Mlamba asali
JF-Expert Member
- Dec 11, 2022
- 1,124
- 2,211
Kwa hiyo ndoto tu ukahama dini siku nyingine ukiota vinginevyo na kuona matukio utahama tena
Tumsifu Yesu Kristu! Kama nilivyosema hapo awali. Mimi nitabakia daima kwenye imani yangu. Na kamwe siwezi kushawishika na imani ya watu wengine wa Mataifa.wewe hauna tofauti yeyote na waislam, mbele za Mungu anawaona ninyi nyote mmepotea.
Upuuzi ni kuona dini ya mwingine ni propaganda za wazungu wakati yako yenyewe imeletwa na waarabu.Wapi pameandikwa hivo? Au nawewe umekaririshwa propaganda za wazungu?
Wewe jua tu ulishagongwa muhuri wa ukristu kwa hio zunguka zunguka ukichoka Mwanakondoo mpotevu rudi zizini utapokelewaHuo muhuri unagongewa wap na unagongwa na nan na kwa ushahidi gan?
Ukiona unajiuliza hili swali basi...bado chembechembe za ukristo ziko rohoni mwako.Hapana, kwanini nifanye hivo?
Uislam ndiyo dini bora kwa binadamu.Karibu katika quran na sunnah.
Uislamu maana yake Kusalimika.
Achana na propaganda za dini hii kuhusishwa na Ugaidi
Hivi unajua kuwa kuoa mke zaid ya mmoja kuna hekma kubwa sana kwa Alie tuumba.
Wacha hiyo, hivi unajua uislamu ndio dini iliyokuna kufundisha watu kujilinda vizuri na najisi( kinyesi na mikojo).
Ntaendelea wacha kwanza nimalizie kazi.
Zote tumeletewa sisi hatuna chetu. Bara la Afrika ndilo bara halina dini yakeTrue story: Tea time,
Nilizaliwa katika ukristo na kukulia kwenye ukristo.
Mwaka Jana nilihamia Tanga kikazi, mtaa niliokuwa Ninaishi ulikuwa una waislam tupu. nyumba nliyokuwa Ninaishi ilikuwa jirani na msikiti, Kila siku pale msikitini walikuwa wanaimba aya za Quran Usiku kucha. Sijui kwanini lakini Ile sauti ilikuwa ni nzuri sana masikioni na ilinifanya nikawa najisikia amani sana nilalapo.
Mwaka huu mwezi fulan nikiwa nimelala, nikaota ndoto ya ajabu iliyonifaonya nisilimu wiki hiyo.
Ndoto yenyewe ilikuwa hivi:
Niliota Mimi na kaka yangu wa Arusha tukitembea maeneo ya mtaani kwetu hapo Tanga. Tukakutana na kundi kubwa la watu wa Kila aina matajiri kwa masikini wakiingia katika ule msikiti jirani.
Pamoja na tofauti zao za kiuchumi lakini wote waliingia ndani katika ule msikiti na kuwa kama kitu kimoja. Hakukuwa na madaraja mule ndani, hakukuwa na mabenchi ila wote waliingia kama watoto wadogo wakijisalimisha kwa Muumba wao. Ni kama vile pesa,vyeo,umaarufu waliviacha nje ya msikiti.
Nikapita jirani nikasikia ndani Quran inasomwa na wote wakistaajabu maajabu ya hiki kitabu kilichoandikwa Karne nyingi zilizopita.
Nikapita kwa pembeni nikielekea zangu nyumbani, ila kwa nje nkakutana na mtu akawa ananialika tuingie kuswali, nikakataa kwa visingizio vingi kama vile Nawahi sehemu,sijui kuswali,siku nyingine nk. Nk.
Lakini yule mtu akanisisitiza na kuniambia kuwa nikiingia Mungu atanitoa gizani na kuniweka kwenye njia ya haki.
Mi nkaondoka lakini nkamuacha kaka angu akiongea na yule mtu. Ndoto ikaishia hapo.
Kaka angu niliokuwa sijawasiliana naye takriban wiki 3 na sikumwambia kuhusu hiyo ndoto,lakini wiki hiyo hiyo nilisikia kuwa kaka angu wa Arusha amesilimu.
Kiukweli nilistaajabu sana na kujiuliza ni nini hiki na maana yake nini?
Baada ya Tafakuri ya mda mrefu niliamua kwenda kwenye huo msikiti labda nitakutana na yule mtu wa ndotoni na hiyo ndiyo ikawa njia iliyonipelekea kurudi kwenye uislam(Kila mtu huzaliwa muislam).
Katika kumtafuta yule mtu Kuna shehe nilimsimulia, akaamua kuchukua jukumu la kunifunza na kunielezea maajabu ya Quran na kiukweli Ile ndoto + maajabu ya Quran ilinifanya nikasilimu.
Bado naendelea kujifunza mengi mapya katika hii Imani ya kweli na haki.
Allahu akbar.
PS: yule mtu Bado sijampata
PS #2: Braza wa Arusha anajua namimi nimesilimu lakini sijamuhadithia kuhusu Ile ndoto.
Unafanya dhambi kubwa na kumkosea Muumba wako unapompa Yesu binadamu kama Wewe hadhi ya Mungu.hiyo ilikuwa ni ndoto toka kwa shetani mwenyewe, umepoteza focus na kitu kikubwa sana maishani mwako, kuna siku utakuja kujuta. lakini hata hivyo una nafasi ya kubadilika na umkiri Yesu Kristo kama Bwana na Mwokozi wa maisha yako, uokoke kwasababu dhambi ya kwanza utakayohukumiwa nayo na ndiyo ambayo wanadamu watahukumiwa nayo ni kumkana Yesu Kristo kuwa Mwokozi wako. sikulaumu kwa hali uliyokuwa nayo kwasababu hata wakati unaota ulikuwa gizani, haukuwa tofauti na huko ulikokweda, kuwa mkristo wa dini hauna tofauti na waislam, kwahiyo haujabadili chochote umetoka kwa shetani ukaenda kwa shetani yule yule umebadilisha vyumba tu. ila kuwa Mkristo aliyeokoka (sio wa dini) ni kitu valuable na special, na ndicho kitakachofanya mtu auridhi uzima wa milele. hapo upo safarini kwenda jehanum ya moto wa milele. uamuzi ni wako.
Unapata faida gani kutunga uongo?Nna Ndugu yangu mmoja yeye alianza tu ghafla akawa Mlutheri akakaa huko kidogo akahama akaanza kuvaa 'ushungi, baibui & nikabu' na jina akabadirishwa aikupita mda akaanza kupandwa na mapepo kuuliza nini maruhani hatuelewi nini kinaendelea duuh ghafla akahamia kwa Mwamposa akaenda huko baadae akachoka akarudisha mpira kwa kipa RC alipotoka, Maisha haya watu wanatangatanga sana aisee
Ni kuwa wa wakristo.Kwan kuwa mkristo mpaka ufanyeje?