HIV ya Zanzibar ni Muungano na TRA ni kirusi(verus) chake cha kunyoya.

abdulahsaf

JF-Expert Member
Aug 31, 2010
858
130
[h=1][/h]Written by makame silima // 28/06/2011 // Habari // No comments

Mtarajiwa urais wa Muungano huyu Mizengwe Pinda

Kirusi kinacho uwa uchumi wa Zanziba hishi."] Hakuna shaka kuwa Muungano ndio tatizo sugu hivi sasa ktk jamii ya ki-Zanzibar katika kupiga hatuwa za kiuchumi na kimaendeleo, Muungano umekuwa ni mzigo mkubwa mno uliowanamia raia wa kawaida wa Zanzibar ktk mbinyo wake wakuwakamua kwa jindamizi la TRA.
Wenzetu hawana nia njema ya Muungano kama kweli walikuwa na nia njema ya Muungano basi Zanzibar ni nchi yene ardhi ndoko na wananchi kidolo ukilinganicha na Tanganyika ijitayo Tanzania Bara, jitihada za wenzetu ndani ya Muungano nikuuwa uchumi wa Zanzibar na kuwafanya Wzanzibar wahame ktk nchi yao ili wapandikize mbegu za watu wenye asili ya Tanganyika ijitayo Tanzania Bara kwa lengo la kuvitawala visiwa na kupunguza nguvu ya wazaliwa wazawa wa Ki-Zanzibar
Ndio ukaona mikakati ya Mwanzo ni kuuwa utawala wa Zanzibar(power)ASP 1977 na kushukuwa mamlaka ya Zanzibar na nguvu ya Zanzibar kui-tranfer ccm-Dodoma, Agenda nyigine iliofuata ni divide & Rule ya Wzanzibar wenyewe kupashikizwa chuki za rangi,jisia,u-chama na ukabila kwa kutumia Wzazibara ambao wengi wao wamepewa nafasi Nyeti katika Serekali ya watu wa Zanzibar na wengine kupashikwa ktk usalama wa Taifa Zanzibar.
Hii yote nimikakati ya wenzetu kuibinya Zanzibar kwa kutumia mwevuli wa chama na watapia mloo (Wanafiki) ili wapate kuizibiti Zanzibar kirahisi na kufanya hivyo ni kuitia Ziki Zanzibar na watu wake ili wapote kuhama makaazi yao.
Kuna mifano mingi tu hai, mfano wa viwango vya mishahara ya Zanzibar na ya Muungano? wafanya kazi wa Muungano wanapo kuja kufanya kazi Zanzibar hupewa mishahara mikubwa ukilinganisha na mishahara ya Zanzibar, huu ni mtego hutegwa Wzanzibar kupenda Muungano(Tanganyika), yani haingii akilini kabisa kuwa mishahara ni ya Muungano wa Tanganyika na Zanzibar kwa nini upande mmja iwe mikubwa upande mwengine iwe midogo hali ya kuwa Muungano ni moja? hapa ndipo panapokuja majibu yasio na Jawabu?.
Kuwa Tanganyika haijafa kama wanavyosema wenyewe ipo na imevaa Koti la Tanzania, maana haingii akilini kuwa Muungano huu uwe na upendeleo wa mishahara inayolipwa ktk Muungano, Zanzibar ilipwe mishahara ya Muungano kidogo lakini Muungano ulipe mishahara mikubwa? kwa nini hamu fufuwi Tanganyika yenu na tukajuwa kuwa hawa watumishi ni Watanganyika na wanalipwa ktk mishahara ya Tanganyika?.
Mimi kuna suala moja nawauliza wangwana? mishahara ya Wzanzibar hawa, Samia Suluh,Haribu Bilali, Hosssen Mwinyi na Shamsu Vuai Nahodha inalipwa na Serekali gani? na kama mfano Vuai Nahodha anafanya kazi kama Tx wa Tanganyika au vipi mbona viongozi wetu wa SMZ munatushanganya ktk kutaka jibu la nimambo gani na gani yasio ya Muungano waulizeni mabwana zenu mutwambie Wzanzibar?.
Au ndio tuseme mumesha kwenda kuikwamisha Zanzibar pabaya munashindwa kutwambia? maana sera yenu ccm/smz ni sera ya serekali mbili kuelekea moja sasa yupi ni looser kwa mfumo huu ambao mimi nasema tayari tuko ktk mfumo wa Serekali moja, hii jina Muungano nikubabaishwa tu na viongozi wetu walafi watabia mloo.
Maana ninavyo juwa mimi nchi zote ulimwenguni zilizo ungana hujaona kuza utaifa wao na uti wa nchi yao, hata balizi za nchi zilizo ungana utaskia Repblic of Senegambia yani Senegali na Gambia, Replic of Sheko/slovakia ,Repblic of South Korea na Noth Korea.
Sasa hapa kwetu ni vishekecho vikubwa na umbubumbu wanao fanyiwa smz na master plan Tanganyika kuambiwa Muungano huu niwakupigiwa mfano na niwapekee? nikweli niwapeekee majuha wa smz, kama kweli niwapeekee basi nchi nyingi za Afrika zinge jiunga lakini nambie nchi gani za afrika zilio jiunga? Nyiyi mazuzu Ccm/smz munao sema Zanzibar ni nchi ilio ungana na Tanganyika?
Hivi sasa kwa tarifa yenu nchi ni moja tu, yani Tanganyika ilio vaa Koti la Tanzania, na ndio ukaona wanajita Repblic of Tanzania unajuwa mana yake hio? hapo hapana wawili ni mmoja tu mana yake? maana ni Serekali ya watu wa Tanzania(Tanganyika).
Nasema (Tanganyika) kwa sababu angalia Tanzania ilivyo Tanganyika/ kwanza Katiba ya Tanganyika ndio ya Tanzania,Rais wa Tanganyika ndio Rais mkuu wa Tanzania,Nembo na Simbuli zilizokuwa za Tanganyika yani nembo ya Adam na Hawa ndio ya Tanzania, Sehemu nyeti za uongozi wa Nchi kuuanzia Rais mkuu,Waziri mkuu na hada Gavana wa Bank kuu BOT, Waziri anae wakilisha mambo ya nchi za njee ni wa Tanganyika yani hakuna walicho tubakishia, mpaka mkushanyaji mapato mkubwa TRA ni wa Tanganyika.
SMZ wakeup unawabebesha jukumu Wzanzibar kuiuza nchi yao na nyiyi kushukuwa zima mbele ya M/mungu, hivi sasa mikakati na choyo cha Watanganyika ni kuuwa ushumi wa Zanzibar foroho na wafanya biashara wadogowadogo kufa maana wakubwa tayari wamesha wavuta bara bada ya kuuwa bandari ya Zanzibar, hivi sasa ni kuramba Kikango, yani kuwa wafanya biashara wadogo wadogo Zanzibar?.
Kivipi maana angalia choyo cha hawa wanao jita ndugu zetu lakini mbele ya uchumi sio ni makatili? hivi sasa kuna bizaa kibao zikiwemo magari ktk Bandari ya Dar zimekwama kutokana na mabadiliko mapya ya bizaa kutoka Zanzibar kuingia Tanganyika, mfano ikiwa umepeleka gari Dar gari lile ukiliteremsha moja kwa mija Dar ushuru wake ni millioni 7 lakini Ukiliteremsha Zanzibar ni milioni 5 sasa kwa vile wanajifanya wajanja Wtanganyika ukipeleka Dar unalipe tena ushuru kama uloeteremsha moja kwa moja kwao? inakuwa vipi wanakwambia tuletee karatasi ulolipia Zanzibar ikiwa umelipa million 5 wao wanakukomowa unalipa 3 Zaidi kwa sababu 7 ushuru wa Dar na moja kuieka sana katika storege.
Hizi ni mbinu za Wafanya biashara Zanzibar kukomolewa na kuuliwa Zanzibar kibiashara na kiuchumi kukuwa, hishi ni choyo cha hawa wanaojita tumeungana, na TRA ilikuwa tayari ije ifunge mitambo yake ya Cumputer Zanzibar ili iwe kama hadithi ile ya Farene carence yani pesa za kigeni ma mambo ya kigeni kuwa yanasimamiwa Tanganyika Zanzibar hatuna letu jambo tusubiri tuombe na tusumbuliwe 5.4%.
Sasa na TRA ilikuwa tayari wafunge mitambo yao na waiseti ili kukipeleka kitu chochote mpaka Tv moja inaulizwa Cumputer Tanganyika Tv Philip kiasi gani Bwana? hivi sasa kuna wafanya biashara wa Zanzibar walio peleka magari ya Toyota Amazoni Dar yamekwama wanambiwa ushuru millioni 20.
Jee huu Muungano ulipo tufikisha hapa bado tu tuendelee kuzama Wzanzibar na kizazi shetu? viongozi wetu asheni itikadi za chama kiokoweni kizazi shenu cha Zanzibar kinapotea ktk mikono miwili ya majambazi hawa wa Ki-Tanganyika lao moja.
Mungu ibariki Zanzibar na Wzanzibar wote.
 
Back
Top Bottom