Luggie the great
Member
- Oct 20, 2019
- 18
- 52
Kuna mgao wa Maji sugu unaendelea katika Jiji la Dar es Salaam.
DAWASA walikuwa wamekata Maji kwa muda wa majuma matatu bila kutoa taarifa. Wananchi walipoanza kuhoji, sasa hivi wamakuja na mtindo wa kufungua Maji kwa muda mfupi halafu yanakatika. Kwa mtindo huu hata kupata Maji ya kuhifadhi inakuwa ngumu.
Nimeshaongaa leo nikiwa mitaa ya Mbezi Luis, nilipiga simu kwa wauza Maji wa kwenye magari, akaniambia ataniletea Maji muda si mrefu kwa kuwa anakaribia DAWASA Mbezi kuchukua Maji. Nikashikwa na butwaa, yaani hawa DAWASA wanaotakiwa watufungulie Maji, wanauza Maji kwa wauzaji wa Maji ili sisi tununue kwa Bei ya juu.
Hiki kinachofanyika ni hujuma ya wazi dhidi ya wananchi, serikali iliangalie hili suala. Waziri wa Maji chukua hatua kuwawajibisha viongozi wa DAWASA. Kama waziri hawezi kuzisimamia idara zilizopo chini yake ni bora ajiuzulu.
Swali la kujiuliza , je ni nani ananufaika na hujuma inayofanywa na DAWASA? Je viongozi hawajali yanayoendelea ?
DAWASA walikuwa wamekata Maji kwa muda wa majuma matatu bila kutoa taarifa. Wananchi walipoanza kuhoji, sasa hivi wamakuja na mtindo wa kufungua Maji kwa muda mfupi halafu yanakatika. Kwa mtindo huu hata kupata Maji ya kuhifadhi inakuwa ngumu.
Nimeshaongaa leo nikiwa mitaa ya Mbezi Luis, nilipiga simu kwa wauza Maji wa kwenye magari, akaniambia ataniletea Maji muda si mrefu kwa kuwa anakaribia DAWASA Mbezi kuchukua Maji. Nikashikwa na butwaa, yaani hawa DAWASA wanaotakiwa watufungulie Maji, wanauza Maji kwa wauzaji wa Maji ili sisi tununue kwa Bei ya juu.
Hiki kinachofanyika ni hujuma ya wazi dhidi ya wananchi, serikali iliangalie hili suala. Waziri wa Maji chukua hatua kuwawajibisha viongozi wa DAWASA. Kama waziri hawezi kuzisimamia idara zilizopo chini yake ni bora ajiuzulu.
Swali la kujiuliza , je ni nani ananufaika na hujuma inayofanywa na DAWASA? Je viongozi hawajali yanayoendelea ?