Hatimaye Mahakama Kuu yaamuru DOWANS walipwe

Mwana Mpotevu

Platinum Member
Sep 7, 2011
3,295
2,500
Pamoja na kelele zetu zote, hatimaye mahakama kuu imesema Dowans lazima walipwe;

James Magai

MAHAKAMA Kuu Kanda ya Dar es Salaam, imetupilia mbali maombi ya Shirika la Umeme Tanzania (Tanesco) kutaka isitishe utekelezaji wa malipo ya Sh96 bilioni kwa Kampuni ya Kufua Umeme ya Dowans kutokana na kuvunja mkataba wa kibiashara kinyume na sheria.

Kufuatia uamuzi huo, Tanesco sasa inatakiwa kuilipa Dowans kiasi hicho cha fedha ambacho kwa ujumla kinaliongezea shirika hilo mzigo wa madeni.

Tanesco kupitia mawakili wake Rex Attorneys iliwasilisha mahakamani hapo maombi mawili; kibali cha kukata rufaa kupinga hukumu ya Mahakama hiyo iliyotolewa Septemba 28, 2011 na kuomba kusimamishwa kwa utekelezwaji wa hukumu hiyo.

Katika hukumu ya awali iliyotolewa na Jaji Emilian Mushi, mahakama hiyo ilikubali maombi ya Tuzo kwa Dowans iliyotolewa na Mahakama ya Kimataifa ya Usuluhishi wa Migogoro ya Kibiashara (ICC), Novemba 15, 2010.

ICC iliamuru Tanesco kuilipa Dowans fidia ya Dola za Marekani 65,812,630.03, kutokana na kuvunja mkataba wa kibiashara kinyume cha sheria. Mahakama Kuu Tanzania ilikubaliana na tuzo hiyo na kuipa kampuni hiyo nguvu ya kisheria.

Hata hivyo, Tanesco haikuridhika na hukumu hiyo, badala yake ikawasilisha mahakamani hapo taarifa ya kusudio la kukata rufaa kuipinga.

Jana, kwa mara nyingine mahakama hiyo iliendelea kubariki Dowans kupewa tuzo hiyo na kutupilia mbali maombi ya Tanesco, ikiwamo pingamizi la utekelezaji wake.

Katika uamuzi wake aliousoma jana asubuhi, Jaji Dk Fauz Twaib alikubaliana na hoja za Wakili wa Dowans, Kennedy Fungamtama kwamba mahakama hiyo haina mamlaka kisheria kusimamisha utekelezaji wa malipo hayo baada ya hukumu ya ICC.

Awali, wakili Fungamtama katika hoja zake, alidai kuwa maombi hayo yamefunguliwa chini ya Kanuni ya 11 (2) na ya 47 ya Mahakama ya Rufani ya Tanzania ya mwaka 2009.

Alidai kuwa kanuni hiyo ya 47 inatumika kwa maombi ambayo Mahakama ya Rufani na Mahakama Kuu nchini zina mamlaka ya kisheria lakini, katika maombi hayo ya Tanesco kusimamisha utekelezaji wa malipo hayo, mahakama kuu haina mamlaka hayo.

Lakini, Jaji Dk Twaib alikubaliana na hoja za wakili Fungamtama kwamba kifungu cha kanuni ambacho Tanesco ilikitumia katika maombi hayo, hakiipi mamlaka Mahakama Kuu kusimamisha utekelezaji wa hukumu zake.

Jaji Dk Twaib alisema kuwa, namna na masharti ya kusimamisha utekelezaji wa hukumu yalivyoainishwa katika kifungu (d) cha kanuni hizo za Mahakama ya Rufani.

Alisema kama Wakili Fungamtama alivyoeleza kwa usahihi, kanuni hizo zinaihusu Mahakama ya Rufaa tu kama ilivyoainishwa vizuri katika Kanuni ya 3 ya Kanuni za Mahakama ya Rufaa za mwaka 2009.

“Mheshimiwa Jaji Mkuu anatambua msimamo wa kisheria uliowekwa katika maamuzi mbalimbali kwa misingi kwamba, mchakato wa rufaa unapokuwa umeanza kwa kuwasilisha taarifa ya kusudio la kukata rufaa, mahakama hii inakoma kuwa na mamlaka ya kusimamisha utekelezaji wa hukumu,”, alisema Jaji.

Jaji Dk Twaib alisema mahakama hiyo inaweza kuwa na mamlaka hayo kabla kuwasilisha taarifa ya kusudio la kukata rufaa.

“Mara tu taarifa ya kusudio la kukata rufaa inapokuwa imewasilishwa (kama ilivyo katika kesi hii), Mahakama Kuu inakoma kuwa mamlaka,” alisisitiza Jaji Dk Twaib na kuongeza:

“Kwa misingi iliyoelezwa mahakama hii haina mamlaka ya kisheria kushughulikia maombi ya kusimamisha utekelezaji yaliyowasilishwa na muombaji (Tanesco)”, alihitimisha uamuzi wake Jaji Dk. Twaib.

Sakata lenyewe Mwaka juzi jopo la majaji watatu wa ICC lilitoa uamuzi wa kuitaka Tanesco kuilipa Dowans Tuzo ya Sh96 bilioni, kutokana na madai ya kuvunja mkataba wa kibiashara kinyume cha sharia.

Hata hivyo, uamuzi huo umekuwa ukipingwa na baadhi ya watu wakisema Dowans ilirithi mkataba haramu wa Richmond hivyo, mkataba huo haukuwa halali.

Tanesco nayo kwa upande wake, katika maombi yake ilidai kuwa kama mchakato wa utekelezaji wa hukumu hiyo utaendelea, itaathiri uwezo wake wa kuzalisha na kusambaza umeme nchini na hivyo kusababisha tatizo kubwa la ukosefu wa umeme nchini na hivyo kuathiri uchumi wa nchi kwa jumla.


Haya Tujiandae kuchanga mchango watanzania wote tuilipe Dowans
 
Pamoja na kelele zetu zote, hatimaye mahakama kuu imesema Dowans lazima walipwe;

James Magai

MAHAKAMA Kuu Kanda ya Dar es Salaam, imetupilia mbali maombi ya Shirika la Umeme Tanzania (Tanesco) kutaka isitishe utekelezaji wa malipo ya Sh96 bilioni kwa Kampuni ya Kufua Umeme ya Dowans kutokana na kuvunja mkataba wa kibiashara kinyume na sheria.

Kufuatia uamuzi huo, Tanesco sasa inatakiwa kuilipa Dowans kiasi hicho cha fedha ambacho kwa ujumla kinaliongezea shirika hilo mzigo wa madeni.

Tanesco kupitia mawakili wake Rex Attorneys iliwasilisha mahakamani hapo maombi mawili; kibali cha kukata rufaa kupinga hukumu ya Mahakama hiyo iliyotolewa Septemba 28, 2011 na kuomba kusimamishwa kwa utekelezwaji wa hukumu hiyo.

Katika hukumu ya awali iliyotolewa na Jaji Emilian Mushi, mahakama hiyo ilikubali maombi ya Tuzo kwa Dowans iliyotolewa na Mahakama ya Kimataifa ya Usuluhishi wa Migogoro ya Kibiashara (ICC), Novemba 15, 2010.
ICC iliamuru Tanesco kuilipa Dowans fidia ya Dola za Marekani billion 65,812,630.03, kutokana na kuvunja mkataba wa kibiashara kinyume cha sheria. Mahakama Kuu Tanzania ilikubaliana na tuzo hiyo na kuipa kampuni hiyo nguvu ya kisheria.

Hata hivyo, Tanesco haikuridhika na hukumu hiyo, badala yake ikawasilisha mahakamani hapo taarifa ya kusudio la kukata rufaa kuipinga.

Jana, kwa mara nyingine mahakama hiyo iliendelea kubariki Dowans kupewa tuzo hiyo na kutupilia mbali maombi ya Tanesco, ikiwamo pingamizi la utekelezaji wake.
Katika uamuzi wake aliousoma jana asubuhi, Jaji Dk Fauz Twaib alikubaliana na hoja za Wakili wa Dowans, Kennedy Fungamtama kwamba mahakama hiyo haina mamlaka kisheria kusimamisha utekelezaji wa malipo hayo baada ya hukumu ya ICC.

Awali, wakili Fungamtama katika hoja zake, alidai kuwa maombi hayo yamefunguliwa chini ya Kanuni ya 11 (2) na ya 47 ya Mahakama ya Rufani ya Tanzania ya mwaka 2009.
Alidai kuwa kanuni hiyo ya 47 inatumika kwa maombi ambayo Mahakama ya Rufani na Mahakama Kuu nchini zina mamlaka ya kisheria lakini, katika maombi hayo ya Tanesco kusimamisha utekelezaji wa malipo hayo, mahakama kuu haina mamlaka hayo.

Lakini, Jaji Dk Twaib alikubaliana na hoja za wakili Fungamtama kwamba kifungu cha kanuni ambacho Tanesco ilikitumia katika maombi hayo, hakiipi mamlaka Mahakama Kuu kusimamisha utekelezaji wa hukumu zake.
Jaji Dk Twaib alisema kuwa, namna na masharti ya kusimamisha utekelezaji wa hukumu yalivyoainishwa katika kifungu (d) cha kanuni hizo za Mahakama ya Rufani.

Alisema kama Wakili Fungamtama alivyoeleza kwa usahihi, kanuni hizo zinaihusu Mahakama ya Rufaa tu kama ilivyoainishwa vizuri katika Kanuni ya 3 ya Kanuni za Mahakama ya Rufaa za mwaka 2009.

“Mheshimiwa Jaji Mkuu anatambua msimamo wa kisheria uliowekwa katika maamuzi mbalimbali kwa misingi kwamba, mchakato wa rufaa unapokuwa umeanza kwa kuwasilisha taarifa ya kusudio la kukata rufaa, mahakama hii inakoma kuwa na mamlaka ya kusimamisha utekelezaji wa hukumu,”, alisema Jaji.
Jaji Dk Twaib alisema mahakama hiyo inaweza kuwa na mamlaka hayo kabla kuwasilisha taarifa ya kusudio la kukata rufaa.

“Mara tu taarifa ya kusudio la kukata rufaa inapokuwa imewasilishwa (kama ilivyo katika kesi hii), Mahakama Kuu inakoma kuwa mamlaka,” alisisitiza Jaji Dk Twaib na kuongeza:

“Kwa misingi iliyoelezwa mahakama hii haina mamlaka ya kisheria kushughulikia maombi ya kusimamisha utekelezaji yaliyowasilishwa na muombaji (Tanesco)”, alihitimisha uamuzi wake Jaji Dk. Twaib.

Sakata lenyewe Mwaka juzi jopo la majaji watatu wa ICC lilitoa uamuzi wa kuitaka Tanesco kuilipa Dowans Tuzo ya Sh96 bilioni, kutokana na madai ya kuvunja mkataba wa kibiashara kinyume cha sharia. Hata hivyo, uamuzi huo umekuwa ukipingwa na baadhi ya watu wakisema Dowans ilirithi mkataba haramu wa Richmond hivyo, mkataba huo haukuwa halali.

Tanesco nayo kwa upande wake, katika maombi yake ilidai kuwa kama mchakato wa utekelezaji wa hukumu hiyo utaendelea, itaathiri uwezo wake wa kuzalisha na kusambaza umeme nchini na hivyo kusababisha tatizo kubwa la ukosefu wa umeme nchini na hivyo kuathiri uchumi wa nchi kwa jumla.


Haya Tujiandae kuchanga mchango watanzania wote tuilipe Dowans


Re: Red mark
Shirika la TANESCO halijawahi kuwa na pesa hata useme limeongezew mzigo mkuu. Mzigo ni wa mimi na wewe. Viongozi wa nchi hii nawakubali kwa jinsi wanavyocheza kama Gaucho. Wanajipasia mapande ili wakakutane nayo mbele
 
Re: Red mark
Shirika la TANESCO halijawahi kuwa na pesa hata useme limeongezew mzigo mkuu. Mzigo ni wa mimi na wewe. Viongozi wa nchi hii nawakubali kwa jinsi wanavyocheza kama Gaucho. Wanajipasia mapande ili wakakutane nayo mbele

Hapa kuna watu wanataka kuigawana keni ya taifa waitumbue vizuri.
 
Kesi hii alitakiwa asimame werema,
Ila kwasababu kulikuwa na malafide wamelipwa wapuuzi flani wajikoseshe ili watu flani wapige hela.
Kidumu chama cha majambazi.

Sent from my BlackBerry 9700 using JamiiForums
 
Jamani wawalipe yaishe... kadizo!!!!
Laiti tungejuwa ni nani anayelipwa.Kwanini ilikuwa ngumu sana kumtaja mmiliki wake?hata mkuu mwenyewe aligoma kumtaja.Hilo linawezekana only in Tanzania.Kampuni inayoingia mkataba ba serikali halafu eti mmiliki hatajwi,na hbajulikani na wananchi.Na sasa analipwa,bado hatujui tunamlipa nani,only in Tanzania
 
Kesi ya ziwa Nyasa ikipilekwa mahakamani tegemea matokeo ya namna hii...
Sheria, common sense na siasa ni vitu tofauti kabisa...
 
Laiti tungejuwa ni nani anayelipwa.Kwanini ilikuwa ngumu sana kumtaja mmiliki wake?hata mkuu mwenyewe aligoma kumtaja.Hilo linawezekana only in Tanzania.Kampuni inayoingia mkataba ba serikali halafu eti mmiliki hatajwi,na hbajulikani na wananchi.Na sasa analipwa,bado hatujui tunamlipa nani,only in Tanzania

Brigedia mstaafu Al Adawi
 
Ni kwanini walioishiriki kuandaa mkataba wa Richmond na Dowans wasishtakiwe kwa kuliingiza Taifa katika hasara kubwa hivi, hasa mwanasheria mkuu wa serikali waziri wa nishati na madini na wengine waliohusika directly and indirectly. Lakini sitashangaa kuona hilo kutofanyika kwa kuwa waliohusika ni watawala na wananchi ni mbumbumbu wala wengine hawajui nini kinaendelea Tz. Na wale wanaofahamu kidogo wanaona ni sawa tu kuilipa Dowans. Hii inaonesha uzalendo zero.
 
Wanasheria ndio watujuze. Kwa namna mkataba ulivyoandaliwa huenda haman njia ya kukwepa/kukataa kulipa. Ndani ya mkataba owner wa Dowans yupo. Majai wetu kwa kufuata sheria zilizopo watakuwa wamefanya kazi yao inavyotakiwa. Kama wameenda kinyume vilio vyo Watanzania vitawamaliza mmoja baada ya mwingine. Mahali popote duniani HAKI prevails.
 
ni kwanini walioishiriki kuandaa mkataba wa richmond na dowans wasishtakiwe kwa kuliingiza taifa katika hasara kubwa hivi, hasa mwanasheria mkuu wa serikali waziri wa nishati na madini na wengine waliohusika directly and indirectly. Lakini sitashangaa kuona hilo kutofanyika kwa kuwa waliohusika ni watawala na wananchi ni mbumbumbu wala wengine hawajui nini kinaendelea tz. Na wale wanaofahamu kidogo wanaona ni sawa tu kuilipa dowans. Hii inaonesha uzalendo zero.

hawa washughulikiwe kwa uzembe lakini maadamu walishatuingiza mkenge kulipa hatuna ujanja. Wanatakiwa adhabu kali sana ila inashangaza si serikali si wabunge wote kimya! Rushwa kweli ni adui wa haki.
 
Back
Top Bottom