Hatimaye serikali yaamua kunyoosha mikono... Gesi sasa kubaki Mtwara!

... CCM wameona - ni bora nusu shari kuliko shari kamili
... bora vijengwe Mtwara mapema kuliko hatua ya yote mawili likiwemo la shinikizo la Chadema kuanika mikataba ya gesi!
 
Wewe unaishi DAR. Ungekuwa Mtwara, 100% ww ni miongoni ya wanaopinga dhuluma. "Wana Mtwara Gas kwanza uhai baadae". Kuwa mwana Mtwara pingana na dhuluma, uhai sio kitu, ukiwa kama serikali utadhalilika, sababu unaemdhurumu kila kunapokucha anakuwa na kitu kipya na kizuri zaidi ya jana. Tuache dhuluma kaka tutaumbuka.
 
Huku ughaibuni tunaishi na wakimbizi kutoka nchi nyingi duniani,
Sisi watanzania ni wakimbizi wa kiuchumi lakini wenzetu ni wa kimbizi wa kisiasa,
katika maana kwamba hawawezi kurudi kwao.

Naona kijna unadharau mwiba.
Serikali ya ki mamruki ya Tunisia iliangushwa baada ya tukio la polisi kumnyanyasa mchuuzi wa mboga(Machinga) bidhaa zake
Kisha kumburuta ili kumuweka lupango, akaamua kijitia kiberiti.
Hakufa bure leo Tunisia,Misri na Libya wameza kuwaondoa mamruki wao kwa sababu ya kijana mchuuzi wa mboga

Hawa watu wanaodai gesi isitoke Mtwara ni walewale wakija Dar tunwaita Machinga.
Machinga ni kabila huko Mtwara.
Huoni kwamba Wanyonge wakianzisha vita, vita hiyo haizimwi kwa Noti au Wadhifa serikalini???

Nakusubiri huku Ughaibuni hivi karibuni utakuja kama mkimbizi wa kisiasa huku umefyata mkia wako na mdomo umeupiga ZIPU



Magaidi wa RENAMO hawawezi kuyumbisha maendeleo ya Tanzania kwa hiyo wana Mtwara wamekanusha vikali wanasiasa uchwara ambao hawana kazi ya kufanya bali kuchonganisha wananchi ilimradi wapate mtaji wa kisiasa. Kifo hakiepukiki kwa vyama TATA
 
Dentist wa Vinywa vya Tembo MH Abdalahaman Kinana.
Yeye hazibi mashimo anang'oa tu.
Haramia la Kiogadeni linapigwa fukuto na washenzi wa CCM
 
Simwamini Pinda.....

Rejea sakata la madaktari na la Jairo!!!!!!

Huyu jamaa ni dhaifu zaidi kuliko JK

Jamaa kaamua kumtolea uvivu JK lakini unajua!! ETI anataka madaraka ya rais yapunguzwe unajua hapa inajenga picha flani kuhusu udhaifu wake huyu.
 
Hakukuwa na njia nyingine zaidi ya serikali kunyoosha mikono kwa kuzingatia yaliyokuwa yanaendelea. Approach nyingine ingemwaga damu nyingi za wananchi, polisi, na viongozi pia na hakuna serikali iko tayari kwa hilo kama inataka kudumu madarakani. Hili lina negative na positive impacts kwenye Taifa hili. Lakini angalau limetuachia somo la kushirikisha wananchi katika miradi ya maendeleo, zama za ubabe na ulevi wa viongozi zimefika mwisho, kuigeuza Dar ni kila kitu ni kosa na walioamua kujiajiri kwenye ufisadi.
 
Kama wana Mtwara wamekubali kupeleka gas Dar basi wameingizwa King............. nasubiri kamatakamata siku chache zijazo!!

Anyway, Mpaka sasa sioni justification ya kutokuzalisha umeme mtwara na kuunganisha kwenye grid. Hivi hivyo viwanda ambavyo vinahitaji gas Dar kwa kiasi cha serikali kujenga bomba kwa gharama kubwa hivyo ni vipi?? Kama ni gas ya kupikia tu majumbani hivi kweli kuna haja ya kutumia gharama zote hizo kuipeleka Dar?? Pinda kapiga blah blah wananchi wanashangilia lakini ukiangalia kwa undani hakuna alichozungumza cha maana. Kama bomba ni kwa ajili ya umeme tu basi nafikiri ni vema kama Mtwara angeendelea kulikataa hilo bomba.
 
Kama wana Mtwara wamekubali kupeleka gas Dar basi wameingizwa King............. nasubiri kamatakamata siku chache zijazo!!

Anyway, Mpaka sasa sioni justification ya kutokuzalisha umeme mtwara na kuunganisha kwenye grid. Hivi hivyo viwanda ambavyo vinahitaji gas Dar kwa kiasi cha serikali kujenga bomba kwa gharama kubwa hivyo ni vipi?? Kama ni gas ya kupikia tu majumbani hivi kweli kuna haja ya kutumia gharama zote hizo kuipeleka Dar?? Pinda kapiga blah blah wananchi wanashangilia lakini ukiangalia kwa undani hakuna alichozungumza cha maana. Kama bomba ni kwa ajili ya umeme tu basi nafikiri ni vema kama Mtwara angeendelea kulikataa hilo bomba.

Ni kweli amewalaghai wananchi wa Mtwara, tatizo viongozi wa CCM wanafikiri wao ni waerevu ila kwa hili wamechemka zaidi. Tulioko Mtwara tunajua nini kinaendelea, wananchi wanasema wajenge kwanza plant ya kusafisha gas ba ya umeme. Sasa kwa uzuzu wao wataanza kuweka mabomba hapo ndipo watawasalimu wanamtwara kwa kimakonde.
 
Kufuatia mgogoro uliodumu kwa muda sasa na kusababisha maafa makubwa huko Mtwara juu ya suala la gesi, Serikali hatimaye imeamua kunyoosha mikono kuhusu uamuzi wake wa kutaka kuipeleka gesi hiyo toka Mtwara kwenda jijini Dar es salaam.

Serikali kupitia Waziri Mkuu pamoja na Mawaziri wengine kwa upande Mmoja na Wawakilishi wa wananchi wa Mtwara imeamua kukubaliana na wananchi hao wa Mtwara walioonesha kuwa ngangali juu ya kutohamishwa gesi hiyo kwenda DSM, hivyo Gesi hiyo sasa itabaki Mtwara.

Taarifa pia inasema kutajengwa mtambo mkubwa wa uzalishaji umeme huko huko Mtwara.


My Take:
Endapo Watanzania tungekuwa na msimamo ktk mambo mengi yahusuyo Taifa kama walivyofanya wananchi wa Mtwara leo hii kusingelikuwa na Mafisadi na tungekuwa mbali sn kimaendeleo. Tunawaomba watu wa Mtwara sasa ni wakati wa kuunga nguvu kutetea twiga wetu wanaosafirishwa nje, mabilioni ya uswiss, nk. Kwa pamoja Kuifikia Tanzania tunayoitaka Inawezekana. Nazidi kuwapongeza sana wananchi wa Mtwara.



Source: Hotmix Eatv

Hii taarifa imetoka wapi? Manake mpango wa kujenga "...... mtambo mkubwa wa uzalishaji umeme huko huko Mtwara." ulikuwepo tangu zamani. In fact, sasa hivi gesi ya Mnazi Bay inabadilishwa kuwa umeme pale Mtwara mjini ambapo kuna 12MW tayari zinasambazwa Mtwara na Lindi.

Hii taarifa potofu - umeitunga tuu humu.
 
Mhh...Mbona kuna taarifa tofauti kutoka Mtwara kwenyewe ? Angalia habari hii kutoka MTWARA KUMEKUCHA blog

MTWARA KUMEKUCHA



DONDOO MUHIMU KATIKA MAJUMUISHO

  • Mkuu wa Mkoa wa Mtwara Kanali Mstaafu Simbakalia kawaomba radhi wananchi wa Mtwara.

  • Waziri Nchimbi kutumia lugha kibabe na vitisho dhidi ya raia pamoja na taarifa isiyokuwa na tathmini halisi na yenye uwiano pale alipotolea mfano askari aliyevamiwa dukani/baa yake na kuibiwa pesa kiasi cha sh. 1,895,oo/= na Kupoteza mali ya sh 200,000,00/= (milioni mia mbili) na kusababisha watu wagune.

  • Kawambwa kawahimiza wazazi kuwaruhusu watoto kwenda shule kupata elimu sanjari na chuo cha VETA kutoa masomo ya mitaala ya gesi sanjari na uchomeleaji baharini.

  • Tibaijuka amezungumzia kuhusu upanuzi wa mji wa Mtwara na kuleata kauli mbiu ya "Amani na maendeleo" kutoka kwao Kagera.

  • Mwakyembe amezungumzia upanuzi wa bandari kavu na ujenzi wa reli Mtwara, Liganga, Mchuchuma hadi Mbamba bay na kuahidi kuja Mtwara kila baada ya miezi 3 na kujadili na kutathmini changamoto.

  • Waziri Mkuu ametoa udhuru wa waziri wa ujenzi Dr Magufuli ambaye alitakiwa kuwepo lakini hataweza kuhudhuria.

  • Bi Mapunjo kaahidi mipango mikubwa ya ujenzi wa viwanda mkoani Mtwara.

  • Mbilinyi kaainisha idadi ya makampuni yaliyoonyesha nia ya kuja kuwekeza Mtwara (Sina hakika sana kama ni Mtwara).

  • Waziri Mkuu katoa majumuisho ya ziara yake ambayo hayana tofauti na haya yaliyojadiliwa.

  • Kwa ufupi ni sarakasi, sanaa, ngonjera, kwaya na maigizo hakuna jipya.



Hamna lolote hapo! Changa la macho hilo!! WanaNtwara wasidanganyike hata kidodgo!! Pinda na Mwakyembe ni watu waongo sana!! Shikilieni msimamo wenu ulele: GESI HAITOKI NTWARA
 
Wajenge viwanda na sio pipeline Wana mtwara Mimi nimeshtukia hiyo ni kupoozwa kazi iendelee naibu waziri kasema Wana mtwara hamjasoma kwa iyo fursa yenu ni kuuza chapati na mandazi kwa wachina Leo pinda anawaadaa na mambo mengi siku zote walikuwa wapi? Au baada ya kuonekana gas? Msikubali
Khaa!! wewe vipi?? wameshakubaliana kuwa gesi itasafishiwa Mtwra itasafirishwa hadi Dar kwa ajili kuwasha majenereta kisha umeme utarudishwa mtwara. hivyo pipeline lazima ijengwe. JIULIZE KWANZA kabla hujakurupuka
 
Hakukuwa na njia nyingine zaidi ya serikali kunyoosha mikono kwa kuzingatia yaliyokuwa yanaendelea. Approach nyingine ingemwaga damu nyingi za wananchi, polisi, na viongozi pia na hakuna serikali iko tayari kwa hilo kama inataka kudumu madarakani. Hili lina negative na positive impacts kwenye Taifa hili. Lakini angalau limetuachia somo la kushirikisha wananchi katika miradi ya maendeleo, zama za ubabe na ulevi wa viongozi zimefika mwisho, kuigeuza Dar ni kila kitu ni kosa na walioamua kujiajiri kwenye ufisadi.

Hapo kwenye RED: Jamani serkali haijasalimu amri!!! Kilichofanyika ni kuwapiga changa la macho watu wa Ntwara, basi!!!
 
All along kulikuwa na two plans, first was the pipeline to Dar cause it is urgent and second was the power plant in Mtwara.
And this is what is going to happen!

The only thing govt did is something they should have done long time ago: to explain the master plan to wanamtwara so that they understand.

Instead govt ikawapuuza Wanamtwara kama kawaida yao kupuuza maombi ya wananchi.
And ofcourse wanasiasa wakachochea moto.

Haya yote yangeepushwa kama kungekuwa na TRANSPARENCY ya master plan!
 
kama ccm hili linawashinda hadi wanashindwa kujua wapi pa kutokea, ni wasiwasi sana kama kikwete atafika mwisho wa term yake.
 
Hapo kwenye RED: Jamani serkali haijasalimu amri!!! Kilichofanyika ni kuwapiga changa la macho watu wa Ntwara, basi!!!
Siyo kuwapiga changa la macho bana, kuwapa ukweli waliokuwa wamepotoshwa!! wao blue waliambiwa ni white
 
KWA NINI MIKATABA YA GESI INAFICHWA?

KWA NINI SERA YA KUONGOZA UTAFUTAJI NA UVUNAJI WA GESI INA ANDIKWA SASA BAADA YA KUSAINI MIKATABA NA MAKAMPUNI 26 NA KUANZA MIRADI/KUKOPA HELA ZA MIRADI?????

KIONGOZI WA SAFARI ANAYE WEKWA WAKATI SAFARI IMEFIKA UKINGONI NI KIONGOZI HEWA, NA UONGO.

Hiyo mikataba ndio imeongoza utafutaji wa gesi na ndio inaongoza uvunaji wake, iwekeni wazi watanzania tuione,,,,
 
kesho na sisi tunalianzisha huku nyamongo!!watu wa Mtwara wametutoa tongotongo!

Samaki mkunje angali mbichi, nyie mlishachelewa. Wakati Afrika Mashariki Gold Mine (AMGM) inaingikatika miaka ya 90, wawakilishi wenu walisaini mikataba kama ya Chief Mangungo na kupewa ahadi kede kede kwa mikataba binafsi - Chezea Jerf + Boscow weye !!! . AMGM (Jerf) walivyokuwa wajanja wakauza Kampuni kwa Barick. Sasa mtalianzisha kwa nani miaka 20 baadaye, wakati mara ya kwanza mlikubali. Labda kama wataanza kuchimba maeneo tofauti Nyabirama, Matongo na Nyabigena. Majuto ni Mjukuu.
 
Kama ni kweli, japokuwa simuamini Pinda basi Serkali ya kikwete itegemee migogoro mingi toka maeneo mengine! Walitakiwa kusimamia kauli sio kufuata upepo! "Dhaifu"

Maamuzi kama haya yalitakiwa mapema kabla ya fujo kuanza. Tunashukuru kama serikali itatekeleza kwa dhati.
 
Back
Top Bottom