Kiumbe duni
Senior Member
- Dec 3, 2011
- 100
- 8
Huduma hii baada ya kupapatikiwa na watu wengi imeshaanza kuwa kero. Kama ukitaka kutuma pesa mkoa mwingine tofauti na unaoishi wakala atakuambia hairuhusiwi mpaka akurushie wewe na wewe ndio umrushie huyo wa mkoani. Huu ni wizi kwa sababu wakala akikurushia wewe halafu wewe ukamrushia wa mkoani ni lazima ukatwe hela, na wamkoani akienda kwa wakala kutoa pesa ni lazima akatwe. Kwa hiyo wanakula mara mbili kwako na kwa wa mkoani, tofauti kama wakala angeruhusiwa kurusha moja kwa moja mkoani angekatwa mtu mmoja tu. Wadai wakirusha moja kwa moja hela inaweza kupotelea njiani utetezi ambao hauna mashiko.