endeleeni mi yangu macho tu
hahahahha asante mkuu.Ukishaandika umefanya zaidi ya kutazama kwa macho.
Pale mkeo au mwenzio anapomwachia housegirl kila kazi hata weekend? kutandika kitanda, kukupikia, kukutarayirishia chakula mezani, maji ya kuoga mhhhh.....................ndio uzungu au sie wengine tumepitwa na wakati?
whaaat? hahhahahah haya makubwa kuanzia leo ntaajiri mahouse gal wenye sura za kutisha na maumbo yasioeleweka,
hadi kutandika kitanda? Loh........
Mmhhh we nawe mfukunyuku kama nini
Uvivu tu,wao ni Tamthilia,mara kuna kikao cha harusi,mara kuna birthday ya nani,il mradi tabu tuupu,na kama ana ka blackbery ka uongo hapo ndio baalaaa,atatongozwa kwenye hizo bibi em msg mpaka basi,kuweni makini watoto wa kike,jifunzeni kutulia majumbani na kupanga maisha na waume zenu!Pale mkeo au mwenzio anapomwachia housegirl kila kazi hata weekend? kutandika kitanda, kukupikia, kukutarayirishia chakula mezani, maji ya kuoga mhhhh.....................ndio uzungu au sie wengine tumepitwa na wakati?
...aaaaaaaaaarrrghhh jamani, mnamuogopa housegal kuliko 'popo bawa'?
Wetu huingia chumbani kumsaidia mamsap kupanga dressing table, nguo kabatini, kusafisha master bedroom na kudeki bafuni...
kwanini mamsapu ataabike wakati kuna 'binti' analipwa bana?
Unajua kuna kitu ambacho tunashindwa kujua ni kuwa hata kama housegirl ingekuwa kazi yake ni kuteka maji na kupika tu basi huyo mwanaume(Mume) akiamua kutembea na huyo binti atatembea naye tu.
Ni kama alivyosema MwanajamiiOne kuwa wengine waliamka na kuwapikia chapati sijui za kumimina lakini bado walitendwa tu. Ninachotaka kusema ni kwamba suala la housegirl kufanya mapenzi na Mume siyo eti kwasababu anadeki mpaka chumbani au anatandika kitanda kwahiyo Mume ameona ufanisi wa housegirl ni mkubwa kuliko wa Mkewe. No, hapana, hii naipinga kabisa bali ni hulka ya mtu binafsi. Na ukiona mwanaume amefanya kitendo hiki halafu akatoa sababu hizo hapo juu atakuwa mwendawazmu na mpumbavu. Hutakiwi kumu-award housegirl mapenzi kwa kuwa anafanya kazi vizuri.
Basi kama ndio hivyo uku maofisini ingekuwa kila mfanyakazi anayefanya kazi vizuri angekuwa anakuwa awarded mmapenzi bila ya kujali kama huyu ni mwanamke au mwanaume. Mimi naona huu ndio utaahira wa wanaume wenzangu, kwani uko chumbani ni madhabahuni kwahiyo wassingie watu wengie zaidi ya mume na mke?
Mimi nafikiri sababu ya mume kutembea na housegirl iwe ni kuwa amemtamani kama ambavyo anamtamani mwanamke mwingine yeyote. Tuache kuwaonea wake zetu na kuwadhalilisha wake zetu eti kwa kisa housegirl anafanya sana kazi za ndani mpaka chumbani anaingia
Jamani ,wengine tulichapa kazi mpaka nguvu zikatuishia ,unaamka alfajir unapika na kumfungia mahanjumat ya kula asubuhi na mchana akiwa akazini,ngou zake zote nafua ,chumbani nasafisha mwenyewe na kunakosita*6 nahakikisha mambo mazuri ,nilichotendwa sitasahau mpaka naingia kaburini hivyo hawa jamaa zetu hata ukiwabeba mgongoni huwa wanapanda na viwembe ,nawaasa wenzang msimalize nguvu zenu zote kwa ajili ya wanaume hawana shukurani hawa tena msije mkaacha shughuli zenu za kiuchumi kwa watu wadhalilishaji wasiothamini utu wa wenzao,kwani mwanamke yeye ndio ameumbwa kwa ajili ya kumtumikia mume!maisha ni kusaidiana tena ukimkuta sio tu na housegirl bali na mwingine yeyote mwambie nyuma geuka mbele tembea shoto kulia ,shoto kulia asisimame na atokomee mojakwa moja