chobu
JF-Expert Member
- Nov 5, 2010
- 308
- 26
hili ni jambo la muhimu sana kwa serikali kulifanyia mabadiliko ya haraka ili kupunguza gharama za matumizi ya fedha za serikali; baadhi ya viongozi ambao wamepewa magari na madereva wa kuwahudumia wanasababisha upotevu wa fedha za serikali kutumika pasipo sababu za msingi; ambapo wangeweza kuzuia. Na hili limo kabisa ndani ya uwezo wao mfano; kiongozi anaishi bahari beach, halafu dereva wake anaishi mbagala; dereva huyo ni lazima asubuhi sana awahi kumchukua boss wake amuwahishe kazini. Imagine dereva huyo atatoka saa ngapi kwake mbagala hadi bahari beach? Ni mafuta kiasi gani yatatumika? Hivi kweli hakuna mbadala? Kwanini kiongozi kama huyo asipewe dereva anayeishi angalau karibu na maeneo yake ili kupunguza gharama za mafuta? Ninashauri wahusika mliangalie hili kwa makini sana na hatimaye mlipatie ufumbuzi.