HIV: Kuwe na kituo cha kuripoti watoro na wasiochukua dawa za kufubaza maambukizi ya HIV na kupima wageni

Braza Kede

JF-Expert Member
Nov 1, 2012
1,706
3,355
Kuna wakati ilikuwa ukienda hospitali ikakutwa na maambukizi walikuwa wanakwambia uwape majina ya ulioshirikiana nao tendo hlf wao kwa muda wao wanawatafuta kwa ajili ya upimaji na tiba. Sina hakika kama utaratibu huo bado upo.

Kwa sasa bado kuna watu wengi tu huku mitaani unakuta mtu ana maambukizi lakini kwa sababu anazojijua yeye haendi kuchukua dawa za kufubaza maambukizi. Wengine wakidai wameombewa na wachungaji huko kwenye nyumba za ibada na kwamba kwa sasa wamepona!

Mimi naamini watu hawa ndo chanzo kikubwa cha wimbi la maambukizi mapya ya ugonjwa huu maana kama kila mhusika angekuwa anafuata utaratibu wa matibabu hayo maambukizi mapya yangetoka wapi?

Nashauri Wizara ya Afya Tanzania iweke utaratibu wa jamii kuwaripoti watu kama hao maana wengine unakuta kwa namna moja ama nyingine wanajulikana kwenye jamii zao kuwa ni waathirika lakini wamekataa kuchukua dawa.

Hii itasaidia kupunguza au kuondosha kabisa maambukizi mapya hasa kwa vijana wadogo ambao mara nyingi wanaishia kupata maambukizi kutoka kwa watu wazima ambao kwa sababu wanazozijua wao wamejiweka nje ya mfumo wa matibabu.

Vinginevo haya maambukizi hasa kwa vijana wadogo hayataisha kamwe.

Hlf kuwe na utaratibu wa wageni wanaotoka nchi zingine kupima maana km nchi tunapokea wageni kutoka kila engo ya dunia hii na hakuna upimaji wowote. hawa nao wanaingia na kuchangamana na wananchi wazalendo. salama iko wapi hapo? Kuwe na utaratibu wa kupima hawa wageni kabla hawajaingia nchini tuweze kulinda vizazi vyetu vijavyo.
 
Naona unaandika huku unatetemeka kwa hofu...

Eti hakuna HIV/AIDS...

Ninyi ndio wapiga kura wa CCM...
Siwezi kutetemeka mzee mimi sio muoga.
Ninachosema nina hakika nacho na nimefanyia utafiti. Hakuna ugonjwa unaoitwa UKIMWI ambao unaambukizwa kwa ngono. HAKUNA
 
Ndio nyinyi na hizi ndo kauli zenu halafu mnaishia kuwapasia madogo maambukizi

Jitambue kapime na uanze dawa mapema
Acha wenge, huo ukimwi unapimwa kwakutumia kipimo gani?
Na ni nini hasa kinachopimwa ili kuutambua ukimwi?
Unaweza ukawa na picha yoyote ya kirusi wa ukimwi utuwekee hapa?
Ukosefu wa kinga unaweza kuambukiza vipi mtu kwa tendo la ngono?
 
Nasikia ukiacha tu kumeza dawa ata siku moja homa inakukamata sasa hao wanaotoroka kabisa kuchukua dawa inakuwaje
 
Mkuu hili ni wazo mfu kabisa, kumbuka ambao hawajapima na wana maambukizi ni wengi kuliko hao wanaotumia ARV. Kinachotakiwa ni elimu ya kutosha kwa kila raia kujikinga kwa kufanya ngono salama.
Wengi usiowadhania kabisa unakuta ni waathirika, na wengi hawajijui na wanaendeleza ngono zembe. Huwezi kuanza kumpima kila mgeni, hili halipo popote, pambana na raia wako wawe na uelewa wa namna ya kujikinga.
 
Siwezi kutetemeka mzee mimi sio muoga.
Ninachosema nina hakika nacho na nimefanyia utafiti. Hakuna ugonjwa unaoitwa UKIMWI ambao unaambukizwa kwa ngono. HAKUNA
mtafiti wa mchongo (kwa sauti ya mwaisa)
 
Acha wenge, huo ukimwi unapimwa kwakutumia kipimo gani?
Na ni nini hasa kinachopimwa ili kuutambua ukimwi?
Unaweza ukawa na picha yoyote ya kirusi wa ukimwi utuwekee hapa?
Ukosefu wa kinga unaweza kuambukiza vipi mtu kwa tendo la ngono?
skiza kijana

inawezekana miaka iyo ya nyuma haukuwepo, ngoja nikupe stori fupi kidogo

kabla ya hizi dawa hazijaja hali ya vifo kwa wagonjwa wa ukimwi ilitisha sana

mtaani mkiona fulani haonekani na hakuwa safari basi ilikuw waz keshapatwa na gonjwa hili

mgonjwa alikuwa akichongeka kama mbao ya seremala na hata ikibidi aende hospitali inabidi mumpeleke na giza watu wamelala wasimuone maana mwili mzima unabaki mafuta matupu! mtu mzima aliisha mwili na kubaki km katoto kadogo na akitolewa nje na kuanikwa kama wewe unavoanika nguo na kurudishwa ndani!

kinacholeta utofauti leo na ndomaana nyie wengine hata mnadai homa haipo ni hizo dawa zinazomezwa kiasi kwamba mtu anaonekana mzima mwenye afya yake.

bahati mbaya dawa hizi ni za ufazili maana ni gharama sana serikali haiwezi kuwanunulia wagonjwa wote. sasa tuombe wafazili waendelee kutoa dawa na watu wazipate bure kama hivi. nje ya hapo tutarudi kule tulikotoka kuanika watu nje kama nguo kama miaka ile na mpaka apo ndo hata hizi kauli zenu zitabadilika

kijana USIJICHANGANYE!
 
Mkuu hili ni wazo mfu kabisa, kumbuka ambao hawajapima na wana maambukizi ni wengi kuliko hao wanaotumia ARV. Kinachotakiwa ni elimu ya kutosha kwa kila raia kujikinga kwa kufanya ngono salama.
Wengi usiowadhania kabisa unakuta ni waathirika, na wengi hawajijui na wanaendeleza ngono zembe. Huwezi kuanza kumpima kila mgeni, hili halipo popote, pambana na raia wako wawe na uelewa wa namna ya kujikinga.
Kiongozi kuna nchi nyingi tu huingii kama uko + hasa km unalengo la kwenda kuishi huko
 
bahati mbaya dawa hizi ni za ufazili maana ni gharama sana serikali haiwezi kuwanunulia wagonjwa wote. sasa tuombe wafazili waendelee kutoa dawa na watu wazipate bure kama hivi. nje ya hapo tutarudi kule tulikotoka kuanika watu nje kama nguo kama miaka ile na mpaka apo ndo hata hizi kauli zenu zitabadilika

kijana USIJICHANGANYE!
Hoja yako yote imebebwa na huu mstari.
Ni biashara na serikali inalipa hela nyingi.
Naijua historia ya huu ugonjwa, nilikuwepo tangu unaanza miaka ya 80 mwanzoni ukiitwa Juliana.
Na nimeshuhudia ukiuwa watu kwa wingi miaka ya 80 mwishoni na miaka ya tisini.
Huo ugonjwa kwa sasa haupo imebaki biashara
 
mtafiti wa mchongo (kwa sauti ya mwaisa)
Tatizo madaktari wetu ni mizigo wanachoagizwa kufanya na wazungu ndicho wao wanafanya. Ni mabingwa wa kukariri kama kasuku.
Hawana tafiti wala uchunguzi hasa kitu kikitokea kwa mzungu.
Tumeshuhudia vioja vingi tu kwa watumishi wetu wa afya hawana cha ziada zaidi ya gugo.
Hata korona km bila vita ya uklein na Russia hadi sasa ingekuwepo na tungekuwa lockdown.
 
Hoja yako yote imebebwa na huu mstari.
Ni biashara na serikali inalipa hela nyingi.
Naijua historia ya huu ugonjwa, nilikuwepo tangu unaanza miaka ya 80 mwanzoni ukiitwa Juliana.
Na nimeshuhudia ukiuwa watu kwa wingi miaka ya 80 mwishoni na miaka ya tisini.
Huo ugonjwa kwa sasa haupo imebaki biashara
inawezekana ni kweli ni biashara lakini hata kama ni ivo basi haiwezi kuwa biashara ya serikali.

hapo labda useme ni biashara ya hayo makampuni ya kutengeneza hizo dawa maana mwisho wa siku ndo yanayolipwa izo pesa za madawa.
 
Back
Top Bottom