Medecin
JF-Expert Member
- Nov 29, 2011
- 7,900
- 21,311
mkuu nami naanza kuifanyia kazi falsafa yako.Mimi ilikuwa ni falsafa yangu, siwezi kuishi ama kufanya kazi nilipozaliwa!!! Kuna majungu na ujinga mwingi sana, huwezi kuendelea.
mkuu nami naanza kuifanyia kazi falsafa yako.Mimi ilikuwa ni falsafa yangu, siwezi kuishi ama kufanya kazi nilipozaliwa!!! Kuna majungu na ujinga mwingi sana, huwezi kuendelea.
Dunia ina mambo sana hii!Ukoo umeenda mbali, wengine tukikusimulia ya ndani ya familia ya ndugu wa tumbo moja, wazazi kupendelea waovu na kuungana nao kuhujumu wengine wanaoonekana "wanajidai wako vizuri" hutakaa uamini. Tenda wema uende zako.
Ni kweli Gyole, upo sahihi kabisaMambo ya ndugu sometime ovyooo sana, fata yako mkuu
Tenda wema uende zakoMiaka kadhaa iliyopita ndugu yetu katika ukoo alipata ajali mbaya ya barabarani na ilihitajika matibabu ya dharura lakini yenye umakini, na kama mnavyojua matibabu ya umakini kwa nchi hii ni yakulipia. Ndugu tulikusanyana ili kila mtu aweze kutoa mchango wake kufanikisha matibabu hayo.
Michango ilikua ya kusuasua sana, na kwakweli kasi ya utolewaji wake ilikua hailingani na mahitaji ya udharura ya mgonjwa, kwani baada ya muda mrefu wa kikao na kuhamasishana bado hela zilizopatikana zilikua kidogo na zisingeweza kufanya mgonjwa apelekwe theater.
Nilipoona mambo yako hivyo na hisia za maumivu anazopata mgonjwa nikaanza kujitolea kutangaza kuchangia kiasi kikubwa, baada ya sekunde chache nikaungwa mkono na ndugu wengine watatu waliochangia kiasi kikubwa na baada ya muda mfupi pesa ya matibabu ikapatika.
Siku ileile nikapata wito kutoka kwa mama yangu mzazi kua kesho yake niende kwake ananiita, na mimi nikaamua kwenda siku ileile bila kusubiri kesho. Nilipofika alinionya sana kwa kitendo nilichofanya cha 'kutangaza' kutoa pesa vile mbele ya kikao japo kilikua cha wanandugu. Akanambia watu sio wazuri mwanangu japo ni ukoo wenu, na maneno meengi ambayo niliona kama maneno ya kizee tu. Risala ilikua ndefu na yenye kunisisitiza lakini mimi nilimsikiliza Bi mkubwa kama ada tu huku yakiingia sikio moja na kutokea jingine
Wiki moja baadae nilishangaa baada ya kukutana hospitali(mgonjwa alikua kashafanyiwa oparation) na mmoja kati ya wale ndugu waliotoa mchango mkubwa, akaniambia baba yake hakufurahishwa na kitendo cha yeye kujitolea 'hadharani' kutoa mchango. Akamwambia bora angefanya siri au angelipa moja kwa moja hospitali kimyakimya. Japo sikumwambia kua na mimi nilikabiliwa na hali kama yake lakini wote tukakubaliana kua wazazi wanazeeka na visheria vyao ambavyo havisaidii jamii.
Miezi kama kumi na nane baadae nilipatwa na mshituko. Nilikua naongea na dada yangu binamu ambae alinimwagia maelezo meengi kuhusu tukio lile la kuchanga siku ile. Eti watu hawakulipokea vizuri japo walijifanya wameshangilia tulipokua tumetangaza michango yetu. Dada binamu akaanza kunitajia kwa majina ndugu ambao wanauwezo kuliko hata sisi tuliotoa michango mikubwa lakini kila mmoja alikua anasubiri atoe kiasi kilekile ambacho watu wote watapangiwa kutoa! Akanihadithia na maneno watu waliyokua wanayasema pembeni na baada ya kikao eti tunajifanya tunaazo na mengine mengi ya kebehi na kuvunja moyo sana!
Kipindi kirefu kilikua kimepita toka mchango ule na yale mazungumzo na dada binamu lakini kwakweli niliumia sana kwa maneno yale na nikiri yaliniathiri sana na yalinibadilisha kabisa mtazamo na approach yangu kwenye shughuli za kifamilia. Nilikua nahisi watu hawaoni mahitaji ya watu kwenye ukoo lakini unashangaa huyo unaedhani anauhitaji badala akufuata umpe ramani za michongo ya town yeye anakusema unapofanya kitu positive! Najiuliza hivi ni ukoo wetu tu ndio tuko hivyo au ndugu zangu nanyie mshawahi ku experince kitu kama hicho?
Thanks mkuuTenda wema uende zako
Ombeni mfunge kuondoa hiyo laana.Unaweza ukawa tajiri lakini ukawa mfungwa ktk mambo muhimu kiasi kwamba huna uhuru hata na mali zako.Anahitajika mtu asimame kuwaokoa ninyi ktk giza hilo.Kataeni muanze kutoka ktk wimbi hilo muifikie nchi ya ahadi.Zoezi la kutoka si lelemama.Inahitajika uvumilivu pia usiwe na hasira.Miaka kadhaa iliyopita ndugu yetu katika ukoo alipata ajali mbaya ya barabarani na ilihitajika matibabu ya dharura lakini yenye umakini, na kama mnavyojua matibabu ya umakini kwa nchi hii ni yakulipia. Ndugu tulikusanyana ili kila mtu aweze kutoa mchango wake kufanikisha matibabu hayo.
Michango ilikua ya kusuasua sana, na kwakweli kasi ya utolewaji wake ilikua hailingani na mahitaji ya udharura ya mgonjwa, kwani baada ya muda mrefu wa kikao na kuhamasishana bado hela zilizopatikana zilikua kidogo na zisingeweza kufanya mgonjwa apelekwe theater.
Nilipoona mambo yako hivyo na hisia za maumivu anazopata mgonjwa nikaanza kujitolea kutangaza kuchangia kiasi kikubwa, baada ya sekunde chache nikaungwa mkono na ndugu wengine watatu waliochangia kiasi kikubwa na baada ya muda mfupi pesa ya matibabu ikapatika.
Siku ileile nikapata wito kutoka kwa mama yangu mzazi kua kesho yake niende kwake ananiita, na mimi nikaamua kwenda siku ileile bila kusubiri kesho. Nilipofika alinionya sana kwa kitendo nilichofanya cha 'kutangaza' kutoa pesa vile mbele ya kikao japo kilikua cha wanandugu. Akanambia watu sio wazuri mwanangu japo ni ukoo wenu, na maneno meengi ambayo niliona kama maneno ya kizee tu. Risala ilikua ndefu na yenye kunisisitiza lakini mimi nilimsikiliza Bi mkubwa kama ada tu huku yakiingia sikio moja na kutokea jingine
Wiki moja baadae nilishangaa baada ya kukutana hospitali(mgonjwa alikua kashafanyiwa oparation) na mmoja kati ya wale ndugu waliotoa mchango mkubwa, akaniambia baba yake hakufurahishwa na kitendo cha yeye kujitolea 'hadharani' kutoa mchango. Akamwambia bora angefanya siri au angelipa moja kwa moja hospitali kimyakimya. Japo sikumwambia kua na mimi nilikabiliwa na hali kama yake lakini wote tukakubaliana kua wazazi wanazeeka na visheria vyao ambavyo havisaidii jamii.
Miezi kama kumi na nane baadae nilipatwa na mshituko. Nilikua naongea na dada yangu binamu ambae alinimwagia maelezo meengi kuhusu tukio lile la kuchanga siku ile. Eti watu hawakulipokea vizuri japo walijifanya wameshangilia tulipokua tumetangaza michango yetu. Dada binamu akaanza kunitajia kwa majina ndugu ambao wanauwezo kuliko hata sisi tuliotoa michango mikubwa lakini kila mmoja alikua anasubiri atoe kiasi kilekile ambacho watu wote watapangiwa kutoa! Akanihadithia na maneno watu waliyokua wanayasema pembeni na baada ya kikao eti tunajifanya tunaazo na mengine mengi ya kebehi na kuvunja moyo sana!
Kipindi kirefu kilikua kimepita toka mchango ule na yale mazungumzo na dada binamu lakini kwakweli niliumia sana kwa maneno yale na nikiri yaliniathiri sana na yalinibadilisha kabisa mtazamo na approach yangu kwenye shughuli za kifamilia. Nilikua nahisi watu hawaoni mahitaji ya watu kwenye ukoo lakini unashangaa huyo unaedhani anauhitaji badala akufuata umpe ramani za michongo ya town yeye anakusema unapofanya kitu positive! Najiuliza hivi ni ukoo wetu tu ndio tuko hivyo au ndugu zangu nanyie mshawahi ku experince kitu kama hicho?
Hahahahaa, hapanaBila shaka unatoka kanda ya nyanda za juu kusini.
Dah sawa mkuuOmbeni mfunge kuondoa hiyo laana.Unaweza ukawa tajiri lakini ukawa mfungwa ktk mambo muhimu kiasi kwamba huna uhuru hata na mali zako.Anahitajika mtu asimame kuwaokoa ninyi ktk giza hilo.Kataeni muanze kutoka ktk wimbi hilo muifikie nchi ya ahadi.Zoezi la kutoka si lelemama.Inahitajika uvumilivu pia usiwe na hasira.
Hayo yapo kwenu tu mkuu.