Hebu wanawake wa hapa JF ondoeni huu Mkanganyiko!

TUKANA UONE

JF-Expert Member
Jan 3, 2018
1,816
5,151
Mimi na salamu ni vitu viwili tofauti,salamu zimefanya waafrika wengi wamekuwa masikini!



Hebu nyie mademu wa hapa Jf naomba mniondolee huu utata(Mkanganyiko) ambao unaendelea kunitia wasiwasi humu Jf.

Kumekuwa na utaratibu siku hizi humu Jf hata wanaume kutumia Id za kike,sijajua lengo la wao kufanya hivyo ni kitu gani!

Kwakuwa uongo na utapeli hapa Jf umekuwa wa kutosha,naomba kesho niwatoe wafuatao "OUT" ili kujiridhisha kweli kama ni KE na wala siyo ME.

MALENGO

Malengo ya Kutoka Out ni Kufahamiana,Kubadirishana Mawazo na Ku-Enjoy kwa pamoja kama wanafamilia wa JF.

Kwakua watumiaji wengi wanaotiliwa mashaka ni wanaotumia Id zenye majina ya KE,naomba wafuatao ikiwapendeza kesho tutoke wote kama Familia ili niamini kweli ni KE.

1. Jemima Mrembo
2. cocastic
3. MZURI SANA
4. Lamomy
5. Demi
6. To yeye
7. Leejay49
8. Carleen
9. recho Jr
10. Hornet


Kama nilivyosema,lengo ni kufahamiana,kubadirishana mawazo na Ku-have funny!

ENEO

Eneo ambalo kwangu nahisi litakuwa Karibu na nililolizoea ni pale Mlimani City Samaki- Samaki,Ila nyie mnaweza pia mkapendekeza eneo ambalo mtakuwa mnaona mko- Comfortable kuenjoy.

Nimependekeza hao wanawake kwa siku ya Kesho kwasababu gharama za kuwamudu ninazo,watakula watakacho na kunywa watakacho!.

Nia na Lengo ni kuondoa huu utata wa kudhani nyie ni madume,naombeni mnidhitishie kwa vitendo hiyo Kesho.

Wengi wenu nafahamu mnao usafiri wenu binafsi lakini itakuwa vema kila mmoja akatumia Uber au Bolt ili tuweze kuwa Comfortable zaidi(Ili wasiokuwa na usafiri wasijisikie vibaya).

Fedha ya Usafiri nitalipia mimi,wala msijali!

Naomba kufahamu ratiba zenu nyote niliowatag ili nijue nafanyaje,nitakapojua ratiba zenu nitapanga muda sahihi wa sisi kukutana pale!.

Lengo si kutongozana wala mambo ya Ajabu,Lengo ni kufahamiana tu!.


Nawasilisha!
 
Back
Top Bottom