanaandika vitu hata haviingii akilini. ni kwamba pesa hizo si kwaajili ya kusaidia umeme vijijini embu nambie kwahiyo umeme ukishakwenda vijijini ndo gharama itapungua? na je kama haitapungua hao uliowaunganisha vijijini nao si watapaswa kulipa bei hizo mpya? sasa piga picha maisha ya kijijini then angalia kama inawezekana kwao kufanya hivyo. si bora wabaki hawana umeme, na kwa taarifa yako hata kama bei wangeongeza mara kumi bado isingewatosha kutokana na ufisadi ulokithiri na kumbuka kuna deni tanesco wanalilipa kwa moja ya makampuni yenu yaleeeeee. KWELI ALIYESHIBA HAMJUI MWENYE NJAA YAANI KWASABABU WEWE MAMBO SAFI BASI UNASHADADIA TU KUWA IPANDE KWA SABABU WALIZOKUDANGANYA KUWA NDIZO AMKA WEWE.
 
Huu ni wizi wa hali ya juu, watu wanaficha mikataba ili watuibie halafu viongozi wa cvm wanakuja humu ndani wanajifanya wanakuja humu wanajifanya cdm haiewezi kuongoza. Hatutaki siasa tunataka maelezo ya kina kuhusu umeme kwanini ipande wakati pato letu watz liko palepale.
 
Sidhani kama ni busara kulipongeza hili, Hii ni hatari sana kwa ustawi wa maisha ya Watanzania Unapopongeza ni vema ukatafakari kwa kina kwani kuna mambo yaliyopita ambayo CCM wametuaminisha kuwa yatasaidia kupeleka umeme vijijini
1. Kikwete akiwa katika ziara zake kanda ya Ziwa alitamka kuwa Marekani (USA) imeisaidia Tanzania katika Mradi mkubwa wa umeme na ni nchi pekee Africa iliyopewa fedha nyingi katika Mradi huu wa Umeme. Kwa kauli hii kulikuwa na haja ya kuongeza gharama eti kusaidia kupeleka umeme vijijini?

Mareakani itatoa na kwa ajili ya sector development sio kwa ajili ya recurring budget

2. Tunaponunua umeme kuna 3% REA ambayo tunaambiwa ni kwa ajili ya kusaidia kupeleka umeme Vijijini, Kato hili maana yake nini?
Hoja nzuri; only remember the company is running at loss as we speak!

3. Nakumbuka Zanzibar walikuwa wanadaiwa na TANNESCO 50,000,000,000/= lakini cha kushangaza deni hili lilisamehewa na TANNESCO na mzigo huu ndio unatuangukia sisi kufidia.
Whether wamesamehe au wanadai ukweli ni kwamba hizo hela hawanazo

4. TANNESCO wananunua umeme kutoka SONGAS na IPTL sisi kama wananchi hatujui wanauziwa kwa shillingi ngapi na wao wanaamua kula cha juu kutuuzia sisi, lakini cha msingi tungejiuliza hii Gesi inayozalisha umeme ule kule Songas ni ya kwetu lakini cha ajabu wageni wamemiliki mitambo hiyo kwa kutumia gesi yetu wanazalisha umeme na kutuuzia huu ni ujinga.
I think it is clear, gesi ya kwetu, ila hatukutafiti sisi, hatukuchimba sisi, hatusafirishi sisi, na kwa kiwango kikubwa hatu-convert gas to power sisi; So why get free? Bei iliyopo is better tatizo bado tunatumia umeme wa mafuta mazito na diseal.

*** Namalizia kwa kukuambia na kaa ufahamu hivyo ongezeko hili ni kwa ajili ya kupata fedha za kuwagawia CCM kwa ajili ya matumizi ya uchaguzi 2015 kwani lile dili la line za Simu lilipogonga mwamba ndio maana wamehamia huku. Hakuna cha Umeme vijijini wala nini yote hii ni wizi na unyanyasaji kwa raia.
Ni mtu asiyekwenda shule tu ndiye anaweza kufikiri CCM inauwezo wa kuchukua sumni ya TANESCO.... That is impossible hata kama wangetaka iwe hivyo!
 
wanakusanya pesa ya uchaguzi 2015
Taifa haliwezi endelea na mindset za kipuuzi kama hivi! Hela ya Kampuni la Umma haitoki kihuni huni tu ndugu, Ndio maana CCM wanakimbizana kufufua miradi yao b'se other than ruzuku ya vyama no any cent from
government viongozi wa CCM, CHADEMA, CUF etc wanajua hili!
 
Wengine tunaongozwa na ku-think Big na critically; TANESCO lazima tuipe uwezo iweze kukopesheka ili tuitoe kwenye mzigo wa kubebwa na serikali... na tunaweza tu kufanya hivyo kwa kuipa momentum. Ambayo ni kulipia huduma zake ili serikali ikate kupeleka ruzuku ambayo inachezewa, then tuibane TANESCO kwa huduma ambayo ni fully paid without subsidy!!!!

nafikiri utakuwa mmoja wa beneficiaries wa tanesco. naona kale kakampuni kako ka kifisadi kataanza kuchota nyingi. mwe,hu mkubwa wewe.
 
nafikiri utakuwa mmoja wa beneficiaries wa tanesco. naona kale kakampuni kako ka kifisadi kataanza kuchota nyingi. mwe,hu mkubwa wewe.

Mimi sitegemei favour yoyote kwenye maisha yangu, nina viungo vyote namshukuru Mungu kwa hilo na biashara yangu ya uvuvi inalipa!!! Sitegemei maisha yangu nisaidiwe na vyama vya siasa au serikali,
 
Wa akina Zitto na Mbowe njoeni sasa mtutetee kuhusu umeme,yeyote mwananchi atakayeudhuria mikutano yao yenye ajenda zao za mipasho na wakasahau kuhusu kuzungumzia jinsi ya kuandamana kupinga ongezeko la bei ya umeme wewe mwananchi utakuwa mjinga wa kutupwa.

Goso la Sumbawanga limekulevya, unashindwa kuwashutumu CCm waliopandisha bei ya umeme olive wapate pesa za kuwahonga wavutaji kama wewe, una anza kuwa2kana makamanda. Haya being imepanda-wewe umechukua ha2a gani?
 
Mimi sitegemei favour yoyote kwenye maisha yangu, nina viungo vyote namshukuru Mungu kwa hilo na biashara yangu ya uvuvi inalipa!!! Sitegemei maisha yangu nisaidiwe na vyama vya siasa au serikali,
Bwana Kasheshe unaonekana unatokea huko serekalini unaonanaje ukatusaidia sisi eatanzania tukajua mikataba ya umeme inasemaje? Kwani nasikia hamtaki hata kuipeleka bungeni iwekwe wazi. Unadhani mnsogopa nn watz wasijue maana hapo ndio siri ya kupandisha hivi ilipo
 
Umetoa hoja nzuri sana. Lakini hiyo principle itafanya kazi pala tayari umeme, nguzo, nyaya, mita na internal wiring zimefanyika kwa waTanzania wengi, Other than that it does not apply. Nawakumbusha tu kwamba TANESCO inataka ku-kopa iendeleze generation, distribution na supply ya umeme majumbani na viwandani lakini wakopaji wanasema hawezi kopesha shirika ambalo haliwezi kujenereti its own money, linategemea hisani
ya waziri wa fedha. Hivyo kupanda huku kwa tarifu kutalitoa kampuni kwenye matatizo,

Hoja kwamba TANESCO haiwezi kujiendesha yenyewe na inategemea hisani ya serikali inabidi ichunguzwe zaidi.

Deni ambalo TANESCO inaidai serikali limefika kiasi gani? Deni la Zanzibar limelipwa? madeni ya Wizara n taasisi zingine nyeti za serikali yamelipwa?

Kama hayajalipwa yamefikia kiasi gani?

Maana tusije kusema serikali inaifanyia hisani TANESCO wakati ukweli unaweza kuwa serikali inalipa deni lake polepole.

Hili ni swali tu, sina maana kusema deni ambalo TANESCO linaidai serikali ni kubwa kuliko "ruzuku" ya serikali kwa TANESCO.

Hilo moja, la pili, dunia nzima, wanaobeba mzigo wa kulipia gharama za uendeshaji wa wafua na wasambazaji umeme ni wafanyabiashara wakubwa na viwanda vyao. Wananchi wa kawaida wanaotumia taa, friji, TV na pasi hawana matumizi makubwa ya umeme. Serikali iangalie hali ya maisha ili umeme usije kuwa kitu cha anasa kwa mtu wa kawaida. Hili litatugharimu sana, kwani hata watoto wanaotaka kusoma itabidi watumie taa kwa kuangalia LUKU, au waende kutumia taa ya barabarani, kama ipo.

Kwa nini Tanzania bei ya umeme iko juu hivi? Who is responsible for this?
 
Naunga mkono bei kupandishwa ili na wengjne nao wapate umeme, tulikuwa only 10% Now we need to go 30%. Sasa haiwezekani kufanya hivyo kwa ruzuku ya serikali.

mkuu unaweza kuniambia kodi wanazokusanya wanapeleka wapi na katika bajeti hii pesa za maendeleo zilikuwa ngapi na za matumizi ngapi ikiwemo safari lukuki za rais?
muache kutukamua tumechoka!!!!
na gas mmpandisha ili iweje?
 
Bei za kusaga na kuboa nazo juu,wenye visima vya maji baadhi wamepandisha kutoka sh.50 kwa ndoo hadi sh.100, bei za unga nazo zinaanza kupanda kwakuwa nao hutumia umeme ktk kukoboa na kusaga. Huu ni mwanzo tu mengi yanakuja... Mbebaji wa mizigo yote hiyo ni mwananchi wa kawaida.

Mkuu kila kitu kimepanda kwa asilimia kubwa si ugali si wali.
 
Back
Top Bottom