Hapa, Waziri Mkuu Majaliwa anakosea sana

Synthesizer

JF-Expert Member
Feb 15, 2010
11,143
18,774
Waziri Mkuu ametoa amri kwamba katika kipendi cha miezi miwili serikali yote iwe imehamia Dodoma.

Japokuwa suala la kuhamia Dodoma limekuwa la muda mrefu, lakini kutoa miezi miwili Wizara ziwe zimehama ni kufanya kazi kutumia nguvu ya siasa badala ya lojiki (lack of rational thinking), hasa ukizingatia mambo yafuatayo;
  • kuhamishia serikali Dodoma ni zaidi ya waziri na katibu mkuu (ambao wengi wana nyumba tayari Dodoma) kuhamia Dodoma. Wizara ni watu
  • kuhamishia serikali Dodoma inatia ndani kuhamishia ofisi zote za ubalozi kwenda Dodoma (je nao unawapa miezi miwili?)
  • kuna suala la kupata majengo na vyumba vya ofisi kwa wafanya kazi
  • kuna suala la malipo ya kuhamisha wafanya kazi na vyombo vyao
  • kuna suala la kuhamisha furniture, computer za ofisini toka Dar kwenda Dodoma
  • kuna suala la kusuka mfumo wa mawasiliano katika ofisi mpya huko Dodoma
  • kuna suala la wafanyakazi kupata sehemu za kukaa huko Dodoma
  • kuna suala la kutatua mambo yanayohusu familia, kama mke au mume ndie anaehama, au kama mke na mume wote ni wafanya kazi hapa Dar wataathiriwaje na kuhama huku
  • kuna suala la watoto wa wafanyakazi hawa walioko mashuleni hapa Dar kuhamia Dodoma
  • kuna suala la baadhi ya familia kutatua suala la nyumba zao watakazoziacha Dar
  • kuna suala la kuwaandaa watu kisaikolojia kuhusu kuhama badala ya kuwahamisha kama vile tuko kwenye state of emergency
  • kuna suala la kuimarisha usafiri wa treni kati ya Dodoma na Dar, ikiwezekana treni za kwenda kasi, kwa kuwa Dar bado itabaki kuwa centre of business na kutakuwa na safari nyingi sana kati ya Dodoma na Dar. Hata viza za kusafiria tutafuata Dodoma. Kufikiria kwamba tutatumia barabara ya Dodoma kama ilivyo ni kuamua kuua watanzania huenda mamia kila mwezi - madereva wetu wa mabasi tunawafahamu - kichaa kapewa rungu. Barabara hii ilishatuulia waziri mkuu, Sokoine.
  • nk
Ukizingatia mambo kama hayo hapo juu, utaona wazi kwamba Waziri Mkuu alitakiwa kutoa miezi kwa kiwango cha chini kabisa, sita, ili kuwe na maandalizi yenye utaratibu ili watu weze kuhama kwa mpangilio, na sio kuhamisha watu kama vile kupeleka kikosi cha jeshi mpakani baada ya kuvamiwa na nchi jirani. Hivi viongozi wetu huwa hawayaoni haya wanapotoa amri? Nashangaa sana awamu ya tano ya uongozi wa Tanzania imejaa amri ambazo zinatolewa kushoto, kulia na katikati bila kufanyiwa tafakari za kina. Hivi kweli hiyo ndiyo filosofia ya "Hapa Kazi Tu"?

Na cha ajabu, Waziri Mkuu anasema kwamba "hatuchezi mchezo wa siasa hapa, tutapitisha sheria katika Bunge mwezi Septemba kufanya suala la kuhamia Dodoma liwe rasmi" (we are not playing politics here...we will pass legislation in parliament in September to make the move to Dodoma official)

Sasa suala la kujiuliza ni kwamba, kama sheria itafikishwa Bungeni Septemba, siku zote hizi suala la kuhamia Dodoma halikuwa rasmi? Na kama sheria ya kuhamia Dodoma itapelekwa Bungeni Septemba, kwa nini Waziri Mkuu anatoa amri juu ya jambo ambalo bado si rasmi kisheria?

Hivi kwa nini viongozi wetu wanadhani kila jambo linahitaji amri kama za kijeshi ili litekelezwe? Je, kutoa amri bila kufikiria athari za kisosholojia na kiuchumi (socio-economic impacts) sio ubwana ambao tuliupinga kwa muda mrefu sana? Frankly, I was expecting much better from my prime minister than this kind of reckless leadership style.

Ushauri wa bure kwa Waziri Mkuu Majaliwa ni kwamba nguzo na nguvu ya taifa lolote iko katika muungano wa kifamilia. Unapovunja familia unavunja nguvu ya taifa. Huko nyuma empire ya Roma ilivunjika kwa sababu ya mvunjiko wa kifamilia. Kwa hiyo hili suala linahitaji utaratibu mzuri, gradual relocation implementation labda katika kipindi cha mwaka mzima, likifanyika kwa kuhamisha wafanya kazi katika kila wizara kwa awamu kulingana na impact zao katika kuendesha Wizara. Sio kuwaambia watu funga virago ondoka nenda Dodoma haraka. La sivyo utaona barua nyingi za kujiuzuru kazi au hata mivunjiko katika familia. Na watu wa ubalozi je, au umeamua serikali yote itakuwa Dodoma na wao wabaki Dar?

Na vyama vya wafanyakazi iweje viko kimya katika hili?
 
“It always seems impossible until it's done’’― Nelson Mandela.

Sisi tumezoea sana porojo kiasi kwamba hata mtu akiwa serious tunadhani ni porojo.

Madawati tu kwenye shule zetu ilikuwa ni porojo kwa muda mrefu na hata Rais Magufuli aliposema suala la uhaba wa madawati lazima tulimalize kwa muda mfupi, kuna wengine walidhani ni porojo zile zile za miaka mingi.

He who knows not and knows not that he knows not is a fool!
 
“It always seems impossible until it's done’’― Nelson Mandela.

Sisi tumezoea sana porojo kiasi kwamba hata mtu akiwa serious tunadhani ni porojo.

Madawati tu kwenye shule zetu ilikuwa ni porojo kwa muda mrefu na hata Rais Magufuli aliposema suala la uhaba wa madawati lazima tulimalize kwa muda mfupi, kuna wengine walidhani ni porojo zile zile za miaka mingi.
Kuwa watashindwa au hawatashindwa sidhani kama ni issue hapa!!

Hivi unafikiri uamuzi huu umeangalia effect zake Kisiasa, Kiuchumi na Kijamii (Politically, Economically and Socially)!!
 
“It always seems impossible until it's done’’― Nelson Mandela.

Sisi tumezoea sana porojo kiasi kwamba hata mtu akiwa serious tunadhani ni porojo.

Madawati tu kwenye shule zetu ilikuwa ni porojo kwa muda mrefu na hata Rais Magufuli aliposema suala la uhaba wa madawati lazima tulimalize kwa muda mfupi, kuna wengine walidhani ni porojo zile zile za miaka mingi.

He who knows not and knows not that he knows not is a fool!

tangu magufuli atangaze suala la madawati ni miezi mingapi? na mpaka leo bado. kisha compare suala la madawati na suala la kuhamisha ofisi zote ndani ya miezi miwili. kujenga ofisi tu, hiyo miezi miwili sio chochote!
 
tangu magufuli atangaze suala la madawati ni miezi mingapi? na mpaka leo bado. kisha compare suala la madawati na suala la kuhamisha ofisi zote ndani ya miezi miwili. kujenga ofisi tu, hiyo miezi miwili sio chochote!
hawa c.c.m hawana akili kweli!ingekuwa hayo madawati yametolewa kutoka ktk bajeti rasmi ya serikali,at least wangekuwa na jeuri ya kujisifu!sasa cha ajabu madawati yenyewe tumewachangia,halafu wanajifanya wajanja kuchukua sifa zote!dadeki
 
Mkuu, tuache kulalamika. Fursa hiyo, kama una vijipesa tutafute viwanja Dodoma na kwenda kujenga huko. Ingawa hata mimi siamini kama ndani ya miezi hi 2 Waziri mkuu kwa maana ya taasisi ya Waziri mkuu inawezekana kuhamia Dodoma, achilia mbali wizara zingine.
 
hawa c.c.m hawana akili kweli!ingekuwa hayo madawati yametolewa kutoka ktk bajeti rasmi ya serikali,at least wangekuwa na jeuri ya kujisifu!sasa cha ajabu madawati yenyewe tumewachangia,halafu wanajifanya wajanja kuchukua sifa zote!dadeki

dah! nimesahau kumwambia hiyo point. nimesahau kama madawati tumewachangia. basi tuwachangie kuhamia dom
 
Kuwa watashindwa au hawatashindwa sidhani kama ni issue hapa!!

Hivi unafikiri uamuzi huu umeangalia effect zake Kisiasa, Kiuchumi na Kijamii (Politically, Economically and Socially)!!
Kwanza lazima uelewe kuwa uamuzi wowote wa serikali una effect zake kiuchumi, kijamii au kisiasa.

Rais amesema litachukua miaka minne kuanzia sasa.

Suala la kuhamia Dodoma lilipitishwa na kuanza kutekelezwa kuanzia mwaka 1974. Labda uniambia kuwa lilikuwa ni kosa kufanya hivyo kwa sababu ya athari za kiuchumi na kijamii.
 
CC msemajiukweli:-
Tofautisha non livingthings na living things. Namaanisha madawati na watu.
Kisha msome kwa kituo mleta uzi. Kaelezea juu ya miundombinu, rasilimali watu, malazi na mahitaji pamoja na sheria.
Ukimwelewa ikosoe serikali yako na viongozi wake na uwaambie wavute subira, wajipange na wasubiri bajeti kwani hii ya sasa waziri mkuu hakuomba fungu. Kuburuzana huku bila kutafakari kutatupeleka kubaya siku isiyo na jina.
Hata nchi zulizohamisha makao take makuu zilizingatia sheria na kuweka bajeti ya kutosha. Jipeni muda kwani kipindi chenu kina muda bado. Kwanini mkurupuke?
 
Mkuu, tuache kulalamika. Fursa hiyo, kama una vijipesa tutafute viwanja Dodoma na kwenda kujenga huko. Ingawa hata mimi siamini kama ndani ya miezi hi 2 Waziri mkuu kwa maana ya taasisi ya Waziri mkuu inawezekana kuhamia Dodoma, achilia mbali wizara zingine.

hahaha!!! ila viwanja vitapanda bei sana asee, waliowahi wameula ila watakaoenda sasa itakuwa noma! inanikumbushia mtwara wakati wa vuguvugu la gesi. viwanja vilipanda bei kuliko dar. halafu hamna kitu mpaka leo
 
tangu magufuli atangaze suala la madawati ni miezi mingapi? na mpaka leo bado. kisha compare suala la madawati na suala la kuhamisha ofisi zote ndani ya miezi miwili. kujenga ofisi tu, hiyo miezi miwili sio chochote!
Nani amekuambia ofisi zote zitahamia Dodoma ndani ya miezi miwili?

Rais amesema zoezi litachukua miaka minne kuanzia alipozungumza.
 
“It always seems impossible until it's done’’― Nelson Mandela.

Sisi tumezoea sana porojo kiasi kwamba hata mtu akiwa serious tunadhani ni porojo.

Madawati tu kwenye shule zetu ilikuwa ni porojo kwa muda mrefu na hata Rais Magufuli aliposema suala la uhaba wa madawati lazima tulimalize kwa muda mfupi, kuna wengine walidhani ni porojo zile zile za miaka mingi.

He who knows not and knows not that he knows not is a fool!
Tafta vitu vya kulinganisha na wala sio hilo, je shule za Dodoma zimeongeza madarasa mangapi kwa kila shule kwa mwaka huu? au unadhani watoto watakaohamia uko watasoma vipi ? Nyumba za kupanga nazo vipi? hii ni kutaka kuongeza ugumu wa maisha kwa watumishi wa umma na kwa kifupi ni aina flani ya UKATILI
 
Back
Top Bottom