Hii kasi ya Nyalandu imetokea wapi?

Kifupi nakerwa na namna wa bongo wanavyoyachukulia mambo. Sijui lipi bora afanye Mh Nyarando. Ndio maana hawa viongozi hawajali wala kuogopa lolote kwakua wanajua aina ya fikra za Wabongo wachache wapenda kuchalenge vitu bila kuta fakari ili kujiona wamesema tuu na akili zimekalia kila kiongozi hafai hafai. Ukimpekua mtu kidogo yeye mwenyewe hata kusimamia familia yake hawezi. Wanadamu wote siwakamilifu na waadilifu ndani ya makundi ya waovu wapoo. Kila mtu asijifanye ni minzani ya mwenzake bila kujipima na yeye kwanza. Ni kweli Chama Cha Mapinduzi kina aina ya mapungufu yake lkn sidhani kama ndio dhamira ya Sera zake. Kutawla si jambo jepesi kiasi cha kila mtu kudhani anaweza ila kukosoana kwa misingi ni jambo labusara ktk kujenga nchi na sikushika Dola.

Usilazimishe watu kufikiri kama unavyotaka,hatuwezi kuwa na fikra sawa jenga hoja zenye mantiki juu ya utetezi wako kupata uhalali wa kuungwa mkono.

Fikra ndizo zinazojenga nchi na utekelezaji wa jambo lolote huanza kwenye fikra,busara ni kuambiana ukweli na kutambua ukweli sio kusifiana kinafiki.
 
Yeah halafu anaita waandishi WA Habari kila siku na kila saaa
 
Unayoyasema yote wewe ndiye kinara, kejeli na matusi imekuwa part of ur life
alikuwa wapi siku zote au ndo kaingia hapo wizarani leo. Sema tu tumuache ajitafutie ugari wa mwisho mwisho.lakin kuchapa kazi kwa nguvu ya soda na wale chomekea kwende offisini no support. Magufuli mwakyembe tiki.
 
Jamani si tunapiga kelele humu kila siku tukitaka viongozi wafanye kazi kwa bidii?sasa wameanza tunalalamika tena jamani?sasa mnataka iweje?tumpe muda huenda kilio chetu kimesikika,la kama ni geresha tu,basi mbio za sakafuni.....
 
Ana kampuni ya utalii wamtoe ana mgongano wa kimaslahi hata majangili pengine alikuwa anakutana nao mbugani lakini anawahifadhi majina

Wakati fulani hapa JF kulikuwa na uzi uliotuhabarisha kuwa kuna siku nyakati za usiku bwana huyu alikataa kukaguliwa kwenye kizuizi fulani kilichokuwepo kwa ajili ya kuangalia mali asili ndani ya gari lake hivyo pamoja na kampuni yake ya utalii sishangai mtu akisema yawezekana na yeye ni wale wale ila tu kavaa ngozi ya kondooo
 
Anajipendekeza ili baraza jipya la mawaziri lijalo asisahaulike.Swali langu:inawezekanaje waziri ajiuzulu kwa kushindwa kusimamia vizuri wizara yake halafu naibu waziri abaki,kwani yeye wakati unyama unafanyika alikua wapi?
 
Kumbukeni alikuwa naibu waziri, maamuzi mengi aliyokuwa anatekeleza yalikuwa ya boss wake Kagasheki. Muacheni achape kazi, ni wajibu wake.
 
Kesho atakuja na kuutaka URAIS,maana hatujui lengo kamili ni nini?Wapiga debe watakuja muda si mrefu,tusubiri kidogo.
 
Mnyonge mnyongen lkn haki yake mpen,Mimi binafsi nampongeza kwa juhud zake. Kipindi yupo Kagasheki isingekuwa rahsi kujua nini anafanya hata angefanya kazi kias gani pongezi zilikuwa zinaenda kwa aliyekuwa boss wake Kagasheki ila kwa wanaomfatilia sana aliwekeza sana kwenye kuutangaza Utalii nje na aliendesha kampen nyingi za kuupinga Ujangiri ikiwemo ile ya watembea kwa miguu waliotoka Arusha hadi Dar ya Walk for Elephant.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom