incredible terminator
JF-Expert Member
- Aug 1, 2016
- 2,241
- 3,529
Wakuu habari,
Inasikitisha sana hawa wakandarasi wanaorekebisha barabara wanavyofanya kazi kimazoea na kusababisha kero kwa watumiaji.
Mimi ni mkazi wa Dodoma, ikiwa jiji hili lilipewa hadhi ya kuwa Mji Mkuu wa Tanzania, sijui kwanini wizara husika zinakubari Jiji hili kuchukuliwa poa.
Kuna vijitabia vinafanyika kimazoea jijini hapa kiasi kwamba hadi watu tunashindwa kuelewa kwamba hili taifa halina uongozi au nikuchukuliana poa?
Mfano barabara ya Bahi ambayo wengi huitamka kama byeroad, Mwanza road etc, kumekuwa na tabia ya barabara hii kujazwa kokoto, kutoka round about hadi Kizota Msikitini, pasipokuwepo na viashiria vyovyote vya tatizo katika barabara husika.
Kokoto hizo hujazwa na kusababisha kero kama vile vumbi pamoja na hatari ya utelezi kwa watumiaji wa barabara hii, pasipo sababu za kimsingi zozote zile.
Inaonekana kama ni bajeti za upigaji tu zinaratibiwa kwa kuwa barabara iko vizuri tu, chanzo cha kumwaga makokoto na kusababisha kero kwa watumiaji hakieleweki kabisa, maana hata mara baada ya kokoto hizo kuisha ndio husababisha mabonde na mitikisiko katika barabara.
Pili, Barabara ya Mbeya, tangu mwaka jana mkandarasi anaetengeneza barabara ya standard guage, au Barabara ya Treni ya umeme, waliharibu kipande cha barabara maeneo ya Mkonze, kutoka njia panda ya Hosptali ya Mkonze hadi maeneo ya White Rore, au Image Petrol Station, kwa ajili ya marekebisho ya barabara ya juu ya treni ya umeme, na baada ya kukamilisha zoezi lao.
Hadi sasa, kipande kile hakijafanyiwa marekebisho, na kimegeuka kero kubwa kwa watumiaji wa barabara ile, ukilinganisha barabara ile ni miongoni mwa barabara ambazo zinatumika sana kwa magari ya mizigo.
Kuna vumbi lisilokuwa la kawaida, tena kibaya ni vumbi lenye mchanganyiko wa cement, kitu ambacho ni hatari sana hata kwa afya za watumiaji wa barabara ile. Ila cha ajabu wizara ziko kimya, na njia hii inazidi kuwa hatarishi kwa kuwa kuna muda vumbi linafunika njia nzima na hata mtu asijue kipi kinakuja mbele yake kutokana na wingi wa vumbi.
Sijui kama ndio kuchukulia poa au wanajifanya hawaoni. Pia barabara hii hii ya Mbeya maeneo ya Matumbulu, Mpunguzi, hadi sasa barabara iko katika marekebisho ila mchepuko wa njia iliyoandaliwa ili kupisha marekebisho ya barabara haukidhi mahitaji kulingana na umhimu wa barabara husika na matumizi yake, na bado kasi inayotumika kutengeneza barabara ile ni taratibu sana, kiasi kwamba hadi sasa ni Mwezi wa Tatu unaelekea wa Nne tangu marekebisho yale yaanze kufanyika ila kazi inaonekana bado sana; kama ndio wameanza siku tatu!
Hapa tuaniomba serikali iingilie kati changamoto hizi, hasa kile kipande cha Mkonze kwani lile vumbi ni hatari kwa afya za watumiaji wa barabara ile.
Inasikitisha sana hawa wakandarasi wanaorekebisha barabara wanavyofanya kazi kimazoea na kusababisha kero kwa watumiaji.
Mimi ni mkazi wa Dodoma, ikiwa jiji hili lilipewa hadhi ya kuwa Mji Mkuu wa Tanzania, sijui kwanini wizara husika zinakubari Jiji hili kuchukuliwa poa.
Kuna vijitabia vinafanyika kimazoea jijini hapa kiasi kwamba hadi watu tunashindwa kuelewa kwamba hili taifa halina uongozi au nikuchukuliana poa?
Mfano barabara ya Bahi ambayo wengi huitamka kama byeroad, Mwanza road etc, kumekuwa na tabia ya barabara hii kujazwa kokoto, kutoka round about hadi Kizota Msikitini, pasipokuwepo na viashiria vyovyote vya tatizo katika barabara husika.
Kokoto hizo hujazwa na kusababisha kero kama vile vumbi pamoja na hatari ya utelezi kwa watumiaji wa barabara hii, pasipo sababu za kimsingi zozote zile.
Inaonekana kama ni bajeti za upigaji tu zinaratibiwa kwa kuwa barabara iko vizuri tu, chanzo cha kumwaga makokoto na kusababisha kero kwa watumiaji hakieleweki kabisa, maana hata mara baada ya kokoto hizo kuisha ndio husababisha mabonde na mitikisiko katika barabara.
Pili, Barabara ya Mbeya, tangu mwaka jana mkandarasi anaetengeneza barabara ya standard guage, au Barabara ya Treni ya umeme, waliharibu kipande cha barabara maeneo ya Mkonze, kutoka njia panda ya Hosptali ya Mkonze hadi maeneo ya White Rore, au Image Petrol Station, kwa ajili ya marekebisho ya barabara ya juu ya treni ya umeme, na baada ya kukamilisha zoezi lao.
Hadi sasa, kipande kile hakijafanyiwa marekebisho, na kimegeuka kero kubwa kwa watumiaji wa barabara ile, ukilinganisha barabara ile ni miongoni mwa barabara ambazo zinatumika sana kwa magari ya mizigo.
Kuna vumbi lisilokuwa la kawaida, tena kibaya ni vumbi lenye mchanganyiko wa cement, kitu ambacho ni hatari sana hata kwa afya za watumiaji wa barabara ile. Ila cha ajabu wizara ziko kimya, na njia hii inazidi kuwa hatarishi kwa kuwa kuna muda vumbi linafunika njia nzima na hata mtu asijue kipi kinakuja mbele yake kutokana na wingi wa vumbi.
Sijui kama ndio kuchukulia poa au wanajifanya hawaoni. Pia barabara hii hii ya Mbeya maeneo ya Matumbulu, Mpunguzi, hadi sasa barabara iko katika marekebisho ila mchepuko wa njia iliyoandaliwa ili kupisha marekebisho ya barabara haukidhi mahitaji kulingana na umhimu wa barabara husika na matumizi yake, na bado kasi inayotumika kutengeneza barabara ile ni taratibu sana, kiasi kwamba hadi sasa ni Mwezi wa Tatu unaelekea wa Nne tangu marekebisho yale yaanze kufanyika ila kazi inaonekana bado sana; kama ndio wameanza siku tatu!
Hapa tuaniomba serikali iingilie kati changamoto hizi, hasa kile kipande cha Mkonze kwani lile vumbi ni hatari kwa afya za watumiaji wa barabara ile.