Hivi wasichana wanaangalia nini kwa wanaume?

Papa Mopao

JF-Expert Member
Oct 7, 2009
4,107
2,506
Juzijuzi pale Mlimani city nilikuwa na washkaji wawili,mshkaji mmoja alimuona binti mzuri,mzuri saana yaani mweupeeee ngozi haijakwaruzwa hata kidogo,figure imeenda shule mtembeo wake unaleta raha ukimuanaglia anavotembea,sasa huyu jamaa yetu uvumilivu ulimshinda mpaka akachukua uamuzi wa kumfuata mdada akamwage sera za kufungua 'mawasiliano tamu',tulimjibu poa,jamaa aliondoka zake,mie na mshkaji mwingine tulibaki pale samaki samaki.Baada ya muda jamaa akarudi pale alipotuacha akiwa mnyongeee kwanza tulivoona hivyo tulicheka saaana yaani sana,tukamuuliza kulikoni? alitujibu kwa neno moja tu,"unanuka!" tulicheka saana tuliposikia hilo jibu.Huyu mshkaji mwingine akamjibu kwamba yule mdada hamfai anajua dharau!

Sasa kutokana na hili,kitu ninachojiuliza bila majibu hivi hawa wasichana wanatafuta nini mpaka wanadiriki kumtamkia mtu hayo maneno kwa mwanaume? Au malezi?
 
Kwa wasichana wengi wa mjini kwa mtu ambaye hamjui yaani ndio first anamuona,kwanza mavazi ya mwanaume,perfum,muonekano,hata ile aproach ya mwanaume ndio silaha kuu ya kuanzia,huwezi muaproach msichana wa mjini uko rough huku jasho linakutoka,hatakuona kama mtongozaji bali utaonekana kama Kibaka unataka kumuibia tu ,inawezekana huyu kweli hakuwa smart!!!
 
Kwa wasichana wengi wa mjini kwa mtu ambaye hamjui yaani ndio first anamuona,kwanza mavazi ya mwanaume,perfum,muonekano,hata ile aproach ya mwanaume ndio silaha kuu ya kuanzia,huwezi muaproach msichana wa mjini uko rough huku jasho linakutoka,hatakuona kama mtongozaji bali utaonekana kama Kibaka unataka kumuibia tu ,inawezekana huyu kweli hakuwa smart!!!

Na msichana wa mjini ni nani?? Hivi kuna binadamu asiyetoka jasho?? labda mi sijui.

Unajua huku kujitia matawi ya juu ndiko kunakowafanya wanaume waghairi kuoa siku hizi na watoto wa kike kupenda mambo makubwa wanayoyaona kwenye tamthiliya na movies yanayowafanya kuishia kufanywa nyumba ndogo na kuishia kufa single and lonely.
 
Na msichana wa mjini ni nani?? Hivi kuna binadamu asiyetoka jasho?? labda mi sijui.

Unajua huku kujitia matawi ya juu ndiko kunakowafanya wanaume waghairi kuoa siku hizi na watoto wa kike kupenda mambo makubwa wanayoyaona kwenye tamthiliya na movies yanayowafanya kuishia kufanywa nyumba ndogo na kuishia kufa single and lonely.

Mkulu hilo nalo neeeeeno... Warembo hasa wa mjini wanaigiza hadi maisha yao ya kila siku... Wengi wao wanapenda kinakifiki!Bora niwe Super Bachelor!
 
Mkulu hilo nalo neeeeeno... Warembo hasa wa mjini wanaigiza hadi maisha yao ya kila siku... Wengi wao wanapenda kinakifiki!Bora niwe Super Bachelor!

Unajua tunaishi ktk kipindi cha social turmoil. Na media inatawala kwa kiasi kikubwa maisha yetu, jinsi watu wanavyo-behave na kuinteract na jamii zao. Bahati mbaya nionavyo mimi kadiri muda unavyoenda hali itazidi kuwa mbaya zaidi.
 
Kwanza mshikaji alikwenda kwa papara. Neno kunuka linaweza kuwa na maana nyingi, mojawapo huenda likawa kwamba alikuwa anamwambia kwamba "Umezidi mno kudandia usivyovijua". Kwani unapomwambia mtu ananuka rushwa, rushwa ina harufu? Huenda dada yule alishaona mbali, kwamba ikiwa kaka huyu hawajuani lakini anavutwa nami hivi, akiona mwingine si atamwendea vivyo, ANANUKA ufuska!

Wasichana wanawaona wanaume kama wanaume wanavyowaona wasichana. Simple, chemistry ikianza kati ya dada na kaka ni lazima reaction iwepo ili kujua compatibility yao. Any chemical reaction will reach an equilibrium na there will be no more reaction unless another chemichal interferes. Unaweza kupenda kiasai kwamba huwezi kuelezea kitu gani kimekuvutia. Mwingine kavutwa na makalio, mwingine miondoko, mwingine rangi, mwanya, miguu ya bia, macho, sauti, kifua, kiuno .... na kadhalika. Lakini mwisho wa yote mnalazimishwa jembe na shamba vikutane kazini. Kwani unashiba mwondoko wake? Hiyo rangi mbona huioni ukiwa kazini taa unazima?

Leka
 
Na msichana wa mjini ni nani?? Hivi kuna binadamu asiyetoka jasho?? labda mi sijui.

Unajua huku kujitia matawi ya juu ndiko kunakowafanya wanaume waghairi kuoa siku hizi na watoto wa kike kupenda mambo makubwa wanayoyaona kwenye tamthiliya na movies yanayowafanya kuishia kufanywa nyumba ndogo na kuishia kufa single and lonely.
Mkuu Abdulhalim nakupa tano. Mwishowe wasichana wanaishia kuwa wasagaji!!
Wengi ni wazuri kwa nje tu, lakini ndani hawajui mapenzi wala hawana upendo.
 
lakini wajameni Nguli aliwahi kusema kwa ukitaka amani ya moyo kwenye malovee bora uende uswazi mademu hawana nyodo za kijinga. Huyo mdada kwa maelezo tu ya huyo jamaa inaonyesha ni wale watoto wa geti na anajijua kuwa yuko juu fulani kwa hiyo lazima ukienda namna gani vipi itakuwa tabu. any way kwa uzoefu wangu majibu aliyopata jamaa kuambiwa ananuka ni majibu ya kawaida sana unapo-muapproach demu wa kiswahili for the first time. Mi kama huyo jamaa ningekuwa naye ningemwambia asikate tamaa ya kumfatilia huyo dada lazima mahali fulani mwenyewe angeamua kumsikiliza then na yeye angemaliza udhia!
 
Hujui wasichana wanaangalia Noti kwa mwanaume, we tafuta mwanamke alafu uwe huzami mfukoni uone.
 
Hujui wasichana wanaangalia Noti kwa mwanaume, we tafuta mwanamke alafu uwe huzami mfukoni uone.
Kwa mtazamo huu, tunakoelekea wasichana watakuwa wanapanga na kupokea mahali wenyewe.............. na si wazazi wao tena........!!!
 
Kwa mtazamo huu, tunakoelekea wasichana watakuwa wanapanga na kupokea mahali wenyewe.............. na si wazazi wao tena........!!!

Wanaume tunachunwa balaaa, kuna binti humu jamaa anamgharamia full DSTV, full tank wese, kodi ya nyumba si chini ya laki mbili kwa mwezi na mazaga zaga mengine alafu jamaa anamega tu hana mpango nae wa kumuoa.
 
Wanaume tunachunwa balaaa, kuna binti humu jamaa anamgharamia full DSTV, full tank wese, kodi ya nyumba si chini ya laki mbili kwa mwezi na mazaga zaga mengine alafu jamaa anamega tu hana mpango nae wa kumuoa.
Tatizo hata nyie wanaume mnapojipresent kwa wadada mnakwenda huku mkijionyesha kwa pesa na siyo nyie kama nyie mkiwa na moyo ulojaa upendo.
 
hivi kwani kunjibu mtu kistaarabu nayo ni big deal? hata kama umeona anakusumbua/kukera nmjibu tu kiutu uzima sio kumwambia "unanuka"....na wakaka punguzeni kuparamia, mkiona vichaka tu......yanawabana.
 
Tatizo hata nyie wanaume mnapojipresent kwa wadada mnakwenda huku mkijionyesha kwa pesa na siyo nyie kama nyie mkiwa na moyo ulojaa upendo.

Sasa kama na nyie bila pesa hamtukubali tufanyeje?
 
hivi kwani kunjibu mtu kistaarabu nayo ni big deal? hata kama umeona anakusumbua/kukera nmjibu tu kiutu uzima sio kumwambia "unanuka"....na wakaka punguzeni kuparamia, mkiona vichaka tu......yanawabana.

Halafu na wewe mbona hukunitakia heri ya mwaka mpya? Wanawake wengine wakijibu kibabe ndio wanaona dili eti!
 
Back
Top Bottom