...miongoni mwa dhambi ya wageni wote waliokuja afrika ni pamoja na kupindapinda ukweli, mfano huo wa ati "zanzibar hapakuwa na maisha rasm"...lol..lugha ya wakoloni wote ilikuwa hivyo..!..unasema mshirazi na mwarabu si watu wa mbali..swadakta..je mwafrika na mwarabu? hapa ishu ni ukoloni wa waarabu ktk zanzibar..! kwenye kikao cha wakoloni cha mwaka 1884, sultan wa oman alikuwepo..! na kwenye mgawo alipewa zanzibar na pwani yote ya afrika mashariki(mogadishu to beira)...! hujui hiyo historia? umesomea wapi kaka, arabuni? hunajua kuwa kulikuwa na tawala nyingi ktk afrika lkn sababu hazikuwa na malengo ya kikoloni hazikushirikishwa kwenye mkutano huo...!hivi ndugu yangu we hujui kuwa ukoloni ni ukoloni tu? kisha nakuona we ni "mwelewa", niambie tafsiri ya kisomi ya ukoloni, kisha uniambie ukoloni wa tanganyika ktk zanzibar..mbona unakuwa na hoja za "kichimvi mno" ambazo ni kichekesho kinachoashiria mapungufu ya kujenga hoja kwa mwanazuoni wa kiwango cha kuchangia kwenye jf?...! jamsheed alikuwa msomi yakhe..! msomi kweli kweli..! na anajua kwenda na ukweli na wakati, bahati mbaya waliomzunguka ambao aliwaamini hawakuwa wakimpa ukweli wa mitaani ili afanye mabadiliko yaliyohitajika ambayo yangeepusha dhulma iliyowakuta maelf ya wanyonge ambao walidhulumiwa nafsi zao na mapinduzi matukufu..! stay blessed bro..! salaam!
RED Xs,
Vipi ndugu yangu,yale maafa ya 1964 wewe ndo unaita mapinduzi matukufu!?...khalaf wewe ndo unajinasibisha na Ungazija kweli,au ndo wale Wangazija pori!?
Sasa wewe unamstaajabu Bin Faza,khalaf nawewe si ndo unafanza yaleyale!?
Takriban watu 20,000 kupoteza maisha yao katika siku chache mno ikiwemo; virongwe,watoto,walemavu, wanawake wajawazito...khalaf wewe ndo unaita ati hayo ni mapinduzi matukufu!?
Jingine nakusihi jitahidi uondoshe hiyo mifano ya kidini hapa jamvini,maana italazim wengine kukujibu matokeo yake ghafla jamvi lote litachafuka. Kama wewe ni "Muislamu",basi tumeshakusikia!
Jitahidi kuulindia hishma na hadhi yake huo usomi wako ndugu yangu!
Ahsanta.