Jamaa yangu wa karibu alie Arusha ananiambia kwamba viongozi wengi wa CCM na serikali wameshafika kwa babu wa Loliondo kupata matibabu. Naambiwa hata mkwere na baadhi ya mawaziri wake wameshapatiwa huduma na babu na ndio maana baada ya tangazo la waziri wa afya kukataza matibabu ya babu, mkuu wa mkoa wa Arusha alisema haiwezekani kukatisha huduma. Hivi inawezekana haiwezekani kwasababu hata mkwere anaamini kikombe cha babu kitarefusha maisha yake? NAsikia hata mfipa nae si mzima, yawezekana wamekubali yaishe na kujisalimisha kwa babu Ambilikile? Hata babu alikaririwa na magazeti mengi akisema vigogo wanaenda kwake kwa siri. Wenye data, tafadhali wekeni wazi orodha ya vigogo hawa wanaojipatia huduma ya shillingi 500.