Hivi hii ya serikali nzima kuhamia kwenye mazishi imekaaje?

The Khoisan

JF-Expert Member
Jun 5, 2007
15,396
12,979
Hivi hii ya serikali nzima kuhamia kwenye mazishi ya wabunge imekaaje?? Personally nashindwa kuelewa kwa nini viongozi wote wakuu wa selikali wanaacha kazi na kutumia rasrimali zetu kuhudhuria mazishi. Nasema hivi kwa kuamini kabisa kuwa safari ya Rais , makamu, waziri mkuu au spika lazima serikali itaingia gharama. Au kuna kipengere chochote kwenye katiba kinachosema msiba wa mbunge ni msiba wa kitaifa?? Kwa mila na desturi zetu Waafrika ni uungwana kuwafariji na kuwapa pole wafiwa. Lakini sidhani kama ni lazima kila mtu asafiri kuyafuata mazishi kule yaliko bila kujali umbali na gharama.
  • Je ni harari kwa jinsi serikali ilivyohandle msiba wa Mzee Sumari ambaye hakuwa na hadhi ya ubunge kwa vile hakuwahi kuapishwa au ndiyo kutafuta mtaji wa kisiasa.
  • Hivi ikitokea mbunge mwingine akafa wiki ijayo, serikali zima itafunga tena safari kuhamia kwenye maziko mikoani??
  • Kwa nini serikali haitumi viongozi wake kama mkuu wa mkoa au wilaya ambao wako eneo husika kuiwakilisha serikali?





attachment.php
 
Ulitaka wafanye jambo gani wakati sasa hivi hawana kitu cha kufanya.
 
Wengi wao wanatarajia kufa siku yoyote. Wangependa kuzikwa na kundi kubwa la watu, hivyo kuhudhuri kwenye mazishi ni kuwaita watu kwenye mazishi yao. Ila kwa vile mimi si wafu sitafungwa nira pamoja nao.
 
Acha Siasa, Unaposema Sumari hakuwa na hadhi ya ubunge unamaana gani?
 
Hawako economical ,
Hawana uchungu na pesa ya Tanzania,

Unafiki wetu ndio unaotufikisha hapa


Hakuna sababu ya serikali nzima kwenda msibani ni mwakilishi mmoja mmoja kutoka idara husika anatosha.

Hawa viongozi wetu:shock:
 
Lack of Confidence, walianza kama plan ya makinda kumuonyesha JK kwamba yeye ana strategy ya kuwabana Chadema, katika msiba wa Regia kwa kuwa walijua kwamba watu wengi sana watajitokeza kumzika Regia. Wakataka ku dilute issue ionekane watu wallijaa kwa sababu ya msiba wa mbunge kwa hiyo bunge na serikali ndio ionekane imefanya mambo. Hawakujua kwamba mungu hajaribiwi ndio maana akamuondoka Sumari immediately, sasa manunga ya embe na magamba wakabaki hawana jinsi bali kuonekana kwamba huo ndio utaratibu mpya wa mazishi ya kiserikali. Ndio maana hata baada ya kukosa watu kanisani na Karimjee walitumia mtindo wao wa kubeba watu waonekane wamejaa jambo ambalo walishindwa maana tunajua haikuchukua zaidi ya dk 45 kumaliza kuaga. Kwa Regia watu walitaka hata kumkata pua Yakubu aliyejifanya kuwa na haraka ya kuondoa msiba wakati huo huo akitangaza kwamba watu wawapishe wabunge waage. Magamba wakaendelea kubuku ndege zote jana kwa staili ya kubeba waombolezaji ticketi za bure zikiwa kila mahali, ndio maana watoto wa mjini wanasema serikali hii sasa imekua ya misiba, Raisi wetu JK Raisi wa Misiba, acheni nao waandike kitabu chao, maana najiouliza kama mwenyekiti wa chama alishakwenda, Msekwa nae allfuata nini? Kama Anna Makinda alishakuwepo, Ndugai alifuata nini? kama ni ushiriki binafsi sawa, lakini ukishatangaza kuwa ushiriki wa kiserikali hapo napo kuna jambo. Halafu sikumuelewa bibi kiroboto kutumia wakati huo kueleza habari ya kufiwa na wafanyakazi wa ofisi ya bunge, alitaka kuashiria kuna bundi ama kidudu mtu, ama kumtaka mungu ahamie kwenye taasisi nyingine? Hapa ndio matumizi ya siasa misibani yanapowarudia magamba, mwenzao mbowe pale Karimjee alikua relevant, kwamba msimpambe mpambanaji leo, vingaavyo vimeundwa waacheni wanafunzi wa vyuo wafanye siasa ilimradi hawavunji sheria.
 
Ni kitu tutamkumbuka rais wetu. Hicho na anachotuambia watanzania.
 
Jambo jingine ni kwambwa wanapowakilisha kuna allowance. Nakwambia hii hawaiachi hata siku moja.
 
Pamoja na kwamba kuzikana na kupeana faraja wakati wa misiba ni desturi ya Waafrika lakini kwa viongozi wengi wa serikali kuhudhuria ni gharama kubwa sana maana watalipiwa gharama zote za safari. Labda kuwe na utaratibu wa uwakilisha wa serikali kama vile waziri moja tu au mkuu wa mkoa inatosha.
 
Ninaamini kabisa kuwa kama wasingeenda, basi kungekluwa na malalamiko kuwa viongozi wa serikali wakacha mazishi ya mbunge
 
Hawana code of conduct. Fine mimi sina ugomvi if they wish to attend all funerals hapa Tanzania. This should not be at the cost of the tax payers money. This is bull shit. Kama wabunge wote irrespective of their parties kwa gharama zao bila kutumia magari ya Serikali fine. Swala linakuja muda ambao walipaswa kufanya kazi katika kamati za Bunge and this is the time watafidia vipi? Ni kweli hawana kazi ya kufanya. Can the new Chief Secretary or exchequer tell us how much it costs the government for Jakaya and Pinda to travel to Arusha and back. You can see that they are simply not serious. Hivi Watz wote wakifanya hivyo tunaweza kuendelea? All this bazaar is done at the cost of the tax payer, this more than Ujuha!
 
Nchi imewashinda kuongoza wanachotafuta sasa ni ili waonekane machoni mwa watu kuwa wana huruma kitu ambacho si kweli,hatukatai watu kwenda kwenye msiba lakini kwa hili la karibu serikali yote kuhamia msibani ni uwendawazimu,tukio la kukutana msibani rais na waziri mkuu ni ukosefu wa kazi,mtu akiamua kubisha udhaifu huu ataandika tu kwa vile baadhi wapo kazini lakini naamini nafsini mwake atajua huu ni upumbavu.
 
kwani huko wanakoenda kwenye misiba sio tanzania?au umeambiwa ukiwa kiongozi ni kukaa dsm tu.
 
kiongozi lazima ashiriki masuala ya kijamii na hasa matatizo ya watu wake,kwani we ulitaka kusemaje.
 
Back
Top Bottom