Anselm
JF-Expert Member
- Nov 16, 2010
- 1,710
- 291
Kuna mtu aliwahi kutoa pendekezo humu kuwa Simba ianzishe mashindano maalumu kwaajili ya kuuenzi mchango wa Mafisango lakini naona tumeutia kapuni mazima.
Jamani ni ukweli usiopingika kuwa jina la Patrick Mutesa Mafisango huwezi kulitenganisha na mafanikio ya Simba kwa msimu huu wa 2011/2012 tukianzia na yale ya Kagame (kufika final),kutwa bingwa wa Ligi ya Vodacom na kufikia hatua ya 16 bora kwenye mashindano wa Kombe la Shirikisho Africa,sote ni mashahidi wa zile jitihada zake binafsi zilizokuwa mara kwa mara zikibadili matokeo ya Simba yaliyokuwa yanaelekea kuwa hasi na kuwa chanya ghafla.
Binafsi pamoja na kuwa na itikadi ya mlengo wa opposite na Simba lakini nilikuwa namkubali sana Marehemu, lakini najiuliza je kuitoa katika mpango wa kutumika jezi No. 30 iliyokuwa inavaliwa ndo kitu pekee walichoweza kufanya kwa aliyekuwa mchezaji wao mahiri ambao wenyewe walimbatiza jina la "jembe"?
Iliniwia vigumu kuamini kuwa Simba ilishindwa kutoa siyo tu rambirambi bali hata Mwakilishi anayeeleweka kutoka katika ngazi ya juu ya uongozi kuambatana na mwili wa Marehemu katika safari yake ya mwisho humu Duniani,najiuliza hivi kama Viongozi kadhaa wa juu to mention few Nyange na Rage pasipo ulazima wowote waliweza kuambatana na Mafisango alipokuwa hai na team kwenda Shandy kiasi cha kushindwa kuwa accomodated na kulazimika kulala kwenye makochi reception walishindwa nini kwenda na mwili wa Marehemu mpaka Kinkola?,au ndo zile za kujuana wakati wa raha tu wakati wa shida atajijua mwenyewe na familia yake.....haya na suala la rambirambi nalo.....ni aibu kwa Club kama Simba ambayo dhahiri inaonyesha ndo team iliyoongoza kwa mapato katika mchezo wa Soka hapa Tanzania kushindwa kupeleka hata senti 5 kwa familia ya Marehemu kama rambirambi,na je ziko wapi zile rambirambi zilizotolewa na wadau mbalimbali tokea ulipotangazwa msiba ule mpaka pale TCC tulipokuwa tunamuaga "Jembe"? kwanini hata zile basi hazikuwakilishwa kwa familia ya Marehemu? haya si ndo yaleyale ya kina Mtitu,JB,Ray na wengineo wa Kamati ya msiba wa Kanumba na rambirambi zake.
Kwanini lakini sisi binadamu tunakuwa hatuna uoga na Mwenyezi MUNGU kabisa?
Haya hata wiki 2 hazijaisha tayari viongozi,wanachama na mashabiki wa Simba wameshasahau msiba wa "Jembe" lao na sasa wako kwenye maandalizi kabambe ya kuangusha bonge la sherehe la kusherehekea mafanikio yaliyochangiwa na Marehemu,hivi kweli kwa mwenendo huu nikisema vilio vyao vya siku ile pale TCC vilikuwa ni vya kinafiki kuna mtu anaweza kunibishia?
Nawasilisha.
Jamani ni ukweli usiopingika kuwa jina la Patrick Mutesa Mafisango huwezi kulitenganisha na mafanikio ya Simba kwa msimu huu wa 2011/2012 tukianzia na yale ya Kagame (kufika final),kutwa bingwa wa Ligi ya Vodacom na kufikia hatua ya 16 bora kwenye mashindano wa Kombe la Shirikisho Africa,sote ni mashahidi wa zile jitihada zake binafsi zilizokuwa mara kwa mara zikibadili matokeo ya Simba yaliyokuwa yanaelekea kuwa hasi na kuwa chanya ghafla.
Binafsi pamoja na kuwa na itikadi ya mlengo wa opposite na Simba lakini nilikuwa namkubali sana Marehemu, lakini najiuliza je kuitoa katika mpango wa kutumika jezi No. 30 iliyokuwa inavaliwa ndo kitu pekee walichoweza kufanya kwa aliyekuwa mchezaji wao mahiri ambao wenyewe walimbatiza jina la "jembe"?
Iliniwia vigumu kuamini kuwa Simba ilishindwa kutoa siyo tu rambirambi bali hata Mwakilishi anayeeleweka kutoka katika ngazi ya juu ya uongozi kuambatana na mwili wa Marehemu katika safari yake ya mwisho humu Duniani,najiuliza hivi kama Viongozi kadhaa wa juu to mention few Nyange na Rage pasipo ulazima wowote waliweza kuambatana na Mafisango alipokuwa hai na team kwenda Shandy kiasi cha kushindwa kuwa accomodated na kulazimika kulala kwenye makochi reception walishindwa nini kwenda na mwili wa Marehemu mpaka Kinkola?,au ndo zile za kujuana wakati wa raha tu wakati wa shida atajijua mwenyewe na familia yake.....haya na suala la rambirambi nalo.....ni aibu kwa Club kama Simba ambayo dhahiri inaonyesha ndo team iliyoongoza kwa mapato katika mchezo wa Soka hapa Tanzania kushindwa kupeleka hata senti 5 kwa familia ya Marehemu kama rambirambi,na je ziko wapi zile rambirambi zilizotolewa na wadau mbalimbali tokea ulipotangazwa msiba ule mpaka pale TCC tulipokuwa tunamuaga "Jembe"? kwanini hata zile basi hazikuwakilishwa kwa familia ya Marehemu? haya si ndo yaleyale ya kina Mtitu,JB,Ray na wengineo wa Kamati ya msiba wa Kanumba na rambirambi zake.
Kwanini lakini sisi binadamu tunakuwa hatuna uoga na Mwenyezi MUNGU kabisa?
Haya hata wiki 2 hazijaisha tayari viongozi,wanachama na mashabiki wa Simba wameshasahau msiba wa "Jembe" lao na sasa wako kwenye maandalizi kabambe ya kuangusha bonge la sherehe la kusherehekea mafanikio yaliyochangiwa na Marehemu,hivi kweli kwa mwenendo huu nikisema vilio vyao vya siku ile pale TCC vilikuwa ni vya kinafiki kuna mtu anaweza kunibishia?
Nawasilisha.