Hamad Rashid na wenzake mahakamani leo

hasan124

JF-Expert Member
Jan 2, 2012
716
128
MHE. Hamad Rashid na wenzake Leo wako mahakamani kuisikiliza kesi Yao ya madai kwa chama cha CUF kukiuka amri ya mahakama. Habari za ndani zinadai kwamba CUF wamepanga kumkataa JAJI AGUSTINO SHANGWA ambaye ndiye aliyetoa court injunction kwa CUF.
Najiuliza, Kama Ni kweli watamkataa JAJI huyo sasa JE, wasi wasi wote huo Ni wa nini, Kama wao wapo sahihi na maamuzi Yao waliotoa?
 
Kumkataa jaji hakutawasaidia kitu kwa sababu jaji yoyote atakae pangiwa kesi hiyo watashindwa tu kwasababu wamefanya makosa. hatuhitaji kuwa na degree kutambua kwamba walikaidi amri halali ya mahakama. Lakini huyu hamad rashid asingehangaika hivyo. Ningemshauri awaanike vizuri CUF halafu aachane na siasa.
 
CUF wamevunja katiba ya nchi, ni chama kinachopaswa kufutwa kwenye daftari la Msajili wa vyama vya siasa na si vinginevyo, kudharau amri ya Mahakama ni kosa kubwa sana kwenye nchi yeyote inayofuata utawala wa sheria.
 
Kumkataa jaji hakutawasaidia kitu kwa sababu jaji yoyote atakae pangiwa kesi hiyo watashindwa tu kwasababu wamefanya makosa. hatuhitaji kuwa na degree kutambua kwamba walikaidi amri halali ya mahakama. Lakini huyu hamad rashid asingehangaika hivyo. Ningemshauri awaanike vizuri CUF halafu aachane na siasa.
Kuwaanika then aachane na siasa haitokua sawa.......hapa Ni mapambano hadi kieleweke, tukipoteza viongozi makini Kama Hamad Rashid ndio inapelekea taifa kuzidi kudidimia.
 
CUF wamsulubu kichama yule muuaji (waziri wa usafirishaji zenji mwana cuf) na kuachana na huyu kilaza MROHO WA MADARAKA HR
 
CUF wamsulubu kichama yule muuaji (waziri wa usafirishaji zenji mwana cuf) na kuachana na huyu kilaza MROHO WA MADARAKA HR
Huyo sio mroho wa madaraka, alipofukuzwa ccm na maalim seif yeye alikuwa Waziri wa fedha lakini aliacha kazi kwa sababu ya msimamo. Hamad Rashid Ni kawaida yake kudai haki.
 
Wabara siku zote ni kuona Znz kuna malumbano na nchi haindelei. Maendeleo ya Znz kiuchumi yanawachoma sana wa Tanganyika.

Sasa Hamad is Out na nchi itaendelea. Walifukuzwa watu maarufu kuliko Hamad akina Naila Majid Jidawi, Mapalala, Frank Magoba , Rwekatare na wengine wengi lakin chama kinaendelea.

Kumbukeni chama sio genge la wahuni ni lazima mfuate sheria na kanuun walizojiwekea sio kwenda kinyume nazo kwani kufanya hivyo ni usaliti na adhabu yake ni kufukuzwa. Na ndilo lililompata Hamad Rashid
 
Wabara siku zote ni kuona Znz kuna malumbano na nchi haindelei. Maendeleo ya Znz kiuchumi yanawachoma sana wa Tanganyika. Sasa Hamad is Out na nchi itaendelea. Walifukuzwa watu maarufu kuliko Hamad akina Naila Majid Jidawi, Mapalala, Frank Magoba , Rwekatare na wengine wengi lakin chama kinaendelea. Kumbukeni chama sio genge la wahuni ni lazima mfuate sheria na sio kupinga kufuata sheria ni lazima ufukuzwe.
Maendeleo Ni kwa Mchele wa mapembe kuwa tsh.1800?!! Karafuu sasa hivi watu hawalipwi tena, wanakopwa! Je, haya Ni maendeleo? Nani alokudanganya kwamba lwakatare, Magoba walifukuzwa?! Na huo umaarufu wao wa kumzidi hamad uko wapi?!
 
Hivi kudharau amri ya mahakama ni kosa/shauri la madai au jinai?
 
Hivi kudharau amri ya mahakama ni kosa/shauri la madai au jinai?
Nafikiri hapo kuna utata kwenye katiba zote mbili. Ni vizuri ukajua kuwa Znz na Tanganyika zimeungana kimkataba na sio kikatiba.

Pili mfumo wa mahakama una taratibu zake. Kwa maana kuwa Tanganyika na Zanzibar zimeungana kwa mfumo wa mahakama zenu ni katika mahakama ya Rufaa na sio mahakama za chini ya hapo. Ndio maana Znz kuna Jaji mkuu na Tanganyika yupo pia.

Amri iliyotolewa ilitolewa na mahaka kuu ya Tanganyika ambayo mwisho wake ni Chumbe, ukiwa Znz ni invalid ni lazima ikasajiliwe na mahakama kuu ya Znz ili iweze kufanya kazi.

Kumbuka mkutano wa CUF ulifanyika Znz na sio Tanganyika. Hivyo pana utata mkubwa hapo. Tusihukumu ngoja tusikie wanasheria watakavyozipembua sheria ikiwemo pamoja na katiba zote mbili.

Uwe na subra sio kutupa lawama
 
Maendeleo Ni kwa Mchele wa mapembe kuwa tsh.1800?!! Karafuu sasa hivi watu hawalipwi tena, wanakopwa! Je, haya Ni maendeleo?
Nani alokudanganya kwamba lwakatare, Magoba walifukuzwa?! Na huo umaarufu wao wa kumzidi hamad uko wapi?!

Utazungumza mengi lakini najua imekukera sana Hamad Kufukuzwa. Lakin ndivyo ilivyyo hatakiwi tena CUF labda mumchukue tu huko Bara kama mnamuona bado ni dhahabu.

Nimekupa takwimu za kukuwa kwa uchumi wa Znz kuanzia 2000 mpaka sasa na kasi zake. Sasa kama unataka au una suala kutokana na hilo basi Bismillah lete nitakusaidia tu sio kuniambia bei ya kitu kimoja kimoja kupanda au kushuka.
 
Utazungumza mengi lakini najua imekukera sana Hamad Kufukuzwa. Lakin ndivyo ilivyyo hatakiwi tena CUF labda mumchukue tu huko Bara kama mnamuona bado ni dhahabu.

Nimekupa takwimu za kukuwa kwa uchumi wa Znz kuanzia 2000 mpaka sasa na kasi zake. Sasa kama unataka au una suala kutokana na hilo basi Bismillah lete nitakusaidia tu sio kuniambia bei ya kitu kimoja kimoja kupanda au kushuka.

Hapa tunazungumzia Utanzania, hakuna bara na visiwani, Umimi wako huo ndio tunachopinga hapa, Hamad kaona kuna umuhimu wa kulisimamia jambo hili na kuhakikisha Muungano watu Kama Watanzania unadumu. Hana fikra chovu Kama zako zenye kutizama Uzanzibar tu.
Suala la kumchukua hamad Kama unavyodai mmemchoka ilhali jana tu CUF imeumbuka baada ya kushindwa kufanya maandamano ya KUMPINGA baada ya kugomewa na wananchi (WAPEMBA) hasa wapiga kura wake inaonyesha wazi umetanguliza chuki zaidi mbele kuliko maslahi ya taifa kwa ujumla.
Tutamchukua Hamad na pia basi nanyie wapemba mhame huku bara, na investment zenu zoooote muondoe.
DHAMBI YA UBAGUZI ITAENDELEA KUWATAFUNA HADI MUISHE NINYI.
 
Hapa tunazungumzia Utanzania, hakuna bara na visiwani, Umimi wako huo ndio tunachopinga hapa, Hamad kaona kuna umuhimu wa kulisimamia jambo hili na kuhakikisha Muungano watu Kama Watanzania unadumu. Hana fikra chovu Kama zako zenye kutizama Uzanzibar tu.
Suala la kumchukua hamad Kama unavyodai mmemchoka ilhali jana tu CUF imeumbuka baada ya kushindwa kufanya maandamano ya KUMPINGA baada ya kugomewa na wananchi (WAPEMBA) hasa wapiga kura wake inaonyesha wazi umetanguliza chuki zaidi mbele kuliko maslahi ya taifa kwa ujumla.
Tutamchukua Hamad na pia basi nanyie wapemba mhame huku bara, na investment zenu zoooote muondoe.
DHAMBI YA UBAGUZI ITAENDELEA KUWATAFUNA HADI MUISHE NINYI
.

Hata ikikukera lakini ndio ukweli ulivyo. Hamad is OUT CUF. hakuna mjadala.

Kama anataka kuimarisha muungano basi angeanzia kule kwao wawi na sio habari maelezo dar.

Kumbuka nimekubaiishia toka awali kuwa Chama chochote cha siasa sio genge la wahuni. Ni mkusanyika wa watu wenye nia moja ya kuchukua madaraka ya kuongoza nchi kwa kupitia sera na kanuun walizojiwekea katika mitizamo yao, malengo na mwelekeo wao hususan kukuza uchumi na kuondoa umasikini.

Kila chama kina kaanun na sheria zake. Na kila kitu kimebainisha humo kuanzia unapoingia na kama kuna matatizo namna a kuyashughulikia mpaka kufikia suluhisho.

Kikubwa katika chama ni nidhamu ya kufuata kaanun na sheria za chama hicho na katiba yake. Kuvunja katiba kimakusudi au kutaka kubadilisha mwelekeo wa chama bila kufuata taratibu ni usaliti na adhabu yake muulize Hamad atakujuza.

Mkaribisheni tu hakuna shida kwani pasi na shaka kwenu bado ni dhahabu
 
Hapa tunazungumzia Utanzania, hakuna bara na visiwani, Umimi wako huo ndio tunachopinga hapa, Hamad kaona kuna umuhimu wa kulisimamia jambo hili na kuhakikisha Muungano watu Kama Watanzania unadumu. Hana fikr
a chovu Kama zako zenye kutizama Uzanzibar tu.
Suala la kumchukua hamad Kama unavyodai mmemchoka ilhali jana tu CUF imeumbuka baada ya kushindwa kufanya maandamano ya KUMPINGA baada ya kugomewa na wananchi (WAPEMBA) hasa wapiga kura wake inaonyesha wazi umetanguliza chuki zaidi mbele kuliko maslahi ya taifa kwa ujumla.
Tutamchukua Hamad na pia basi nanyie wapemba mhame huku bara, na investment zenu zoooote muondoe.
DHAMBI YA UBAGUZI ITAENDELEA KUWATAFUNA HADI MUISHE NINYI.
Inaonesha ww ni mchochezi na hufai katika jamii,wa kumtetea HR ni watu wa jimbo lake sio ww au umetumwa??Ww ndo umesema mapembe na karafuu,huko bara kuna karafuu na mapembe??unajibiwa unageuza kibao eti Muungano unajifanya Muungano unakuuma saaana huna lolote ww ni mamluki,mueneza chuki,wapemba waondoke huyo HR ni mnyamwezi.Go to the hell na chuki zako za kipumbavu.
 
Utazungumza mengi lakini najua imekukera sana Hamad Kufukuzwa. Lakin ndivyo ilivyyo hatakiwi tena CUF labda mumchukue tu huko Bara kama mnamuona bado ni dhahabu.

Nimekupa takwimu za kukuwa kwa uchumi wa Znz kuanzia 2000 mpaka sasa na kasi zake. Sasa kama unataka au una suala kutokana na hilo basi Bismillah lete nitakusaidia tu sio kuniambia bei ya kitu kimoja kimoja kupanda au kushuka.
Mkuu Baru, mi wala roho hainiumi kwa kufukuzwa huyu jamaa kwa sababu haiathiri upatikanaji wa ugali wangu. lakini inaonekana kuwa ni suala linaloihusu sana CUF na mashabiki wake. Kwa kuwa unaonekana kuwa ni sehemu ya maamuzi haya ya kufukuzwa kwa HR, nataka kujua kutoka kwako, iwapo mahakama ikisema kufukuzwa kwake si halali hivyo bado ni mwanachama, mtafanya nini? Natanguliza shukrani zangu kwa jibu lako
 
Inaonesha ww ni mchochezi na hufai katika jamii,wa kumtetea HR ni watu wa jimbo lake sio ww au umetumwa??Ww ndo umesema mapembe na karafuu,huko bara kuna karafuu na mapembe??unajibiwa unageuza kibao eti Muungano unajifanya Muungano unakuuma saaana huna lolote ww ni mamluki,mueneza chuki,wapemba waondoke huyo HR ni mnyamwezi.Go to the hell na chuki zako za kipumbavu.

Jina ulilotumia tu linaonyesha upeo wako unapoishia(kifa......?!)
Huyo HR sababu kubwa ya mimi kumsapoti Ni hukoo kuunga MKONO muungano......sera zake ziko wazi kuhusiana na suala zima la muungano. Na hii ndio sababu kubwa ya CUF kushuka sana hasa ktk uchaguzi wa 2010, kwani hawakuweka nguvu nyingi bara instead wakajikita zaidi zanzibar. Reason behind siitaji kurudia.
Problem yenu kubwa wa znz mna Umimi!! Narudia tena ile DHAMBI ya ubaguzi inawatafuna na ITAENDELEA KUWATAFUNA endapo hamtoacha Huu Ummi, ubinafsi na chuki kwa cc wa bara ilhali familia zenu ndugu jamaa wenu wengi tu wako huku bara.....wamewekeza na tunaishi Kama ndugu bila kubaguana.
Sikushangai sana kwani nakumbuka MHe: Masoud alishawahi kuzungumzia korosho and it was a very big mistake Kwake.......eti kwa nini anaongelea korosho anaacha karafuu na mbatata za urojo......that's stupid....U need to wake up guys and stop this non sense za Sisi na NINYI.......Mimi kuzungumzia mapembe kuna tofauti gani na MHE: Masoud kuzungumzia korosho?!!
Wake up guys!!!
 
Jina ulilotumia tu linaonyesha upeo wako unapoishia(kifa......?!)
Huyo HR sababu kubwa ya mimi kumsapoti Ni hukoo kuunga MKONO muungano......sera zake ziko wazi kuhusiana na suala zima la muungano. Na hii ndio sababu kubwa ya CUF kushuka sana hasa ktk uchaguzi wa 2010, kwani hawakuweka nguvu nyingi bara instead wakajikita zaidi zanzibar. Reason behind siitaji kurudia.
Problem yenu kubwa wa znz mna Umimi!! Narudia tena ile DHAMBI ya ubaguzi inawatafuna na ITAENDELEA KUWATAFUNA endapo hamtoacha Huu Ummi, ubinafsi na chuki kwa cc wa bara ilhali familia zenu ndugu jamaa wenu wengi tu wako huku bara.....wamewekeza na tunaishi Kama ndugu bila kubaguana.
Sikushangai sana kwani nakumbuka MHe: Masoud alishawahi kuzungumzia korosho and it was a very big mistake Kwake.......eti kwa nini anaongelea korosho anaacha karafuu na mbatata za urojo......that's stupid....U need to wake up guys and stop this non sense za Sisi na NINYI.......Mimi kuzungumzia mapembe kuna tofauti gani na MHE: Masoud kuzungumzia korosho?!!
Wake up guys!!!


Mbona usemi Dhambi ya UDINI inavyowatafuna huko Tanganyika.

Au ndio funika kombe mwanaharamu apite..

Nakupa pole.
 
Mkuu Baru, mi wala roho hainiumi kwa kufukuzwa huyu jamaa kwa sababu haiathiri upatikanaji wa ugali wangu. lakini inaonekana kuwa ni suala linaloihusu sana CUF na mashabiki wake. Kwa kuwa unaonekana kuwa ni sehemu ya maamuzi haya ya kufukuzwa kwa HR, nataka kujua kutoka kwako, iwapo mahakama ikisema kufukuzwa kwake si halali hivyo bado ni mwanachama, mtafanya nini? Natanguliza shukrani zangu kwa jibu lako

Si ajabu na si mara ya kwanza kutokea.

Naila jidawi aliyewahi kuwa kiongozi wa Upinzani Bungeni kupitia CUF alifukuzwa uanachama na Mahakama ikabatilisha na aliendelea kukaa bungeni kwa amri ya mahakama mpaka bunge lilipovunjwa.

Nafikiri maalim Seif aliliweka bayana kwenye mkutano wake wa hadhara huko manzese Dar. wapo tayari kwa lolote hata akiwa mbunge wa jimbo la mahakama.

Fuatilia speech yake ya manzese.

 
Wabara siku zote ni kuona Znz kuna malumbano na nchi haindelei. Maendeleo ya Znz kiuchumi yanawachoma sana wa Tanganyika.

Sasa Hamad is Out na nchi itaendelea. Walifukuzwa watu maarufu kuliko Hamad akina Naila Majid Jidawi, Mapalala, Frank Magoba , Rwekatare na wengine wengi lakin chama kinaendelea.

Kumbukeni chama sio genge la wahuni ni lazima mfuate sheria na kanuun walizojiwekea sio kwenda kinyume nazo kwani kufanya hivyo ni usaliti na adhabu yake ni kufukuzwa. Na ndilo lililompata Hamad Rashid

Maana ya kufuata sheria ni nini? ni pamoja na kukatazwa na mahakama kusikiliza shauri na kutii au kukaidi? tueleze.
 
Back
Top Bottom