Tegelezeni
JF-Expert Member
- Dec 31, 2009
- 268
- 124
Kwa mujibu wa Takwimu ya mwaka 2002 Tanzania ina idadi ya watu wapatao Milioni 34, na kwa idadi hiyo, idadi ya wanawake ipo milioni 17 na ile ya wanaume ipo Milioni 16. Mpaka hapo kuna ziada ya idadi ya wanawake inayokadiriwa kufikia milioni 1. Hata hivyo inasemekana hadi kufikia mwaka 2010, Tanzania inakadiriwa kuwa na idadi ya watu milioni 40, ambapo idadi ya wanawake inakadiriwa kufikia milioni 22 na ile ya wanaume inakadiriwa kufikia 18. Na katika idadi hiyo ya wanaume milioni 18, kuna zaidi ya asilimia 20 ya watoto wa kiume ambao wana umri chini ya miaka 15 na bado ni kula kulala, achilia mbali wazee wastaafu ambao hawana nguvu za kufanya kazi tena na bila kuwasahau wale wanaume ambao wameamua kuwa mashoga, na pia wagonjwa ambao nguvu zao za kiume zimekwenda harijojo. Ukitoa idadi hiyo unaweza kupata chini ya wanaume milioni 10 tu wanaoweza kuingia kwenye ndoa leo hii.
Je kwa upande wa wanawake hali ikoje? Kwa uzoefu tu, hebu tuangalie idadi ya vifo vya utotoni. Idadi ya watoto wa kiume wasiomudu kuvuka umri wa miaka 5 ni kubwa ukilinganisha na watoto wa kike, na hata wazee waliostaafu, wanawake ndio wanaoishi umri mrefu ukilinganisha na wale wa kiume. Hata ukitoa wanawake wasagaji na wamama wazee waliokula chumvi nyingi, bado idadi ya wanawake wanaoweza kuingia kwenye soko la ndoa ni kubwa ukilinganisha na idadi ya wanaume. Hata hivyo kiwango cha ukuaji cha watoto wa kike na wale wa kiume kinatofautiana sana, kwa sababu watoto wa kike huvunja ungo mapema ukilinganisha na wale wa kiume katika kubalehe, na hata kushiriki ngono, watoto wa kike huanza mapema ukilinganisha na wale wa kiume.
Hivyo basi hata kuolewa wanaowahi kuolewa ni watoto wa kike tofauti na wale wa kiume. Wakati wavulana siku hizi huoa wakiwa na umri wa kati ya miaka 30 mpaka 35, wasichana huanza kuolewa wakiwa na umri wa miaka 15 na kuendelea. Hii inaonesha kwamba soko la wanawake katika kuolewa linazidi kuwa na ushindani mkubwa kutokana na idadi yao kuwa kubwa ukilinganisha na idadi ya wanaume hivi sasa. Leo hii iwapo utamuuliza msichana kama yuko tayari kuolewa uke wenza au mitala atakwambia, "over my dead body" lakini akifikisha umri wa miaka 35, unaweza hata kumsikia akisema, "ngoja nitafute hata mume wa mtu nizae naye" lakini akishazaa na huyu mume wa mtu, kisha akamwambia kuwa angependa amuoe, ombi hilo litakubaliwa haraka sana, kile kiapo cha "over my dead body" hakipo tena. Kiapo kitakuwaje na nafasi wakati ushindani umekuwa ni mkubwa!
Hili jambo liko complex, na ndio maana nawauliza ninyi wanawake hivi mtaoleana nani, maana kila uchao ukienda mahospitalini wanafyatuliwa watoto wa kike wengi ukilinganisha na wale wa kiume achilia mbali wale wanaozaliwa huko majumbani………………… kazi ipo!
Je kwa upande wa wanawake hali ikoje? Kwa uzoefu tu, hebu tuangalie idadi ya vifo vya utotoni. Idadi ya watoto wa kiume wasiomudu kuvuka umri wa miaka 5 ni kubwa ukilinganisha na watoto wa kike, na hata wazee waliostaafu, wanawake ndio wanaoishi umri mrefu ukilinganisha na wale wa kiume. Hata ukitoa wanawake wasagaji na wamama wazee waliokula chumvi nyingi, bado idadi ya wanawake wanaoweza kuingia kwenye soko la ndoa ni kubwa ukilinganisha na idadi ya wanaume. Hata hivyo kiwango cha ukuaji cha watoto wa kike na wale wa kiume kinatofautiana sana, kwa sababu watoto wa kike huvunja ungo mapema ukilinganisha na wale wa kiume katika kubalehe, na hata kushiriki ngono, watoto wa kike huanza mapema ukilinganisha na wale wa kiume.
Hivyo basi hata kuolewa wanaowahi kuolewa ni watoto wa kike tofauti na wale wa kiume. Wakati wavulana siku hizi huoa wakiwa na umri wa kati ya miaka 30 mpaka 35, wasichana huanza kuolewa wakiwa na umri wa miaka 15 na kuendelea. Hii inaonesha kwamba soko la wanawake katika kuolewa linazidi kuwa na ushindani mkubwa kutokana na idadi yao kuwa kubwa ukilinganisha na idadi ya wanaume hivi sasa. Leo hii iwapo utamuuliza msichana kama yuko tayari kuolewa uke wenza au mitala atakwambia, "over my dead body" lakini akifikisha umri wa miaka 35, unaweza hata kumsikia akisema, "ngoja nitafute hata mume wa mtu nizae naye" lakini akishazaa na huyu mume wa mtu, kisha akamwambia kuwa angependa amuoe, ombi hilo litakubaliwa haraka sana, kile kiapo cha "over my dead body" hakipo tena. Kiapo kitakuwaje na nafasi wakati ushindani umekuwa ni mkubwa!
Hili jambo liko complex, na ndio maana nawauliza ninyi wanawake hivi mtaoleana nani, maana kila uchao ukienda mahospitalini wanafyatuliwa watoto wa kike wengi ukilinganisha na wale wa kiume achilia mbali wale wanaozaliwa huko majumbani………………… kazi ipo!