Hasara zipi unazipitia kwa kuwa na tabia za introvert?

Tabia ya kupenda kukaa peke yangu bila kuwa na mazoea sana na washakaji ama majirani, kuna siku niliumwa wakuu nikakaa ndani siku nzima nakunywa maji tu hakuna anayejua kama naumwa.

Homa ilinikamata vibaya nje sionekani washakaji na majirani wakajua ndio kawaida yangu kuwa ndani kumbe mwenzao maji ya shingo, niko mbali na familia, wife hayupo.

Nikapiga simu kwa wife, wife akasema huyu jamaa atakufa kwa sababu ananijua sina kampani, wife akasafiri kesho yake akaja ndio ikawa afadhali yangu maana ugonjwa ukiwa peke yako unazidi.

Nikasema nikipona mimi jamani ntatafuta washkaji wa kutembeleana ili nikipata matatizo nisaidiwe, baada ya wiki kupona ndio kwanza nikazidi kujichimbia ndani na vitabu vyangu uchwara

Nashauri wakuu tujitahidini kuwa na watu wa karibu washkaji ama majirani, mimi imenishinda kidogo.
Jitahidi na wewe Sasa unakubalije kushindwa
 
Mkuu naona shida hatari.

Hasa stori za mipira na baba ake daimond
Mh Sasa watu wa hivi pindi wanapopata matatizo ua na msongo wa mawazo sana na hawakawii kujiua au kufanya tukio litakalopelekea kujuta huko mbeleni maana wanakuwaga na hasira mno.
 
Mh Sasa watu wa hivi pindi wanapopata matatizo ua na msongo wa mawazo sana na hawakawii kujiua au kufanya tukio litakalopelekea kujuta huko mbeleni maana wanakuwaga na hasira mno.
Mimi sijswahi kuwa na hasira hizo.

Ila nina mshkaji wangu yuko kenya ni mshkaji kishenzi,nikipata jambo gumu la stress nalipunguzia kwake nyongo inapungua kidogo mambo yanaenda,mana kuna mambo huwezi kumuambia wife unayamaliza juu kwaju
 
Mimi sipendi kelele ya aina yoyote. Connection niliyonayo ni ya watu ninaofanya nao kazi. Sikuwa mzungumzaji tangu nilivyokuwa shule. Wengine waliniita mkimya, wengine waliniita kauzu. Wengine wakasema huyu wakishua hapendi bughudha na watu.

Starehe yangu muvi, kucheza game, kula na sasa hivi nina plan ya kujifunza kutembelea mbuga na hata mikoa tofauti kwa kutumia likizo zangu ili nijifunze zaidi kuhusu mazingira na maisha kwa ujumla. Imenifanya muda wangu mwingi nimekuwa najifunza mambo tofauti na kusoma vitabu tofauti vya dini vya maarifa na kuhusu mambo mbalimbali.

Vipindi ninavyovipenda unaweza ukaniita dingi! Taarifa ya habari, channel inayoitwa Investigation Discovery, National Geographic, Beyond Belief: Fact or Fiction tangu 2008 nilikuwa naitizama, mpenzi wa You Tube channel zinazohusu watu wanaofanya kilimo na ufugaji wa kuku. Vipindi vinavyohusu ujenzi wa nyumba. Napenda science pia! Imenifanya nawaza tofauti.

Kingine nipo real tu sifeki maisha. Na imenifanya mambo ya ujana mengi siyajui. Sisikilizi radio naona wanachokizungumza si ninachokitaka. Nimeacha kusikiliza tangu 2012 au 2013! Naona wanazungumza ujinga tu na mimi nahitaji vitu vitakavyonijenga.

Kingine imenifanya nafocus kwenye kujenga maisha na kuyafanya yawe bora zaidi. Sipendi ujinga! Sifuatilii mtu labda awe kafanya kitu kinachoigusa jamii ndiyo nitachungulia. Sishoboki na mtu. Hata nikijihisi mpweke kinachonitoa upweke ni kwenda mahali kukaa peke yangu sihitaji bughdha na mtu.

Kingine naamini Mungu yupo. Inanipa amani na furaha ndani ya moyo kwa sababu napenda kumkumbuka.
 
Mimi sipendi kelele ya aina yoyote. Connection niliyonayo ni ya watu ninaofanya nao kazi. Sikuwa mzungumzaji tangu nilivyokuwa shule. Wengine waliniita mkimya, wengine waliniita kauzu. Wengine wakasema huyu wakishua hapendi bughudha na watu.

Starehe yangu muvi, kucheza game, kula na sasa hivi nina plan ya kujifunza kutembelea mbuga na hata mikoa tofauti kwa kutumia likizo zangu ili nijifunze zaidi kuhusu mazingira na maisha kwa ujumla. Imenifanya muda wangu mwingi nimekuwa najifunza mambo tofauti na kusoma vitabu tofauti vya dini vya maarifa na kuhusu mambo mbalimbali.

Vipindi ninavyovipenda unaweza ukaniita dingi! Taarifa ya habari, channel inayoitwa Investigation Discovery, National Geographic, Beyond Belief: Fact or Fiction tangu 2008 nilikuwa naitizama, mpenzi wa You Tube channel zinazohusu watu wanaofanya kilimo na ufugaji wa kuku. Vipindi vinavyohusu ujenzi wa nyumba. Napenda science pia! Imenifanya nawaza tofauti.

Kingine nipo real tu sifeki maisha. Na imenifanya mambo ya ujana mengi siyajui. Sisikilizi radio naona wanachokizungumza si ninachokitaka. Nimeacha kusikiliza tangu 2012 au 2013! Naona wanazungumza ujinga tu na mimi nahitaji vitu vitakavyonijenga.

Kingine imenifanya nafocus kwenye kujenga maisha na kuyafanya yawe bora zaidi. Sipendi ujinga! Sifuatilii mtu labda awe kafanya kitu kinachoigusa jamii ndiyo nitachungulia. Sishoboki na mtu. Hata nikijihisi mpweke kinachonitoa upweke ni kwenda mahali kukaa peke yangu sihitaji bughdha na mtu.

Kingine naamini Mungu yupo. Inanipa amani na furaha ndani ya moyo kwa sababu napenda kumkumbuka.
Sahihi mkuu.

Na mimi nina machache ya kuelezea lakini naona inatosha kuyasoma ya wadau.


Muhimu naona kuwa watu sisi wenye tabia hizi tutumie muda wetu kujinufaisha zaidi kuliko mtu anakaa peke yake huku akifanya ujinga.


Tabia ya kukaa peke yangu imenifanya niwe mtu wa kuwaza tofauti sana,na hili nalishuhudia kwa watu wangu ambao wamekuwa wakinitegemea katika mawazo wakati wao ni watu wazima.

Kwa kweli hii tabia ni nzuri sana,japokuwa mimi nina rafiki angu
 
Back
Top Bottom