Anselm
JF-Expert Member
- Nov 16, 2010
- 1,710
- 291
Mimi natumia Modem ya Voda nilianza kutumia vifurushi vya Unlimited lkn baada ya kuona nabakisha chenchi nyingi nikahamia kwa kile kifurushi cha 5GB cha mwezi,sasa tatizo limeanza wiki iliyopita ngoma sasa hv inazingua ile kinoma,iko very slow na wakati mwingine inakwenda offline kabisa,jana imenitia hasira karibu niivunjevunje na nyundo mwenye maujanja ya kuninusuru kutoka kwenye tatizo hili tafadhali anisaidie otherwise nina mpango wa kuibeba niipeleke pale Mlimani City wakanirudishie chenchi yangu ya kwenye bundle(nimecheki salio jana nimesalaiwa na 3.9GB) kwani ushakuwa us***e,mtu nipo hapahapa Dar na'browse utafikiri niko Nanjilinji sijui Kipatimu,mambo gani haya Voda wananiletea?