Morning_star
JF-Expert Member
- Apr 21, 2018
- 4,174
- 11,502
Nilitoka nikaenda sehemu kupata vyombo na kuchill na washikaji! Sasa tangu niingie pale, meza moja alionekana njemba akiwa na mdada na kwa ukaribu wa jinsi walivyokaa inaonekana ni wapenzi au couple! Sasa bwana muda wote mdada analia na kutoa mchozi njemba inambembeleza kwa kumshikashiga bega na kutoa kitambaa kumfuta muda woote mpaka nikaondoka nikawaacha! Matatizo ya mwanamke yanatatuliwa kwa mwanamme kuingilia kati na kutoa jibu lenye mashiko kimaamuzi! Kama tatizo la kifedha mwaga mpunga au mpige fix/sound na dakika kadhaa mwanamke anaanza kutabasamu! Sasa huyu njemba kutwa nzima kumbembeleza na kupanguza machozi huyo manzi!! Huu si ni undezi?