Hivi kwa nini CUF haina gazeti lake?

Zak Malang

JF-Expert Member
Dec 30, 2008
5,404
234
Wiki iliyopita nilimwona katika TV Profesa Lipumba akiwa katika mkutano wa waandishi wa habari na baadhi ya viongozi wa vyama vya siasa ulioitishwa na Idara ya Maelezo kutoa maelekezo namna ya kurpoti habari katika kipindi cha kampeni.

Akizungumza katika kongamano hilo la siku moja Lipumba, pamoja na mambo mengine, alisisitiza umuhimu kwa vyombo vya habari kufuata maadili na kuandika yaliyo ya kweli, bila upendeleo na ushabiki wa kisiasa.

Tatizo langu na hawa CUF ni kwamba ni zaidi ya miaka 18 sasa tangu chama kingie mambo ya siasa, inakuwaje hakina hata gazeti lake, achilia mbali radio au TV? Mpaka lini chama hichi kitategemea huruma ya vyombo vya habari binafsi (na vya serikali) kuandika habari ya chama hicho bila upendeleo?

Si dhani kama ni tatizo la pesa kwani CUF imekuwa inapata mamilioni ya fedha kila mwezi kama ruzuku lakini hawakuwa na mpango wowote wa kuanzisha angalau hata gazeti – au hata mmoja wa viongozi wake wenye fedha kufanya hivyo.

Kuanzisha gazeti hakuhitaji fedha nyingi sana – Kubenea, mwaka 2006 aliweza kuanzisha gazeti lake na sasa linauza nakala nyingi kila toleo kupita magazeti yote hapa nchini kuachilia yale ya udaku.

Chadema wana gazeti lao – Tanzania Daima – ingawa inaejulikana kama ni la Freeman Mbowe, mwenyekiti wa chama hicho.

Lakini kama tunavyoona sasa hivi, gazeti hilo linakisaidia chama hicho kutokana na propaganda za vyombo vya habari vya serikali na chama tawala pamoja na vile vinavoonekana kununuliwa na chama tawala. Na hivi sasa nasikia linauzwa kama njugu – bila shaka kutokana na kuandika ukweli kuhusu matukio mbali.

CUF ina viongozi wasomi, na waliobobea katika masuala ya siasa na kufanya publicity. Vipi kasoro yao hii hawaioni? Profesa, Maalim, hamad Rashid na Jussa – hela mnapeleka wapi? Msikae kulalamika tu – kuweni na chombo chenu.
 
Al-Nuur linatoka kila Ijumaa

Ni kweli, An Nur huandika habari nyingi kukitetea chama hicho na ndo maana kinaitwa chama cha Kiisilamu. Lakini wangekuwa na gazeti lao, nembo ya Uisilamu wangeweza kuikwepa.

Lakini mimi naona viongozi wakuu wa CUF wanatafuna tu fedha za ruzuku na ndo maana hao hao wameng'ang'ania madarakani miaka nenda miaka rudi.
 
Hawana gazeti rasmi la chama, hilo linawapigia debe tu. Ni uvivu wa kufikiri.
 
Halafu utasikia baadhi ya wafuasi wao wakilalalmika eti vbyombo vbya habari vinaichukia CUF bila sababu na ndo maana havikipi kipaumbele katika habari zao. Kuepukana na hili, si waanzishe tu gazeti lao wenyewe? Nakumbuka kulikuwapo gazeti la Fahamu ambalo lilikuwa linawapigia debe mwaka 2005 -- ikawaje tena?
 
Al Nuur...ishu ya nembo ya udini si tatizo, mbona wakati wanamkaribisha Mwera wa Tarime alisalimia 'ASALAAM ALEKUUM'....
 
Alichozungumza Pr Lipumba ni uhuru na maadili ya waandishi, usibadilishe mada,kuwa na gazeti lake ama hawana ni miongoni mwa mipango yao, kwani Nipashe ni gazeti la chadema? mbona wameipa kipaumbele sana,majira je? mwananchi je? yote hayo wameipa chadema kipaumbele,kama watatoa habari za cuf basi ni kwa uchahe sana na tena page za ndani huko. na mdau mmoja umezungumza kuhusu gazeti la kubeinea,nani asiejua gazeti la kubeinea ni la nani,kumbuka mpaka kesi alikua nayo mhakamani.. fuatili uzuri chanzo cha gazeti hilo...
 
Alichozungumza Pr Lipumba ni uhuru na maadili ya waandishi, usibadilishe mada,kuwa na gazeti lake ama hawana ni miongoni mwa mipango yao, kwani Nipashe ni gazeti la chadema? mbona wameipa kipaumbele sana,majira je? mwananchi je? yote hayo wameipa chadema kipaumbele,kama watatoa habari za cuf basi ni kwa uchahe sana na tena page za ndani huko. na mdau mmoja umezungumza kuhusu gazeti la kubeinea,nani asiejua gazeti la kubeinea ni la nani,kumbuka mpaka kesi alikua nayo mhakamani.. fuatili uzuri chanzo cha gazeti hilo...

Yote unayosema huenda ni kweli. sasa kama magazeti hayo yamekipa kisogo CUF, sasa kifanyike nini? Hakuna sheria ya kulazimisha gazeti kuandika habari zako hata kama huko ni kwenda kinyume cah maadili, au hata kwa pesa, kwani anayo hiari ya kukubali au kukataa, na si lazima atoe sababu. Kwa gazeti kuandika habari ya chama fulani ni hisani tu na siyo lazima.

Inawezekana, kwa mfano, wamegundua kwamba wakiandika habari za CUF mauzo yanapungua. Nasema kwa mfano tu.

Swali linabakia pale pale -- kwamba kuepukana na yote haya si bora CUF ingekuwa na gazeti lake? Ingekata kabisa mzizi wa fitina. Au unayo sababu ya msingi ya chama hicho kutokuwa na gazeti?
 

msiseme kwa kuwa manataka kusema tu tupeni proof, kama ya kusema Tanzania daima ni ya chadema si sawa sote tunajua ni ya freemedia uhusiano wake pengine mwenyekiti wake ndio mmliki sasa tunaomba mtutajie wamilikiwa hiyo al huda na al nurr acheni unafiki Mungu anapenda wanaosema ukweli na hakuna dhabi kubwa kama unafiki.
 
msiseme kwa kuwa manataka kusema tu tupeni proof, kama ya kusema Tanzania daima ni ya chadema si sawa sote tunajua ni ya freemedia uhusiano wake pengine mwenyekiti wake ndio mmliki sasa tunaomba mtutajie wamilikiwa hiyo al huda na al nurr acheni unafiki Mungu anapenda wanaosema ukweli na hakuna dhabi kubwa kama unafiki.

Wewe ndiyo mnafiki mkubwa hivi hujui magazeti hayo yanashabikia chama gani hapa nchini? suala la kutaja wamiliki si hoja ya msingi , hoja hapa je hao wamiliki wana sera gani? Siku zote tunaona hoja za magazeti hayo ni kuipigia debe CUF, kama unabisha ubishe tu.
 
al nuur na al huda ndiyo vijarida vya cuf ndiyo maana haiwezi kuhangaika kuwa na kijarida kingine maana vilivyopo ni vya kidini na cuf ni taasisi ya kidini zaidi
 
Al huda na Al-Nuur kila Ijumaa haya ni CUF! Huwa yanagawiwa misikitini baada ya swala Ijumaa.
 
Ninawaonea huruma sana na fikra zetu watanzani kweli akili mgando.poleni sana
 
Back
Top Bottom