Hivi huyu rafiki yangu anaweza kuwa mtu wa aina gani?

Mmea Jr

JF-Expert Member
May 20, 2016
551
1,222
Habari zenu wakuu?? Natumaini mpo salama kabisa. Okay mimi siyo muanzisha mada humu mara kwa mara ila mara nyingi nimekuwa napenda sana kusoma tu mada, story hata visa mbalimbali viinavyolweta na baadhi ya wadau wenzetu na kama itatokea nikaguswa sanaa basi mara moja moja huwa natupia comment ili mambo yawe swadakta kabisaa.

Sasa bwana mimi mwenzenu nina rafiki yangu (mwanaume ) ambaye huwa tunapeana michongo ya hapa na pale ili maisha yasonge, japo urafiki wetu una muda kidogo lakini mimi mwenzenu kuna kitu huwa sikielewi juu ya huyu mtu, huyu jamaa kama hamna mishe yeye ni mtu wakuchill sanaa ndani mpaka kuna muda huwa namuuliza " we jamaa hivi kukaa ndani peke yako huchoki??" .. yeye atakujibu mbona kawaida tu mkuu .( Hanywi pombe, hashabikii mpira kabisaaaa hata draft siyo mchezaji ni mimo ndiyo huwa namvuta twende kijiweni tukapige danari maana nipo vizuri mno kwenye huu upande basi atakuja tu na kuwa mtazamaji )

Sasa tisa kumi kilichonifanya mpaka nije humu kuwauliza ni hili, ukiachilia mbali kukaa ndani muda mrefu pekee yake. Ana tabia ya kupenda sana kusikiliza muziki, ila sasa yeye usikilizaji wake ndiyo unaonishangaza sana na nakaona nije niwaulizeni . Yaani anaweza kuplay wimbo mmoja tu huo huo akausikiliza hata kwa masaa matano mfano kuna wimbo wa costa titch unaitwa big flexa hapa naandika nimemuacha ameuplay huu wimbo, lakini nje na hapo ni mwezi sasa amekuwa akiusikiliza huu huu non -stop hata kwenye simu yake kama utaangalia most played song ni huu huu nilioutaja hapa, kabla ya hapo alikuwa anausikiliza wimbo unaitwa Dwala lam msaanii anaitwa Dj ksb. Tisa kumi namjua vizuri tu lugha anayoifahamu vizuri ni kiswahili na kiingereza cha tia tia maji ila sasa hizi nyimbo anazozisikiliza ni za kizulu hivyo najua kabisa haelewi kiimbwacho humo. Miaka yake ni 27 kwa sasa.

Sasa je hii hali ni kawaida? Maana mimi najua humu kuna watu mbali mbali ambao pengine mmeweza kukutana na watu wa namna hii na mkaweza kuwaelewa bila shida, naombeni na mimi mnisaidie maana kuna wakati nahisi mwenzangu anapitia wakati mgumu lakini nimeshindwa kujua, lengo ni kujaribu kumsaidia huyu ndugu yangu.. au ili niweze kumuelewa.

Asanteni
 
Huyo ni mtu anayependa routine.

Anapenda mazingira anayoyajua, hapendi mapya.

Ndiyo maana hata muziki akipata anaopenda anakaa nao huo huo anaupiga mara nyingi.

Ndiyo maana anapenda kukaa ndani alipopazoea tu.

Hii inaweza kuwa dalili ya kuwa kwenye autism spectrum, au ni tabia yake tu.
 
Huyo ni mtu anayependa routine.

Anapenda mazingira anayoyajua, hapendi mapya.

Ndiyo maana hata muziki akipata anaopenda anakaa nao huo huo anaupiga mara nyingi.

Ndiyo maana anapenda kukaa ndani alipopazoea tu.

Hii inaweza kuwa dalili ya kuwa kwenye autism spectrum, au ni tabia yake tu.
Aloo na ndyo maana mimi jamiiforum napapenda sanaa , hebu ongezea maelezo kidogo. Inaonekana unaozoefu mkubwa na hawa watuu , hapa nimeanza kupata mwanga jee hii tabia haina madhara kweli kama mtu labda atakapokuja kuoa maana kwangu mimi naona kama siyo tabia ya kawaida hii
 
Hii tabia wakati mwingine inachangiwa na malezi kwa kiasi kikubwa, kuna wazazi wasiopenda kabisa watoto wao wakacheze mbali na nyumbani, hawa muda mwingi wa makuzi yao wanakuwa kwenye mazingira ya nyumbani pekee.

Hivyo hawa hata wakikua, wakaanza kujitegemea, kwasababu walishazoea mazingira ya nyumbani, kutokwenda mbali, kuzungukwa na waliowazoea kila siku, inakuwa ngumu kwao kuja ku adopt ukubwani, japo baada ya muda wengine huanza kubadilika taratibu.

Wengi aina hii mara nyingi hata confidence huwa hawana, wanakuwa wenye aibu, wasioweza hata kukaa mbele ya wengine, mara nyingi hupenda palipo na wengi, wao wawe nyuma tena ikibidi hata uwepo wao usitambulike, pia huwa na maneno machache waliotawaliwa na tabasamu la muda mfupi wakiongea vichache vyao.
 
Kuna kazi anayofanya au hana anashinda home siku nzima?
Mkuu kazi zetu sisi ni kujenga sasa msimu wa mvua umekuwa siyo msimu rafiki sana kwa shughuli zetu hizi basi ni wakati huu ndyo nilipokuja kulijua hilii juu ya rafiki yangu huyu wakati huu muda mrefu tumekuwa tukitumia akiba zetu kuweza kuishi kama ni kazi basi huwa moja moja sanaa
 
zama zimebadilika
FB_IMG_1685802289484.jpg
 
Hii tabia wakati mwingine inachangiwa na malezi kwa kiasi kikubwa, kuna wazazi wasiopenda kabisa watoto wao wakacheze mbali na nyumbani, hawa muda mwingi wa makuzi yao wanakuwa kwenye mazingira ya nyumbani pekee.

Hivyo hawa hata wakikua, wakaanza kujitegemea, kwasababu walishazoea mazingira ya nyumbani, kutokwenda mbali, kuzungukwa na waliowazoea kila siku, inakuwa ngumu kwao kuja ku adopt ukubwani, japo baada ya muda wengine huanza kubadilika taratibu.

Wengi aina hii mara nyingi hata confidence huwa hawana, wanakuwa wenye aibu, wasioweza hata kukaa mbele ya wengine, mara nyingi hupenda palipo na wengi, wao wawe nyuma tena ikibidi hata uwepo wao usitambulike, pia huwa na maneno machache waliotawaliwa na tabasamu la muda mfupi wakiongea vichache vyao.
Aisee nashukuru ushauri wako umenifungua pakubwa sana kwa kweli kwa maisha ya africa haswa hapa Tanzania kuishi hivi labda uwe na kiptao au umesoma sana kwamba chanzo cha mapato yako iwe mshahara au vyanzo vingine ambavyo havihiitaji uwepo wako ili kukupatia pesa . Maana kwa sehemu niliyopo ili mishe mishe zije lazima ujichanganye na watu, watu wajue nini unafanya na watakupata wapi sasa ukiwa unashinda ndani kila saa unafikiri itakuwaje. ??
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom