Heche yuko sahihi kuhusu tamko lake dhidi ya Shibuda-Tundu Lissu

Molemo

JF-Expert Member
Sep 24, 2010
14,534
13,225
Mkurugenzi wa Sheria CDM ambaye pia ni mnadhimu mkuu wa Upinzani bungeni Tundu Lissu amempongeza Mwenyekiti wa BAVICHA Taifa John Heche na kuunga mkono kauli yake thabiti kuhusu mbunge wa Maswa Mashariki John Shibuda.
Lissu alidai kushtushwa na tamko la Makamu Mwenyekiti BAVICHA Juliana Shonza kumpinga Mwenyekiti wake hadharani.Lissu alidai kilichofanywa na Shonza ni kichekesho na utovu mkubwa wa nidhamu ambao hauwezi kuvumiliwa.
Lissu alienda mbali zaidi na kusema kikatiba Heche ni msemaji mkuu wa Vijana na si lazima kila kitu kipitie kwenye kikao bali ana mamlaka ya kutolea tamko jambo lolote analoona linaathiri harakati za chama.Amesema wanaosema Heche aliongea kama Heche hawajui wanachokisema bali aliongea kama Mwenyekiti na analindwa na Katiba ya BAVICHA.

SOURCE:MWANANCHI UK 7
 
Baadi ya wanawake si watu wa kuaminika sana hasa katika harakati ngumu kama hizi!
 
Wanasema yuko timu moja na shibuda je ni kweli????????..... huenda kaahidiwa ukuu wa wilaya,,,, ...... Tatizo njaaa na uzalendo unafiki wa watz tulio wengi,,,, tutaishia kulalamika mpaka mwisho wa dunia
 
Mkurugenzi wa Sheria CDM ambaye pia ni mnadhimu mkuu wa Upinzani bungeni Tundu Lissu amempongeza Mwenyekiti wa BAVICHA Taifa John Heche na kuunga mkono kauli yake thabiti kuhusu mbunge wa Maswa Mashariki John Shibuda.
Lissu alidai kushtushwa na tamko la Makamu Mwenyekiti BAVICHA Juliana Shonza kumpinga Mwenyekiti wake hadharani.Lissu alidai kilichofanywa na Shonza ni kichekesho na utovu mkubwa wa nidhamu ambao hauwezi kuvumiliwa.
Lissu alienda mbali zaidi na kusema kikatiba Heche ni msemaji mkuu wa Vijana na si lazima kila kitu kipitie kwenye kikao bali ana mamlaka ya kutolea tamko jambo lolote analoona linaathiri harakati za chama.Amesema wanaosema Heche aliongea kama Heche hawajui wanachokisema bali aliongea kama Mwenyekiti na analindwa na Katiba ya BAVICHA.

SOURCE:MWANANCHI UK 7

Short and Clear!
Wako wapi wale wote waliokuwa wanajificha na utetezi wao kwa Shibuda? watu wengine naona bado wana roho za kwanini? ndiyo maana wamemdanganya binti wa watu kwamba na yeye akatoe tamko baada ya wao kumwandalia tamko. Najua sasa hivi dada wa watu anajilaumu ni kwanini alidanganywa na wachache wenye roho za kwanini na sasa hana tena mvuto mbele ya vijana. Pole sana mdogo wangu Juliana, kwani itakuchukua muda sana tena kuaminika mbele ya jamii ya Watanzania hasa wanaopenda mabadiliko.
 
Huyu dada ni debe2pu. Namfahamu vizuri tangu 2kiwa wote pale Udsm. Anakawaida ya kukurupuka, alivoona tamko la Heche limepingwa na shibuda na viongozi wa Cdm wamekaa kimya akafkr hawamuungi mkono Heche akajua namna ya kuwafurahisha ni kupingana nae tena hadharani. Nakumbuka wakati Mbowe kawekwa ndani wakati ule alienda kichwakichwa akawekwa nae ndani akijua atapata umaarufu. Wakati 2nafungua tawi la cdm mabibo hostel pale Makuburi alionesha dhahiri ukurupukaji wake hasa kwa kuropoka mambo yacyomhusu tena mbele ya viongozi wakuu wa Cdm. Juliana ni debe tupu.
 
Ni hatari sana kumweka mtu kushika cheo ati kwa sababu ya jinsia ati kutoa fursa sawa kwa wote. Tufike mahali tuwape vyeo kwa sababu ya uwezo wao. Haya mambo ya usawa yatakuja tukishajitosheleza kiuchumi maana sasa tuko katika mapambano na makamanda wanatakiwa wawe na nguvu na kuweza kuruka vihunzi. Kama tunaongozwa na kamanda asieweza hata kuruka mfereji wa maji machafu, tukifika mtoni si atatutumbukiza? Wakati tunapopambana kuikomboa nchi yetu toka kwa mafisadi, twahitaji kuwa na makamanda wanaoweza kuona tatizo na kulishughulikia na sii walalamishi. Huyu juliana ni mlalamishi na hatufai. Tukimpa cheo atakuja kutafanya kama mama wa Malawi alivyoona kuwa suluhisho la matatizo ya malawi ni kuruhusu ushoga.
 
Pole sana Juliana... Siku nyingine usikubali kutumika. Naamini ulikuwepo pale Jangwani jana na kuangalia mood ya watu kuhusu Shibuda na kauli aliyootoa Mwenyekiti wako. Kueteleza sio kuanguka jirekebishe na usonge mbele
 
Mkurugenzi wa Sheria CDM ambaye pia ni mnadhimu mkuu wa Upinzani bungeni Tundu Lissu amempongeza Mwenyekiti wa BAVICHA Taifa John Heche na kuunga mkono kauli yake thabiti kuhusu mbunge wa Maswa Mashariki John Shibuda.
Lissu alidai kushtushwa na tamko la Makamu Mwenyekiti BAVICHA Juliana Shonza kumpinga Mwenyekiti wake hadharani.Lissu alidai kilichofanywa na Shonza ni kichekesho na utovu mkubwa wa nidhamu ambao hauwezi kuvumiliwa.
Lissu alienda mbali zaidi na kusema kikatiba Heche ni msemaji mkuu wa Vijana na si lazima kila kitu kipitie kwenye kikao bali ana mamlaka ya kutolea tamko jambo lolote analoona linaathiri harakati za chama.Amesema wanaosema Heche aliongea kama Heche hawajui wanachokisema bali aliongea kama Mwenyekiti na analindwa na Katiba ya BAVICHA.

SOURCE:MWANANCHI UK 7

Much Respect kamanda Lissu.Huyu Juliana ameonekana mtu wa hovyo ambaye kila mtu anaona ana agenda ya siri dhidi ya CDM.Ninachompenda Lissu ni mtu ambaye ni muwazi sana.
 
Back
Top Bottom