mabhuimerafulu
Member
- May 29, 2012
- 89
- 38
Jana nimesoma gazeti moja likimtaja Mkurugenzi wa Dawasco Bw Archard Mutalemwa nikashangaa; ni Mutalemwa yupi? Aliyekuwa anasambaza maji yasiyo na dawa (1993) wakati akiwa NUWA akaundiwa tume na kuthibitishwa ni kweli? Waziri wa Maji wakati huo alikuwa JK, afya akiwa Meghji.
Ni yule aliyesababisha NUWA kufunguliwa kesi na wakazi wa Sinza baada ya taarifa hizo? Wakazi hao walitetewa na Wakili (sasa marehemu Julius Ndyanabo)?
Ni yule ambaye akiwa NUWA ilikuwa inatuhumiwa kununua madawa ya maji yasiyofaa mara kwa mara na tuhuma za ubadhirifu lukuki?
Kama ni yeye basi muuzieni hayo mashirika ya DAWASCO na DAWASA maana sasa imedhihiri mashirika hayo ni kama mali yake. Cha ajabu nini mbona BWM alijiuzia Kiwira? Ni kweli hakuna mtaalam wa maji nchini mpaka Mutalemwa?
Atakuwa na kizizi kisichokuwa cha kawaida!
Ni yule aliyesababisha NUWA kufunguliwa kesi na wakazi wa Sinza baada ya taarifa hizo? Wakazi hao walitetewa na Wakili (sasa marehemu Julius Ndyanabo)?
Ni yule ambaye akiwa NUWA ilikuwa inatuhumiwa kununua madawa ya maji yasiyofaa mara kwa mara na tuhuma za ubadhirifu lukuki?
Kama ni yeye basi muuzieni hayo mashirika ya DAWASCO na DAWASA maana sasa imedhihiri mashirika hayo ni kama mali yake. Cha ajabu nini mbona BWM alijiuzia Kiwira? Ni kweli hakuna mtaalam wa maji nchini mpaka Mutalemwa?
Atakuwa na kizizi kisichokuwa cha kawaida!