everybody
JF-Expert Member
- Oct 30, 2010
- 337
- 103
Juzi tu tumesikia kwamba msafara wa VP umepata ajali na kwa taarifa nilizosoma leo kwenye gazeti ni kwamba askari polisi wawili wamefariki na wengine hali zao ni mbaya hospitali. Nimekaa nikajiuliza hivi kuna umuhimu kwa haya magari yanayosindikiza viongozi kukimbizwa kiasi wanavyofanya kwa sasa? Je kuna hatari gani ndani ya Tanzania yetu hii ya leo inayowafanya wawe wanakimbizana kiasi hicho?
Kwa maoni yangu sasa hawa viongozi wajifunze kutokana na tukio hili lililosababisha vifo vya watu ambao pengine kuna ndugu zao waliokuwa wanawategemea na kwa sasa wamebaki wakiwa. Sioni umuhimu wowote wa hii misafara kutimua mbio kama wanakimbia vita au ugaidi!
Kwa maoni yangu sasa hawa viongozi wajifunze kutokana na tukio hili lililosababisha vifo vya watu ambao pengine kuna ndugu zao waliokuwa wanawategemea na kwa sasa wamebaki wakiwa. Sioni umuhimu wowote wa hii misafara kutimua mbio kama wanakimbia vita au ugaidi!