hakika strategy za CCM ktk kuvuruga upinzani zinafanya kazi vizuri
hakika strategy za CCM ktk kuvuruga upinzani zinafanya kazi vizuri
Magazeti ya jana 12/12/2011 yaliripoti habari juu ya mvutano mkubwa uliotokea manzese kati ya walinzi wa ofisi kuu ya CUF wakishirikiana na walinzi wa wilaya ya kinondoni kupambana na mabaunsa waliokodiwa na hamad rashid mohammed. Makundi haya hasimu yalivutana katika tawi la KOSOVO ambako hamad rashid alifika na viti na meza kwa ajili ya kuwakabidhi uongozi wa kata katika harakati zake za kuchukua nafasi ya ukatibu mkuu hapo mwaka 2014 kwenye uchaguzi wa ndani ya chama wa CUF. Mivutano hiyo ya jana iliisha salama salimini baada ya walinzi wa ofisi kuu ya CUF na wale wa wilaya ya kinondoni kuamrisha kusitisha zoezi husika kwa sababu chama ngazi ya wilaya na taifa hawana taarifa ya ziara ya hamad rashid wakisisitiza juu ya kanuni za chama hicho ambazo husimamia kwamba kiongozi yoyote wa juu wa chama au mbunge au mwakilishi hawezi kutoka katika jimbo lake la uchaguzi na kwenda katika jimbo lisilo lake wala wilaya isiyo yake wala kata isiyo yake bila kuomba kibali kwa viongozi wa wilaya husika au taifa ambao ndio wana wajibu wa kusimamia ziara zote za viongozi. Baada ya hoja hizo nzito kutoka kwa walinzi hamad rashid alisitisha zoezi lake na kuondoka.
Shughuli pevu ilikuwa leo 13/12/2011 ambapo mbunge huyo wa wawi - Pemba alikuwa na ziara nyingine katika tawi la CHECHNIA lililoko kata ya mabibo. Baada ya walinzi wa taifa na wa wilaya kuzuia shughuli ya KOSOVO inaonekana hamad rashid na wenzie walijipanga zaidi na kukodi kundi kubwa la vijana wapatao 150 ili kulinda mkutano wake wa mabibo. Majira ya saa 8.00 mchana vijana kadhaa walianza kufika ukumbi wa mkutano wengine wakiwa na makoti na wengine wakiwa na kofia za mazoezi maarufu PAMA. Wengi wa vijana hao walionekana kuwa na nyuso nzito na baadhi yao walionekana kama wamepata kilaji kidogo.
Majira ya saa 9.00 walifika hapo ukumbini(ukumbi wa kukodi) wajumbe watatu wa baraza kuu la uongozi la CUF wakiambatana na baadhi ya wanachama wanaompinga MAALIM SEIF. Walipofika ukumbini wanachama na wananchi mbalimbali walianza kukusanyika. Wakati kusanyiko linaendelea ghafla gari ya ofisi kuu ya CUF ikapaki mita 100 hivi kutoka ukumbini. Baadaye walishuka walinzi wawili wa wilaya ya kinondoni na kwenda kwenye mlango wa ukumbi kuuliza kulikoni kikao hicho kifanyike bila wilaya kupewa taarifa?
Walipouliza walijibiwa na mjumbe wa baraza kuu la CUF ndugu DOYO kuwa kikao kile ni halali na ni cha katibu mkuu wa watu! Walipozidi kuhoji ndipo DOYO akakasirika na kuamrisha lile kundi la vijana 150 waliotapakaa nje ya ukumbi wahakikishe wanafanya kazi iliyowaleta. Kivumbi kikaanzia palepale, wale walinzi wa CUF walianza kukatwakatwa mapanga. Mmoja amjeruhiwa mara tatu kichwani na kuzimia, wa pili amekatwa mapanga mawili shingoni, mwingine amechomwa na chupa ya soda pajani. Wengine wawili wamjeruhiwa pajani na mgongoni.
Baada ya majeruhi hayo vijana hao walianza hatua ya kuchoma gari la chama hicho. Kilichookoa gari hiyo ni wananchama wa chama hicho waliotoka ukumbini kuja kutuliza walinzi wa kukodi wa HAMAD RASHID na wale wa CUF wilaya ya Kinondoni.
Baada ya tukio hilo, mwenyekiti wa CUF wa tawi la CHECHNIA ndugu MUHAJI aliwasili na akasisitiza kuwa hakuna kikao kufanyika lakini kundi lilelile lililokata wanachama na walinzi mapanga likamuonya kuwa akileta ujanja watamtoa roho kwani alishakula hela za wakubwa.
Baada ya onyo hilo, katibu wa tawi hilo ambaye anaunga mkono harakati za hamad rashid alisoma risala fupi kwa dakika mbili hivi na kueleza kuwa tawi hilo halina ofisi na kwamba wangeomba kusaidiwa shilingi 350,000 kwa ajili hiyo.
Palepale hamad rashid alitoa shilingi 250,000 na kuahidi kuwa zingine zingemaliziwa kesho yake. Baada ya kutoa fedha hizo aliendelea kutoa shutuma nyingi sana kwa viongozi wenzie. Alieleza namna gani ambavyo MAALIM SEIF ameshindwa kuisimamia CUF na kuwa chama hicho kimepoteza muelekeo na akasisitiza kuwa ili kukiokoa chama hicho lazima wanachama wamuami yeye HAMAD RASHID ili akiwa katibu mkuu CUF iamke tena tanzania bara.
Aliahidi pia kuwa akiwa katibu mkuu wa chama hicho matawi yote yatakuwa yanawezeshwa nchi nzima na kuwa atayatembelea mara kwa mara na kutatua shida zilizoko. Pia aliahidi kuwa atafungua vikundi vya kijasiriamali kila eneo ili wanachama wa chama hicho wanufaike kuliko ilivyo hivi sasa ambapo wanatumiwa kukijenga chama bila kuwa na malipo yoyote.
Aliendelea pia kuwajulisha wanachama hao kuwa chama hicho kimepoteza mwelekeo tazanzania bara kwa sababu amekabidhiwa unaibu katibu mkuu mtoto mdogo Julius Mtatiro(29) na kuwa bwana mdogo huyo ana dharau na ndiye anakiua chama kwa upande wa bara.
Alienda mbali zaidi na kueleza kuwa Lipumba amekosa mtu wa kumsaidia na kuwa yeye ndiye mwarobaini wa CUF kwa kuwa ana ujasiri, amewahi kukaa gerezani miaka mingi na kuwa yuko tayari kufa kwani alizaliwa siku moja na atakufa siku moja na aliwasihi wananchama wamuunge mkono ili apate ukatibu mkuu na kutibu matatizo ya CUF kwa kupambana na CCM kwani yeye peke yake ndiye aliyebakia na ujasiri huo baada ya chama chake kuolewa na CCM upande wa Zanzibar.
Ameahidi kuzunguka nchi nzima na kuwahamasiha wanachama waandamane hadi makao makuu ya CUF na kumshinikiza MAALIM SEIF aache ukatibu mkuu ili anakie na umakamu wa rais wake.
Nimebahatika kuingia katika kikao husika na ku-note vitu vingi sana, MASIKINI MTATIROOOO!
Hebu fikiria upya ulichokiandika. CCM haivurugi wapinzani ila inajivuruga yenyewe. Hawa CUF wanaandamwa na laana ya uroho wa madaraka. Ikumbukwe kuwa:
1. Ni uroho wa madaraka ndio umemfanya Seif Sharif Hamad kuingia ikulu ya SMZ na kuyaacha yale aliyoamini ndio sahihi hapo kabla.
2. Ni uroho wa madaraka ndio uliomfanya Hamad Rashid kuanzisha kambi yake ya upinzani bungeni akiigomea ile iliyo rasmi kwa mujibu wa katiba ili mradi tu alichukizwa kutopanda shangingi la Shadow PM.
3. Ni uroho wa madaraka tu ndio unawafanya CUF kutokuwa na utaratibu ulio wazi wa kuchagua uongozi wa juu wa chama chao
4. Ni uroho wa madaraka ndio unaofanya CUF wasiwe na mgombea urais tofauti na mnyamwezi
Kama haitoshi, CUF pia inaathiriwa na unafiki. Katika kikao cha mwisho cha bunge la kumi, maneno ya wabunge wengi wa CUF yalikuwa yakiwaambia wananchi kuwa CHADEMA ni chama cha fujo na dini. Tukio hili linakuwa jipya ktk historia za fujo za Tanzania (kwani nyingi huwa ni za kufikirika tu kufuatia intelijensia za polisi wetu) kwani CHADEMA ambao ndio wanaolalamikiwa kuwa wanaharibu amani ya nchi, hawajawahi kuonekana na fimbo wala jiwe kwenye maandamano yao achilia mbali mapanga ambayo CUF wameonesha uwezo mkubwa wa kuyatumia.
Kila mwenye ubongo wake na asome magazeti ya leo, atafakari dhana zilizotumiwa ktk fujo yao tukufu, atathmini majina ya viongozi wa CUF wanaoonekana kwenye hizo habari halafu ajipe majibu, kipi ni chama cha FUJO na DINI, CCM B au CDM?