Mzee Mwanakijiji
Platinum Member
- Mar 10, 2006
- 33,483
- 40,011
Hii si sandakalawe ambapo "mwenye kupata apate mwenye kukosa akose"; si sandakalawe kwa sababu yule mwenye kupata atakuwa anashikilia hatima yale waliokosa. Kwamba si sandakalawe kwamba tunacheza bahati nasibu na maisha yetu wenyewe na ya watu wetu. Kwamba, haijalishi nani anapata na nani anakosa. Kinachotokea naamini kugombania kitu fulani ambacho hatutaki wengine wapate na tunataka sisi tupate na siyo wao.
Kitu hicho tunachogombania ni msingi wa mgongano ambao tumeuingia na wengine bila ya kuomba kibali wala kuwaomba radhi watu wengine tunaamini ni ugomvo wa kudumu ambao hauna namna ya kupatana isipokuwa kwa upande mmoja kushindwa - kukosa.
Tunataka wao wakose kwa sababu tunajua wakipata ni madhara zaidi kwa taifa. Lakini si sote tunajua tunachogombania ni nini hasa maana hata wale walioupande mwingine yawezekana wanachuki nasi na kutuona ni maadui zao aidha kwa sababu wanafikiria tunagomba kile ambacho "ni haki yao" na hivyo tunajaribu kuwatibuliwa.
Baada ya mambo fulani ya kupuuzia yaliposemwa kwenye TBC hivi karibuni nimepokea maoni ya watu wengi ambao wameniambia kuwa yawezekana ni kwa sababu "nawavurugia kula" baadhii ya watu au kwamba "ninawawekea kiwingu". Maoni ya wengi yamekuwa kwamba labda wale wanaoikosoa serikali na kutoa mawazo mbadala kwa nguvu na pasipo kutafuta urafiki wanafanya hivyo kwa sababu wana wivu wa aina fulani au husuda kwa sababu hawataki watu fulani fulani "wapate".
Ndipo ninapoendelea kuandaa kwa raha mstarehe jawabu langu ambalo litashtua kushinda ripoti ile ya Meremeta nimejikuta naendelea kurudia swali ambalo niliwahi kuliuliza kwa karibu miaka minne iliyopita na ninaliuliza tena kwa namna nyingie ili tuweze kuona kama jawabu letu limebadilika.
Si wote wanagombania kitu kile kile.
Tunachogombania ni nini hasa? Wengine wanafikiri tunagombania vyeo na madaraka yao; na wengine wanafikiri tunagombania kupata sifa au kujulikana zaidi; na wapo ambao hawajui hata kama kuna kitu tunagombania! Swali ambalo mwanaharakati anatakiwa kujiuliza ni kuwa tunagombania nini hasa? Ni utajiri wao? Ni sifa zao? Ni majina yao? ni nafasi zao?