The Analyst
JF-Expert Member
- Feb 26, 2011
- 464
- 246
Wakuu tutafakari mambo haya kwa kina.
CCM na M/kiti wao waliahidi kujivua gamba ili waweze kukubalika kwa jamii ya Tz. Kwa bahati mbaya wameshindwa (Binafsi, nilijua tangu mwanzo wasingeweza kwa kuwa JK ndiye aliyeahidi). Cha ajabu sasa kupitia Nape, wanajaribu kujenga hoja kwamba hata wengine ni Mafisadi pia. Sijui lengo ni nini hasa but that's it!
Naandika thread hii kutokana na watu wengi kupoteza muda kujadili nani fisadi zaidi kati ya CCM na viongozi wa CDM. Personally sihitaji kuingia huko sana kwa kuwa nahisi hapana umuhimu tena kwa kuwa kinachotusababishia maisha magumu hapa nchini si malori ya Mbowe wala Mshahara wa Dr. Slaa. Wenye akili timamu wote mnajua Tanzania inatapatapa kwa kuwa Ikulu kuna mtu aliyeshindwa kazi. Anayebisha asiishie kuandika pumba hapa jukwaani badala yake afuatilie hotuba ya JK kwenye semina elekezi (Anaomba Mawaziri wasiofuata taratibu wajiondoe wenyewe. What the hell.....?)
Watu kama Nape wameamua kutumia muda mwingi mno kuzungumza na kutumia sekunde chache sana kusikiliza na kutafakari, ndiyo maana jamaa anapoteza muda kuelezea ufisadi wa malori ya Mbowe na Mshahara wa Slaa. Angetumia japo dakika moja kwa siku kusikiliza hoja za watu na kutafakari mantiki zake sina shaka angechagua kuwa mkimya. Kasoro za CCM zimevuka kuwa chama cha Mafisadi na kufikia hatua ya kushindwa kabisa kufanya kazi yoyote ya maana kwa ajili ya wananchi. Ndiyo maana nasema hata kama Mbowe na Slaa wangekuwa mafisadi kweli bado CCM inaendelea kuwa hatari kwa wananchi na taifa letu kuliko CDM na njia nzuri ya kuliokoa taifa letu ni kuwaondoa madarakani.
Imagine uchaguzi uliopita tu; JK kaponea chupuchupu kuingia ikulu kwa maguvu lakini leo yupo malalamikoni dhidi ya mawaziri. Jamaa anafikiri madaraka yote ya kuteua na kutengua uteuzi amepewa ya nini kama si kuondokana na wasioweza ila kazi ziende?
Nape amesema mengi sana ikiwa ni pamoja na ukabila wa CDM lakini hajatuambia ni Chama gani kitaifaa nchi kwa kuwa wao (CCM) tayari wamekubali viongozi wao ni wachafu lakini hawajawafukuza kwa kuwa watajitoa wenyewe. Binafsi, najua hakuna siku JK atajitoa CCM kabla ya 2016.
Kauli yangu ni kwamba wanasiasa wengi katika nchi zetu ni wabinafsi kwa hiyo naogopa kumtetea mtu yeyote anayejiita mwanasiasa kwa kuwa uwazi wa tabia yake unajulikana kwa unakika zaidi anapokuwa madarakani tayari. Lakini hapa tulipo CCM mmeishiwa hoja sawa na mnavyoshindwa kuongoza nchi.
CCM na M/kiti wao waliahidi kujivua gamba ili waweze kukubalika kwa jamii ya Tz. Kwa bahati mbaya wameshindwa (Binafsi, nilijua tangu mwanzo wasingeweza kwa kuwa JK ndiye aliyeahidi). Cha ajabu sasa kupitia Nape, wanajaribu kujenga hoja kwamba hata wengine ni Mafisadi pia. Sijui lengo ni nini hasa but that's it!
Naandika thread hii kutokana na watu wengi kupoteza muda kujadili nani fisadi zaidi kati ya CCM na viongozi wa CDM. Personally sihitaji kuingia huko sana kwa kuwa nahisi hapana umuhimu tena kwa kuwa kinachotusababishia maisha magumu hapa nchini si malori ya Mbowe wala Mshahara wa Dr. Slaa. Wenye akili timamu wote mnajua Tanzania inatapatapa kwa kuwa Ikulu kuna mtu aliyeshindwa kazi. Anayebisha asiishie kuandika pumba hapa jukwaani badala yake afuatilie hotuba ya JK kwenye semina elekezi (Anaomba Mawaziri wasiofuata taratibu wajiondoe wenyewe. What the hell.....?)
Watu kama Nape wameamua kutumia muda mwingi mno kuzungumza na kutumia sekunde chache sana kusikiliza na kutafakari, ndiyo maana jamaa anapoteza muda kuelezea ufisadi wa malori ya Mbowe na Mshahara wa Slaa. Angetumia japo dakika moja kwa siku kusikiliza hoja za watu na kutafakari mantiki zake sina shaka angechagua kuwa mkimya. Kasoro za CCM zimevuka kuwa chama cha Mafisadi na kufikia hatua ya kushindwa kabisa kufanya kazi yoyote ya maana kwa ajili ya wananchi. Ndiyo maana nasema hata kama Mbowe na Slaa wangekuwa mafisadi kweli bado CCM inaendelea kuwa hatari kwa wananchi na taifa letu kuliko CDM na njia nzuri ya kuliokoa taifa letu ni kuwaondoa madarakani.
Imagine uchaguzi uliopita tu; JK kaponea chupuchupu kuingia ikulu kwa maguvu lakini leo yupo malalamikoni dhidi ya mawaziri. Jamaa anafikiri madaraka yote ya kuteua na kutengua uteuzi amepewa ya nini kama si kuondokana na wasioweza ila kazi ziende?
Nape amesema mengi sana ikiwa ni pamoja na ukabila wa CDM lakini hajatuambia ni Chama gani kitaifaa nchi kwa kuwa wao (CCM) tayari wamekubali viongozi wao ni wachafu lakini hawajawafukuza kwa kuwa watajitoa wenyewe. Binafsi, najua hakuna siku JK atajitoa CCM kabla ya 2016.
- Vyombo vya habari vikiwanukuu viongozi wa Jiji la Dar es salaam (Ippmedia) vinadai hata Magufuli tunayedhani anajitahidi kutekeleza wajibu wake anadaiwa kung'ang'ania uondoaji wa Mabango ktk barabara kuu ili kumkomoa adui yake ambaye hata hivyo hakutajwa. Pia kwa mara nyingine swala la urais limetajwa. Sijaamini bado maneno haya lakini ndiyo yamesemwa na miongoni mwa Magamba. So, hata Mzee Pombe urais ndiyo unampagawisha! Kweli CCM Nyoka na magamba yake.
- Nape (ktk CCM) anadaiwa kushangilia kujivua magamba kwa kuwa alitaka Lowasa na Rostam wapotee kabisa maana wao ni kikwazo kwa ambitions zake za uongozi.
- JK hawezi kuchukua hatua kwa mafisadi wakubwa kwa kuwa ni wafadhili na rafiki zake.
- Spika Sitta aliruhusu Kamati ya Mwakyembe kumsulubu Lowasa kwa kuwa jamaa walikula pasipo kumgawia chake. Naye alipohojiwa juu ya posho mbilimbili aligeuka mbogo.
- Orodha ni ndefu lakini ujue katika CCM hakuna anayefanya kazi kwa nia ya kuisaidia nchi kwa dhati isipokuwa unafiki na ajenda binafsi za siri. Nisinukuliwe vibaya hapa maana yote haya yanaelezwa na Magamba wenyewe si CDM wala mimi.
Kauli yangu ni kwamba wanasiasa wengi katika nchi zetu ni wabinafsi kwa hiyo naogopa kumtetea mtu yeyote anayejiita mwanasiasa kwa kuwa uwazi wa tabia yake unajulikana kwa unakika zaidi anapokuwa madarakani tayari. Lakini hapa tulipo CCM mmeishiwa hoja sawa na mnavyoshindwa kuongoza nchi.