The Khoisan
JF-Expert Member
- Jun 5, 2007
- 15,396
- 12,979
Hivi hii ya serikali nzima kuhamia kwenye mazishi ya wabunge imekaaje?? Personally nashindwa kuelewa kwa nini viongozi wote wakuu wa selikali wanaacha kazi na kutumia rasrimali zetu kuhudhuria mazishi. Nasema hivi kwa kuamini kabisa kuwa safari ya Rais , makamu, waziri mkuu au spika lazima serikali itaingia gharama. Au kuna kipengere chochote kwenye katiba kinachosema msiba wa mbunge ni msiba wa kitaifa?? Kwa mila na desturi zetu Waafrika ni uungwana kuwafariji na kuwapa pole wafiwa. Lakini sidhani kama ni lazima kila mtu asafiri kuyafuata mazishi kule yaliko bila kujali umbali na gharama.
- Je ni harari kwa jinsi serikali ilivyohandle msiba wa Mzee Sumari ambaye hakuwa na hadhi ya ubunge kwa vile hakuwahi kuapishwa au ndiyo kutafuta mtaji wa kisiasa.
- Hivi ikitokea mbunge mwingine akafa wiki ijayo, serikali zima itafunga tena safari kuhamia kwenye maziko mikoani??
- Kwa nini serikali haitumi viongozi wake kama mkuu wa mkoa au wilaya ambao wako eneo husika kuiwakilisha serikali?