Hawa ndio Wana JF wenye Ligi na wenye falsafa zao humu ndani

Robert Heriel Mtibeli

JF-Expert Member
Mar 24, 2018
21,340
51,900
Kwema wakuu!

TUlipokuwa tunasoma, tulisoma kina Karl Marx, Wakina Charles Darwin, Kina Pilato, Aristotle na wengineo. Leo hapa JF kuna Watu na Falsafa zao, mitazamo, na nadharia zao. Humu ndani kuna member ambao ni waasisi na ma-father wa Ligi Fulani Fulani. Yaani wao mawazo Yao Kwa sehemu kubwa yamejikita kwenye hizo ligi. Tusipoteze muda.
Orodho ni kama ifuatavyo;

1. Liverpool VPN,
Muasisi wa KATAA NDOA.
Waenezaji WA falsafa hii ni kina dronedrake na wanazuoni wenzake.

2. Smart911
Huyu mdau huwezi kumtenganisha na Falsafa ya "Tatizo la binadamu WA siku hizi ni wabishi Sana"
Yeye mtukane utakavyomtukana, andika utakachoandika lakini jibu lake ndio Hilo.
Hanaga Maneno mengi, unaweza ukadhani hajui Kiswahili,

3. Mshana Jr,
Huyu humu ndani kajipambanua kama Mzee wa ulozi na vilinge,
Anapenda nadharia za ulozi na Uchawi.
Ndiye founder na Father WA ulozi humu, wenzake ni kina Mzizimkavu na Rakims ambao siku hizi wameadimika.

4. FaizaFoxy
Huyu Mama ni Mzee wa "Huko shuleni mmeenda kusomea ujinga"
Huyu falsafa yake imejikita zaidi kwenye Dini ya uislam. Huyu hata kutema mate atataka rejea ya maswahaba wa mtume.

5. Jokajeusi.
Huyu yeye falsafa yake ni "Mwanamke anapaswa Aolewe Bikra"
Yeye kila kitu ni Bikra linapokuja suala la mahusiano.

6. Mpwayungu Village
Huyu yeye ni mwalimu lakini falsafa yake inasema "ualimu ni Laana"

7. Kiranga
Falsafa ya huyu mwamba ni "hakuna Mungu wala Shetani"
Huyu mtabishana mpaka mnyongane,
Yeye humu ndani ndiye Baba WA hiyo Ligi, ingawaje wapo wasaidizi wenza.

8. Demi
Huyu ni mwanamama mwenye falsafa za Haki na usawa baina ya mwanaume na Mwanamke. Yeye na Rebecca, culture me, Mama Wardat, Depal, inapotokea Ligi hasa za usawa au kutetea Wanawake yupo mstari wa Mbele.

9. GENTAMYCINE
Huyu jamaa yeye falsafa zake ni zakujimwambafai, majigambo, mikwala kibao lakini emotional intelligence yake ni sifuri. Huyu analigi nyingi mno na yupo tayari kupambana na yeyote.

10. Istanbul
Huyu ni Mzee wa Ligi za kupambania Wahaya. Utakapowataja Wahaya humu ndani hasa Kwa ubaya huyu jamaa atanunua hiyo kesi na Ligi itaanza Rasmi.

11. Mohamed Said
Huyu Mzee wetu bhana tunamheshimu, yeye Ligi yake kubwa Ipo katika Uislam na Historia na nchi Hii.
Yaani piga ya garagaza hata azungumzie kitu gani ni lazima alinasibishe na Uislam. Anaweza anzia Huko mbali wee, lakini kituo chake utasikia Wazee wa Rufiji sijui wazee wa bagamoyo wakawa ndio wakwanza kulianzisha Jambo Hilo. Namuitaga Mzee wa viambatanisho kwani ni lazima aweke picha alafu aseme, picha hiyo ni Baraza la wazee wa kiislam wa Rufiji wa Wakati huo,

12. MK254
Popote utakapomuona huyu member ujue hapo aidha anaponda Waislam ambao anapenda kuwaita wavaa kobazi, au anawaponda Warusi.
Yeye hiyo ndio kazi yake humu JF, Hana kazi nyingine. Ligi yake ndio hiyo.
Falsafa yake ni kuwa uislamni dini inayokandamiza Haki za Watu wengine hasa Wanawake. Huo ni Mtazamo wake na hakuna sheria ya kuzuia mitazamo ya Watu.

13. Mama D
Huyu falsafa yake ni katika ibada, mambo ya maombi maombi, hapendi fujofujo, anaamini katika Maombi.
Kama utataja Jambo lolote linalohusu malezi na maombi basi huyu Mwanamama atatia timu.

14. Bujibuji
Huyu mwamba yeye falsafa zake ni mrengo wa Kati, uzamani yupo, Usasa yupo. Kutokana na umri wake Ligi haziwezi na hashirikigi Kwa kuhofia kuvunjiwa heshima na watoto wa siku hizi waliovurugwa.
Majibu yake hayatofautiani Sana na Mshana Jr,

15. Extrovert
Huyu falsafa yake ni kukubaliana na kuheshimu mawazo ya wengine.
Wafuasi wenzake ni kina raraa reree.
Ingawaje Extrovert ni mfuasi wa Magufuli hivyo ni rahisi Uvumilivu kumshinda pale unapomzungumzia Jpm Kwa ubaya.

16. Bill Lugano AKA Kidukulilo
Huyu mwamba Kwanza hana Ajira, ingawaje anapiga part-time.
Huyu Hana muda wa kukujibu au kujibizana na watu Kutokana na kuwa kwenye ubongo wake unamabilioni ya fedha. Yeye anaamini mabilioni halipo Ubongoni ndio yanamfanya awe Tajiri.
Hivyo zile Stori zake ingawaje ninyi mtamuona kachanyikiwa lakini yeye anajiona ni kweli mi Tajiri.

17. Pascal Mayalla
Mzee wa "Kwa Maslahi ya Taifa", na "The Voices from Within" huyu jamaa ni muumini wa karma, lakini pia ati anasemeshwaga na Muziki sijui ndio Roho mtakatifu, yaani kuna Sauti ATI inamuongeleshaga😄
Mzee wa Kura moja, Mzee wa ku-declare interest😄😄nafikiri humu JF ndio member pekee akifuatiwa na Popoma ambapo akitoa hoja basi watatokea wapingaji wengi zaidi wakimshambulia direct.
Huyu Ligi yake kuu ukitaka ajitokeze mafichoni basi elezea mambo ya jpm au ya Urais wa Samia in detail, yaani uelezwe mambo ambayo hakuna anayajua. Lazima ajitokeze.

18. To yeye au Beesmom
Huyu falsafa yake ni Mwanaume ni Mwanaume na lazima aheshimiwe, na Mwanamke abaki kwenye nafasi yake.
Anapenda ndoa inayofuata mfumo dume. Anapenda mwanaume anayejua kupiga mzigo. Huyu wanazuoni wenzake wanaofanana tabia ni kina Sophy, Lenie, Bantu Lady, Binti Kiziwi.

19. Luambo Makiadi
Huyu mwanazuoni anaamini kuwa Kanda ya kaskazini ndio inawatu Bora na wenye Akili kuliko Watu wengine hapa nchini. Ukitaka ajitokeze basi itakupasa uiponde Moshi au wachagga hapo lazima umuone.
Hasimu wake katika ulingo ni Instanbul, hawa ni mahasimu katika Ligi hasa ya wachagga na Wahaya. Sio kwamba ni mahasimu wa kuchukiana bali wakugombea Ufahari

Taja wengine wenye Ligi zao humu yaani ukizungumzia Jambo Fulani lazima aje kulitetea au kuliponda Kwa nguvu zote na mtakesha humu, ikiwezekana wapo tayari kupigwa Ban lakini sio kushindwa vita.
 
Back
Top Bottom