Hawa ndiyo wabunge wa viti Maalum CHADEMA, CCM na CUF

Mi nafikiri la muhimu kwanza ni kumpata mwenye moyo wa kukijenga chama kutegemea na uwezo wake wa kujenga hoja na kutoa muda wake kukisaidia chama. Huu ni wakati wa mapambano. Hata Jeshini huwezi kumweka kamanda legelege kwa sababu ati anatoka mkoa fulani. Ujasiri, umakini, na moyo wa kukitumikia chama wakati wa shida na wakkati wa raha ni muhimu zaidi.

Kama wapo wanaotoka mikoa ambayo haikupata wabunge ambao ni majasiri na wanajua kujenga hoja ni vizuri zaidi wakachukuliwa hao. Kama hawapo si vizuri ukamuokota mtu ukamwambia nenda bungeni wakati haoni kuna tatizo.
Kinachozungumzwa hapa ni jinsi ya kujipanga kuenea kwa vuguvugu la mageuzi nchi nzima na si swal la bora mwakilishi. Kuna sehemu ambazo chama hakijaijeng saaana lakini mgombea wake labda amepata kura nying za kumfanya awe wa pili, basi jimbo au mkoa huo watafute mwanachama wa huko anyeweza kukijenga chama. Wa huko sina maana ya kabila bali ukazi.
Bahati mbaya CHADEMA hawakusikilizwa walipopinga utaratibu wa kupeleka majina tume hata kabla ya uchaguzi. hili ndilo linalotakiwa libadilishwe ili vyama viweze kuweka mikakati ya uchaguzi ujao. Ni wazo zuri ila lisitazamwe kama kwamba utaratibu huu utumike irresponsibly na wala wale ambko CHADEMA ndio stronghold wasijisikie kunyang'anywa mkate. Tuweke ujenzi wa chama nchi nzima mbele.
 
Kama mfumo wa kupata watakaochaguliwa kuwa wabunge wa viti maalum utakuwa ni ule uliotangazwa na Kitila Kitumbo basi CHADEMA itakuwa imekosea sana.

Kwa maoni yangu viti maalum visitumike kama asante kwa watu bali kama ni mkakati wa kukiongezea chama mawanda yake na kukijengea umaarufu zaidi kwa jamii.

Kwa mfano kuna haja gani kwa mkoa wenye wabunge wengi wa CHADEMA kupewa tena wabunge wa vii maalum. Na kwenye tayari mbunge wa kuchaguliwa jee kuna haja ya kuteua tena mbunge wa kiti maalum ili afanye nini?

Ingekuwa bora kama CHADEMA ingechagua wabunge wa viti maalum (wanaofaa lakini) kutoka kwenye ile mikoa na majimbo ambayo hayana wabunge wa kuchaguliwa. lengo ni kutumia wabunge hao wa kuteuliwa kama changamoto kwa wabunge wa kuchaguliwa wa CCM (WATCH DOG).

Kilimanjaro ina haja gani tena ya kuwa na mbunge wa viti maalum kuliko Mtwara, au Mbeya mjini kuliko jimbo la Rungwe?

Kaka naona umesahau kuwa chadema ni chama cha kaskazini. Ukabila kwanza, vingine baadaye. Kwa hili wanadhihirisha wazi kuwa wangeshika nchi wachaga wote na wapare wangekuwa ni viongozi wa nchi hii katika kila taasisi. Lakini Mungu ameyaona haya mapema.

Hatudaganyikiiiiiii.:nono:
 
Kaka naona umesahau kuwa chadema ni chama cha kaskazini. Ukabila kwanza, vingine baadaye. Kwa hili wanadhihirisha wazi kuwa wangeshika nchi wachaga wote na wapare wangekuwa ni viongozi wa nchi hii katika kila taasisi. Lakini Mungu ameyaona haya mapema.

Hatudaganyikiiiiiii.:nono:
Nakuonea hruma sana kwa mtazamo wako.
Ila kama ukiamua, waweza pia kuita Mbeya kaskazini, hata Kigoma pia. Unaweza pia kuita Mramba anaekumbatiwa na CCM mkwere vilevile, au muslamu, ni hiari yako.
 
Angalieni mgawanyo usije ukaleta malalamiko ya ukabila........tunajua mikoa ambayo ina upinzani wa kweli km....mbeya,kilimanjaro,arusha,mwanza,kigoma,mara,dar,rukwa,iringa............ni vizuri pia wakachaguliwa kuzingatia nguvu hii ya umma ili kuepusha malalamiko
you are more than 100% right. Wakuu katika chadema, tekelezeni. Ni muhimu
 
Hivi Reggia mtema amechaguliwa kuwa mbunge wa kilombero? maana wengine wanasema wameshinda CCM.msaada wa data pls
 
Utaratibu ni kuwa kila mbunge wa jimbo(wa kuchaguliwa ) anaingiza wabunge wawili wa viti maalum.
kwa mujibu wa katiba ya Jamhuri ya muungano wa Tanzania.

Acha kudanyawa watu. Mwaka 2005 Chadema ilipata wabunge 4, ikapewa mmoja wa viti maalum wakawa watano, hiyo katiba yako in draft au inayotumika?
 
Acha kudanyawa watu. Mwaka 2005 Chadema ilipata wabunge 4, ikapewa mmoja wa viti maalum wakawa watano, hiyo katiba yako in draft au inayotumika?

Wewe mbona pia watudanganya? No research no right to speak!! For your information CHADEMA ilishinda majimbo matano na wakapata viti maalum sita na hivyo kuwa na wabunge 11 na moto wake kila mtu aliuona!!
 
Naona sasa tunaanza kuihalibu jamii forum, kwamba hoja inayoiponda serikali au chama tawala ndio inafaa. kama unataka kuongelea kushuka na kupanda ongelea vyama vyote ili uwe balanced.
 
wana matumaini makubwa hata wewe hujawaona leo pale JK akiapishwa walivyokuwa wanashangilia ....wanajua shavu lipo mlangoni
 
Kinachozungumzwa hapa ni jinsi ya kujipanga kuenea kwa vuguvugu la mageuzi nchi nzima na si swal la bora mwakilishi. Kuna sehemu ambazo chama hakijaijeng saaana lakini mgombea wake labda amepata kura nying za kumfanya awe wa pili, basi jimbo au mkoa huo watafute mwanachama wa huko anyeweza kukijenga chama. Wa huko sina maana ya kabila bali ukazi.

Bahati mbaya CHADEMA hawakusikilizwa walipopinga utaratibu wa kupeleka majina tume hata kabla ya uchaguzi. hili ndilo linalotakiwa libadilishwe ili vyama viweze kuweka mikakati ya uchaguzi ujao. Ni wazo zuri ila lisitazamwe kama kwamba utaratibu huu utumike irresponsibly na wala wale ambko CHADEMA ndio stronghold wasijisikie kunyang'anywa mkate. Tuweke ujenzi wa chama nchi nzima mbele.
Hii ndiyo hoja ya msingi,hapa tunachotaka ni kwa CHADEMA kupingana kwa kila hali na mfumo huu mbovu na wao pia wasiingilie uhuru wa wanawake wa chama chao kuchaguwa watu wa kuwawakilisha hata kwa kisingizio gani kile.

Kama wanawake wao wamekosea kuchagua au uchaguzi wao umeingiliwa na rushwa basi chama kisahihishe makosa hayo lakini mwisho wa siku ni wanawake wenyewe wapewe nafasi ya kuchagua wawakilishi wao,
 
Na bado kuna vile walivyochukua kwa nguvu lazima tuvirudishe mujengoni kupitia The Hague
 
Hii ndiyo hoja ya msingi,hapa tunachotaka ni kwa CHADEMA kupingana kwa kila hali na mfumo huu mbovu na wao pia wasiingilie uhuru wa wanawake wa chama chao kuchaguwa watu wa kuwawakilisha hata kwa kisingizio gani kile.

Kama wanawake wao wamekosea kuchagua au uchaguzi wao umeingiliwa na rushwa basi chama kisahihishe makosa hayo lakini mwisho wa siku ni wanawake wenyewe wapewe nafasi ya kuchagua wawakilishi wao,
Jamani kila chama kina mfumo wake. Uongozi ni zaidi ya hii vita ya madaraka wanayoifanya sisi m jambo ambalo naona wengi hapa wanataka kuja nalo Chadema.

Limeshazungumzwa hapa kwamba utaratibu huo wa kuchaguana wanawake ulileta shida kiasi ambacho tungepata shida walizopata sisi m na sisi kufaidi kwa ugomvi wao. Uongozi imara na wenye busara wa Chadema ukabuni namna yao. Ukatengeneza kamati itakayoshughulikia jambo hili. Na nina hakika hata wakina mama walihusishwa katika kamati hiyo iliyokuwa chini ya Dr Kitila. Msitake kuwapotosha watu hapa na kuzalisha vita ya ki sisi m katika kura za maoni.

Waachie Chadema yao, mwenye ushauri na aweke komenti zake kwenye website yao
Tovuti ya Chama Cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) na watayaangalia.

Hata hivyo ushauri wenu ni chachu kwa maendeleo ya Chadema ingawa chama hakilazimiki kukubaliana nao.
 
CHADEMA haitoi nafasi ya viti maalum kama zawadi na hii inajidhihirisha zaidi na namna inavyowasaidia wanawake jasiri walioshiriki katika mchakaoto wa kukiletea chama ushindi. Tofauti na watani wetu mtu ukiwa viti maalum unakaa kusubiri siku ya kuapishwa. Hebu tuangalie list ya wagombea wa viti maalum wa chadema:

1.Lucy Owenya (Amekuwa mchangiaji na mmoja wa wafadhili wakuu na wakusanyaji hela wa CHADEMA. Ikumbukwe kuwa wafanyabiashara wengi wanaogopa kuchangia chama directly na wanaogopa pia kuchangia kwa Mbowe au Ndesamburo kwa kuwa hawa wanajulikana. Hivyo wako radhi kumpatia fedha Lucy ili aziwakilishe kwenye Chama. Ushindi wa ubunge mkoa wa Kilimanjaro ambako CCM ilikuwa na bajeti ya Bililioni moja umefanikishwa kwa kiasi kikubwa na mchango wa LUCY na Grace Kihwelu).

2.Eather matiko

3. Mhonga Ruhwanya (Chief Strategist kwa kampeni ya Chadema mikoa ya Magharibi. Amempa tough ya kutosha Zito na Mlee wa Kigoma Mjini na wengineo waliogombea mikoa ya Kigoma ambako kulikuwa kugumu mwaka huu kwa kuwa NCCR nayo ilikuwa imewekeza hasa na Chama tawala nacho kilikuwa kimejipanga).

4.Anna Mallac

5. Paulina Gekul (Mgombea mahiri wa CHADEMA jimbo la Babati Mjini. Alipigana kufa na kupona na jabali la Siasa Kisyeri Chambiri na kushindwa kwa kura chache sana. Chambiri alipata 13506 na Pauline alipata 9899

6. Conjesta Rwamlaza
7.Susan Kiwanga

8.Grace Kiwelu (Aliyofanya Owenya ndio aliyofanya Kihwelu. Ametumia utajiri wa familia yake na kujulikana kwao kuleta mafanikia tele kwa CHADEMA)

9. Susan Lyimo (Mbunge wa zamani wa viti maalum na waziri kivuli wa elimu ya juu. Mchango wake kama msomi mchambuzi ulikuwa mzuri na alitetea maslahi ya wananfunzi na walimu katika vyuo. Alikuwa muungwana kuachia jimbo la Kinondoni ligombewe na Mogendi kwa kuwa ilidhaniwa Mogendi angeweza kuleta chachu ya ushindi. Alikuwa miongoni mwa wanamkakati walioshiriki sana kuleta mtazamo chanya wa CHADEMA kwa wasomi wetu).

10. Regia Mtema (Mgombea Mahiri wa Chadema huko Kilombero. Ameshindana kwa nguvu zote na Tapeli la Kimataifa Abdul Mteketa na nusra achukue jimbo kama siyo uchakachuzi wa dakika za Mwisho. (Mteketa alichakachua na kupata 50% ya kura dhidi ya 44% ya Regia - kesi yake imepelekwa Tume)

11.Christowaja Mtinda - Msomi mwenye degree tatu kutoka Mkoa wa Iringa akifundisha Chuo Kikuu cha Mkwawa na mtu anayeshiriki sana shughuli za Chadema huko Iringa na Dar es Salaam: Christowaja Mtinda - WiPaHE Doctoral Scholar, Mkwawa University College of Education

12.Anna Komu - Amepigana vya kutosha CHADEMA Kwanza kama mgombea mwenza wa Mbowe 2005, kama mbunge wa Viti maalum na mwaka 2010 kama Mgombea wa jimbo la Kigamboni. Nusura ashinde lakini uchakachuaji umemponza naye. Amepigana sana na Dk. Faustine Ndugulile wa CCM aliyepata kura 53389 dhidi ya Anna Komu wa Chadema aliyepata kura 25176). Hata hivyo matokeo bado yana mgogoro maana vituo vingi bado havijahesabiwa na wanajeshi walilazimisha matokeo yatangazwe.

13.Mwanamrisho Abama (Mjumbe wa Kamati kuu ya Chadema kutoka Zanzibar na mgombea wa CHADEMA katika jimbo la Chumbuni huko Zanzibar). Kujitokeza kwanke kugombea jimbo la zanzibar akiwa mwanamke ni ujasiri tosha.

14.Joyce Mukya

15. Naomi Kaihula

16. Chiku Abwao: Huyu ni mpiganaji wa kuigwa mfano na ndiye chachu ya Ushindi wa Mchungaji Msigwa pale Iringa Mjini. Kwa waliokuwa kwenye kampeni ya Iringa watakubaliana na mimi nini kimefanywa na Abwao. Kwa waliokuwepo siku ya utangazaji wa Matokeo watakumbuka nini kilifanywa na huyu mama. Ameshakuwa Mbunge kwa muda mrefu pia.

17. Rose Kamil Sukum - Diwani maarufu wa CCM ambaye siku zote ameuwa mpinzani ndani ya CCM. Alichujwa na Nagu kwa mizengwe na kuamua kugombea Hanang kwa tiketi ya CHADEMA. Pamoja na misukosuko aliyokutana nayo wakati wa kampeni iliyomhusisha mzazi mwenzie Dr. Slaa amepigana mno na kuleta kura nyingi kwa CHADEMA. Jimbo lake nalo limechakachuliwa.Kura 21,986 (Kamili)
CCM 34, 338 (Nagu)

18. Christina Lissu Mughiwa (mdogo wa mpambanaji wa CHADEMA Tundu Lisu na mwanaharakati wa siku nyingi wa CHADEMA. Walikuwa ni wapiganaji walioasi chama Tawala na kwenda upinzani. Kaka yao Alute Mugwahi wakili alibaki CCM na aligombea kura ya maoni CCM na kusindwa na Njau ambaye naye alilipiziwa kisasi na Tundu Lisu. Christina na Tundu Lisu wanategemewa kuichangamsha Singida na kuileta upinzani polepole.).

19. Raya Hamisi (Mjumbe wa Baraza Kuu la Wanawake la CHADEMA na mwakilishi wa CHADEMA Zanzibar. Amesaidia sana kuijenga CHADEMA zanzibar ingawa siasa za kule ni ngumu.

20. Philipa Mturano

Maelezo mengine nitawapatia kesho. Hivyo nategemea kuwa mtaona kuwa Chadema si chama cha upendeleo bali nafasi inatoka kwa merit.
Conjesta Rwamlaza
Mwenyekiti wa Chadema kwa muda mrefu tangu kuundwa kwa Chadema mkoani Kagera na sana ni Katibu wa Chama hicho mkoani Kagera. Ni mama mpambanaji, asiyeogopa lolote, jasili wa kukabiliana na dhoruba za aina yoyote. Amekibeba chama hiki Kagera usiku na mchana.

Naomi Kaihula
Mama huyu alikuwa akigombea ubunge katika moja ya majimbo ya Dar-es-salaam ni mwalimu kitaaluma na amekuwa akifundisha katika moja ya shule za sekondari Dar.
 
Leo hinategemewa kutangaza idadi ya viti maalum kwa kila chama.By facebook mr Zitto :israel::israel::israel::israel::israel::israel::israel::israel:kwa hiyo 22+32 Jumla 54 Chadema kitakuwa chama cha upinzani bungeni kwa hiyo idadi ya viti maalum vya ccm vimepunua sana kutoa viti 80 walivyokuwa navyo Idadi hiyo hinatokana na kura za wabunge nchi nzima.sio kra za rais au viti vya wabunge
 
Back
Top Bottom