Hivi ni kwanini hakuna waziri mkuu aliyekuja kuwa Rais wa Tanzania?

Binafsi nafikiri hakuna sheria inayoamua juu ya hili...ila usipotegemea LOWASSA anaweza kuvunja hu utaratibu....
 
Jibu rahisi ni kwamba, waziri mkuu huchaguliwa na mtu mmoja (rais) na wengi huchagua yule anedhani anafanana nae kimtazamo, wakati rais wa nchi huchaguliwa na watu wengi(wnanchi) na wnanch wanapenda mabadiliko kwani uzoefu unaonyesha kila rais ansetoka madarakani huwa na mapungufu mengi hivyo kuhitaji mtu mpya wa kusahihisha na sio kuleta sura inayofanana kiutendaji na raisi aliyekuwepo madarakani.

Kwa mfao, huyo Lowassa unayemsema hawezi kuwa chaguo la wengi kutokana na kashfa zinazomkabili alipokuwa Waziri Mkuu wa Jk.

Kwa mfumo wa sasahivi Raisi wa nchi hachaguliwi na wengi anachaguliwa na wajumbe wa NEC wa CCM ukiwa na hela za kutosha kama Lowasa za Kuwahonga unakuwa raisi wa nchi bila shida
 
Ukiachilia Nyerere, hakuna waziri mkuu mwingine wa Tanzania ambae alifanikiwa kuja kuwa Rais wa nchi, kwa mfano Kawawa, Msuya, Salim, Warioba, Malecela, Sumaye, Sokoine, na kuna kila dalili kwamba at least kwa uchaguzi mkuu ujao 2015, CCM haitamsimamisha mgombea Urais kutokana na Mawaziri wakuu waliopita.

Sababu ya hili ni nini - je ni mpango maalum (kama vile unwritten principle) au huwa inatokea tu?

Mkuu mbona Salim alishurutishwa mara mbili na Kambarage, lakini aka-decline offer - wengine siwezi kuwazungumzia.
 
dah, kumbe wanapeana vyeo bila kuangalia uwezo? Sasa mbona cheo cha waziri mkuu ni kikubwa na kinahitaji mtu mwenye uwezo mkubwa sana kiuongozi
 

Sababu ya hili ni nini - je ni mpango maalum (kama vile unwritten principle) ......?

Ukistaafu uwaziri mkuu kuna masulufu unapewa kila mwezi/mwaka vivyo hivyo ukistaafu urais kuna masurufu unapewa kila mwezi/mwaka...sasa inaonekana siyo vyema mtu mmoja alipwe masurufu kubwa namna hiyo wakati wazee wengine wanataabika...kumbuka nimekupa unwritten Sababu.
 
Kuna hoja deep sana ya mchangaji mmoja humu kwamba ili Waziri Mkuu aweze kuwa Rais wa Tanzania, ni lazima kwanza ajiuzulu Uwaziri Mkuu kama Nyerere alivyofanya. Tafakari, chukua hatua.
 
Mkuu mbona Salim alishurutishwa mara mbili na Kambarage, lakini aka-decline offer - wengine siwezi kuwazungumzia.
Kilichotokea ni kwamba licha ya juhudi za Kambarage za kumweka Salim kama mgombea mwaka 1985, forces za CCM zilimshinda Mwalimu, hasa upande wa Zanzibar. Mwaka 1995 ndio alikataa wazo la kujaribiwa tena. Tunamsema sana mwalimu kwamba alikuwa dictator na mambo kama hayo lakini tunasahau kwamba Mwalimu hakuwa mtu wa kulazimisha kila jambo, vinginevyo viongozi waliomfuatia wangekuwa na fursa katika nyakazi zile za Nyerere, hakuna ambae angewazuia kuweka mtu wao.
 
Uwaziri mkuu Tanzania ndo kazi ya kubeba lawama...
unabeba lawama za Rais pia
mfano Kawawa alibeba lawama zote za Nyerere
Sumaye akabeba lawama zote za Mkapa na kadhalika

Watu huwa wanaogopa kum attack Rais direct ..so wanapeleka lawama
kwa PM ....so by the time uchaguzi unakuja Pm anakuwa kachafuka vya kutosha
 
Nadhani kuna watanzania wengi wenye uwezo wanaoweza kuwa marais na si lazima mawaziri wakuu wa zamani. Simpo. Hakuna anayewazuia kama Nyerere hakuzuiliwa kwanini wao?

Unazungumziaje mawaziri wakuu wengi kuwa wakristo huku muislam akiwa wachache kama Rashid?
 
Ngoja na mimi nitoe mawazo yangu. Sababu ya kwanini mawaziri wakuu huwa hawa pewagi nafasi ya kupeperusha bendera ya chama kwenye chaguzi za uraisi ni kwa sababu mtu ukisha kuwa waziri mkuu tayari wapinzani wako wana assume utautafuta uraisi kwa hiyo wanajiandaa mapema. Kwa maana hiyo usikute hata sasa kuna watu washa jiandaa kupambana na Pinda iwapo ata gombea. Hii inatokana na mentality ya sisi wanadamu kuwa mtu akisha pata nafasi fulani hutaka cha juu zaidi na kwetu baada ya uwaziri mkuu ni uraisi (husikii mtu akililia au kugombania umakamo wa raisi kwa sababu ni nafasi isiyo na nguvu nyingi). Hii inamaana hata leo hii ikatokea bahati bin vuu mlala hoi kama mimi akateuliwa kuwa waziri mkuu tayari maadui au wataka uraisi wata assume moja kwa moja na mimi nitausaka uraisi. Hii nadharia si bure kwani mpaka sasa historia inaonyesha kila alieukwaa uwaziri mkuu kaishia kuutafuta uraisi (ukimuacha Kawawa na pia Sokoine aliefariki dunia kabla ya kupitia chaguzi kuu yoyote).
 
Kweli wewe mende0! Hilo la udini wako unalileta baada ya kuishiwa hoja. Nadhani kuna haja ya kujadili issues badala ya personalities otherwise kujadili watu kunawafaa wenye akili ndogo na mtindio wa mawazo so to speak. Jaribu kutumia ubongo kidogo uangalie hoja inataka nini. Kama una hoja ya udini peleka huko inakofaa lakini si hapa. Maisha mabaya ya watanzania hayaangalii dini. Ni kipofu na taahira anaweza kuunganisha hoja hii na udini. Pia ni muhimu kuficha ujuha kuliko kuuanika. Ni ushauri tu.
Unazungumziaje mawaziri wakuu wengi kuwa wakristo huku muislam akiwa wachache kama Rashid?
 
Ngoja na mimi nitoe mawazo yangu. Sababu ya kwanini mawaziri wakuu huwa hawa pewagi nafasi ya kupeperusha bendera ya chama kwenye chaguzi za uraisi ni kwa sababu mtu ukisha kuwa waziri mkuu tayari wapinzani wako wana assume utautafuta uraisi kwa hiyo wanajiandaa mapema. Kwa maana hiyo usikute hata sasa kuna watu washa jiandaa kupambana na Pinda iwapo ata gombea. Hii inatokana na mentality ya sisi wanadamu kuwa mtu akisha pata nafasi fulani hutaka cha juu zaidi na kwetu baada ya uwaziri mkuu ni uraisi (husikii mtu akililia au kugombania umakamo wa raisi kwa sababu ni nafasi isiyo na nguvu nyingi). Hii inamaana hata leo hii ikatokea bahati bin vuu mlala hoi kama mimi akateuliwa kuwa waziri mkuu tayari maadui au wataka uraisi wata assume moja kwa moja na mimi nitausaka uraisi. Hii nadharia si bure kwani mpaka sasa historia inaonyesha kila alieukwaa uwaziri mkuu kaishia kuutafuta uraisi (ukimuacha Kawawa na pia Sokoine aliefariki dunia kabla ya kupitia chaguzi kuu yoyote).

Well said.
 
Kweli wewe mende0! Hilo la udini wako unalileta baada ya kuishiwa hoja. Nadhani kuna haja ya kujadili issues badala ya personalities otherwise kujadili watu kunawafaa wenye akili ndogo na mtindio wa mawazo so to speak. Jaribu kutumia ubongo kidogo uangalie hoja inataka nini. Kama una hoja ya udini peleka huko inakofaa lakini si hapa. Maisha mabaya ya watanzania hayaangalii dini. Ni kipofu na taahira anaweza kuunganisha hoja hii na udini. Pia ni muhimu kuficha ujuha kuliko kuuanika. Ni ushauri tu.

kwa hiyo umekubali mfumo kristo unafaa kutawala dunia nzima?
 
Back
Top Bottom