Asprin
JF-Expert Member
- Mar 8, 2008
- 68,015
- 95,369
Ndugu wajumbe na wadau wa jukwaa hili maalum la watu wasio na msongo wa mawazo,
Ninawaandikieni waraka huu kuwatakienyi nyote NOELI njema na heri ya mwaka mpya 2013. Nawaombeni safari hii tupeane heri na baraka kwa kutumia lugha yetu adhimu ya kiswahili bila kutohoa maneno kwenye lugha nyingine ikiwemo Kiingereza. Hii ni kutaka kumdhihirishia Yesu kuwa hata sie watanzania tunampenda na endapo kama angezaliwa Hospitali ya Barabara ya Bahari naye angekuwa mswahili mwenzetu.
Kwa muktadha huu basi naomba mnapobonyeza vitufe vya funguo ubao kwenye kutakiana heri ya Noeli basi tutumie lugha yetu adhimu walau kuonyesha mshikamano wa kitanzania.
Mimi na familia yangu tunawakaribisheni nyumbani kwa ajili ya kushehereka pamoja na baadaye tujiunge pamoja kwa umoja wetu katika maduka ya kuuzia vinywaji laini na vileo ili tugonganishe bilauri zetu na kutakiana afya njema.
Kila la kheri, na Mungu aendelee kuwabariki.
Msaada kwa waliosoma shule za watakatifu.
Msongo wa mawazo = Stress
NOELI = Christmass
Hospitali ya Barabara ya Bahari = Ocean Road Hospital
Vitufe = Buttons
funguo ubao = Keyboard
Bilauri = glasi
Atakayetumia lugha ya kiinglishi baraka zake zitapungua na anaweza asiurithi ufalme wa Mbingu.
Salamu za pekee kwa watoto wa shule za watakatifu; BiMtamu ( sweetlady), Bwana Mwamba ( Mr Rocky), Mwanamke Mweusi ( Blaki Womani), Hukumu ( Judgement), Binti Sayuni ( Zion Daughter), BiMcheshi ( charminglady), Arushamoja ( Arushaone), Ruhazwe Mdogo ( Ruhazwe JR) na wengine wote wenye majina yote yenye lugha ya Daudi Kameruni ambao sijawataja.
NB: Ntamuomba mwalimu wangu wa lugha hii adhimu Gaijin aje awacharaze bakora wote watakaokiuka masharti na kuichakachua lugha yetu. Pia wataohashuana kwenye huu uzi ntamwomba walimu gfsonwin, snowhite na SnowBall wachukue sheria mkononi.
Ninawaandikieni waraka huu kuwatakienyi nyote NOELI njema na heri ya mwaka mpya 2013. Nawaombeni safari hii tupeane heri na baraka kwa kutumia lugha yetu adhimu ya kiswahili bila kutohoa maneno kwenye lugha nyingine ikiwemo Kiingereza. Hii ni kutaka kumdhihirishia Yesu kuwa hata sie watanzania tunampenda na endapo kama angezaliwa Hospitali ya Barabara ya Bahari naye angekuwa mswahili mwenzetu.
Kwa muktadha huu basi naomba mnapobonyeza vitufe vya funguo ubao kwenye kutakiana heri ya Noeli basi tutumie lugha yetu adhimu walau kuonyesha mshikamano wa kitanzania.
Mimi na familia yangu tunawakaribisheni nyumbani kwa ajili ya kushehereka pamoja na baadaye tujiunge pamoja kwa umoja wetu katika maduka ya kuuzia vinywaji laini na vileo ili tugonganishe bilauri zetu na kutakiana afya njema.
Kila la kheri, na Mungu aendelee kuwabariki.
Msaada kwa waliosoma shule za watakatifu.
Msongo wa mawazo = Stress
NOELI = Christmass
Hospitali ya Barabara ya Bahari = Ocean Road Hospital
Vitufe = Buttons
funguo ubao = Keyboard
Bilauri = glasi
Atakayetumia lugha ya kiinglishi baraka zake zitapungua na anaweza asiurithi ufalme wa Mbingu.
Salamu za pekee kwa watoto wa shule za watakatifu; BiMtamu ( sweetlady), Bwana Mwamba ( Mr Rocky), Mwanamke Mweusi ( Blaki Womani), Hukumu ( Judgement), Binti Sayuni ( Zion Daughter), BiMcheshi ( charminglady), Arushamoja ( Arushaone), Ruhazwe Mdogo ( Ruhazwe JR) na wengine wote wenye majina yote yenye lugha ya Daudi Kameruni ambao sijawataja.
NB: Ntamuomba mwalimu wangu wa lugha hii adhimu Gaijin aje awacharaze bakora wote watakaokiuka masharti na kuichakachua lugha yetu. Pia wataohashuana kwenye huu uzi ntamwomba walimu gfsonwin, snowhite na SnowBall wachukue sheria mkononi.