Papa Mopao
JF-Expert Member
- Oct 7, 2009
- 4,107
- 2,506
Juzijuzi pale Mlimani city nilikuwa na washkaji wawili,mshkaji mmoja alimuona binti mzuri,mzuri saana yaani mweupeeee ngozi haijakwaruzwa hata kidogo,figure imeenda shule mtembeo wake unaleta raha ukimuanaglia anavotembea,sasa huyu jamaa yetu uvumilivu ulimshinda mpaka akachukua uamuzi wa kumfuata mdada akamwage sera za kufungua 'mawasiliano tamu',tulimjibu poa,jamaa aliondoka zake,mie na mshkaji mwingine tulibaki pale samaki samaki.Baada ya muda jamaa akarudi pale alipotuacha akiwa mnyongeee kwanza tulivoona hivyo tulicheka saaana yaani sana,tukamuuliza kulikoni? alitujibu kwa neno moja tu,"unanuka!" tulicheka saana tuliposikia hilo jibu.Huyu mshkaji mwingine akamjibu kwamba yule mdada hamfai anajua dharau!
Sasa kutokana na hili,kitu ninachojiuliza bila majibu hivi hawa wasichana wanatafuta nini mpaka wanadiriki kumtamkia mtu hayo maneno kwa mwanaume? Au malezi?
Sasa kutokana na hili,kitu ninachojiuliza bila majibu hivi hawa wasichana wanatafuta nini mpaka wanadiriki kumtamkia mtu hayo maneno kwa mwanaume? Au malezi?