tindikalikali
JF-Expert Member
- Jan 14, 2011
- 4,855
- 1,117
Habari za jioni wadau? Nipo nabadilishana mawazo na rafiki yangu ambaye anataraji kuajiriwa na kuwa mwalimu, lakini anachonishangaza eti hataki mwanaume ambaye ni mwalimu kama yeye. Jamani hivi mliobahatika kukutana na walimu wana mawazo kama haya au ni huyu tu na tamaa zake? Maana naona kama ananitega, kwani msisitizo wake eti sisi/mimi tuna uhafadhali kwani kuna semina, safari na vikao. Anadai akiolewa na mwalimu hawataweza kusongesha maisha. Ninachojiuliza, hivi hata akipata mwanaume asiye mwalimu kutakuwa na mapenzi ya kweli?