Mheshimiwa Mbowe ni muumini mzuri sana wa uhuru wa vyombo vya habari na hii inajidhihirisha katka namna ambavyo ameliacha gazeti lake la Tanzania Daima kufanya kazi yake bila ya kuingiliwa. Policy hii ya hands off, ni nzuri na ni nguzo muhimu sana ya uhuru wa vyombo vya habari hasa katika nchi za dunia ya tatu ambako wamiliki wana nguvu sana. Hii ililipa heshima gazeti la Tanzania Daima na nina hakika mauzo yake yaliongezeka sana.
Kwa bahati mbaya sana aina hii ya utawala imetumiwa vibaya na mawakala wa ufisadi na washabiki wa siasa za kihafidhina ambao wametanda katika news room ya gazeti hili na sasa gazeti hili limegeuka kuwa ni mdomo wa mafisadi, sauti ya ukinzani usio na tija dhidi ya serikali na hasa Rais wa nchi na upotoshaji wa kijinga sana. Ukisoma makala za Kibanda, Ngurumo na wachangiaji wengine utaona kwamba gazeti hili limepoteza mvuto, weledi na kuaminika kwake. Sasa hivi ukiona habari katika gazeti hili unajiuliza mara mbili mbili juu ya kuaminika kwake. Hali hii sasa inaonekana kuwakera hata baadhi ya watumishi wa gazeti hili, na mfano mzuri ni makala ya Happiness Katabazi ya gazeti la tarehe 3 Julai, 2012 ambayo alielezea juu ya mgomo wa madaktari. Alishutumu jinsi makala zake mbili ambazo kimsimamo zinatofautiana na 'watawala' wa news room ya gazeti walivyoziminya kiasi cha kuhisi kwamba hata hiyo nayo isingetoka.
Kama hili linamtokea mwenzao ambaye msimamo wake au fikra zake ni tofauti, vipi kwa wengine?
Swali langu ni je, Mheshimiwa Mbowe haya anayajua?
Kwa bahati mbaya sana aina hii ya utawala imetumiwa vibaya na mawakala wa ufisadi na washabiki wa siasa za kihafidhina ambao wametanda katika news room ya gazeti hili na sasa gazeti hili limegeuka kuwa ni mdomo wa mafisadi, sauti ya ukinzani usio na tija dhidi ya serikali na hasa Rais wa nchi na upotoshaji wa kijinga sana. Ukisoma makala za Kibanda, Ngurumo na wachangiaji wengine utaona kwamba gazeti hili limepoteza mvuto, weledi na kuaminika kwake. Sasa hivi ukiona habari katika gazeti hili unajiuliza mara mbili mbili juu ya kuaminika kwake. Hali hii sasa inaonekana kuwakera hata baadhi ya watumishi wa gazeti hili, na mfano mzuri ni makala ya Happiness Katabazi ya gazeti la tarehe 3 Julai, 2012 ambayo alielezea juu ya mgomo wa madaktari. Alishutumu jinsi makala zake mbili ambazo kimsimamo zinatofautiana na 'watawala' wa news room ya gazeti walivyoziminya kiasi cha kuhisi kwamba hata hiyo nayo isingetoka.
Kama hili linamtokea mwenzao ambaye msimamo wake au fikra zake ni tofauti, vipi kwa wengine?
Swali langu ni je, Mheshimiwa Mbowe haya anayajua?