Suley2019
JF-Expert Member
- Oct 7, 2019
- 1,817
- 4,566
Salaam Wakuu,
Katika maeneo mbalimbali ya huduma za kijamii kama vile stendi na hospitali ni kawaida mazingira hayo kuzungukwa na biashara mbalimbali za vyakula.
Maeneo mbalimbali ya jiji la Dar es Salaam hasa msimu huu wa mvua kumekuwa na uchafu uliokithiri maeneo ya vituo vya daladala.
Hali hii ya uchafu imeharibu mazingira mengi ya vituo vya barabara na kusababisha muonekano wa wafanyabiashara wa chakula kutia kinyaa na kuhatarisha afya za walaji wa vyakula hivi.
Hivyo, nalitumia jukwaa hili kuomba mamlaka na wahusika wakiwamo Mabwana na Bibi Afya kupita na kusimamia usafi katika maeneo yote ya uuzaji wa chakula nchi ili kulinda afya za Watanzania kwa kuepusha magonjwa ya kipindupindu na homa za matumbo.
Pia nawashauri wanunuaji wa chakula kutumia nafasi zao kusisitiza usafi wa mazingira katika maeneo wanayonunulia vyakula.
Picha: Sehemu ya chakula Mwenge Stendi
Picha: Sehemu ya chakula Kawe Stendi
Picha hizo juu nimezipiga leo Asubuhi (11/05/2023) maeneo ya Mwenge na Kawe.
Nawasilisha.
Katika maeneo mbalimbali ya huduma za kijamii kama vile stendi na hospitali ni kawaida mazingira hayo kuzungukwa na biashara mbalimbali za vyakula.
Maeneo mbalimbali ya jiji la Dar es Salaam hasa msimu huu wa mvua kumekuwa na uchafu uliokithiri maeneo ya vituo vya daladala.
Hali hii ya uchafu imeharibu mazingira mengi ya vituo vya barabara na kusababisha muonekano wa wafanyabiashara wa chakula kutia kinyaa na kuhatarisha afya za walaji wa vyakula hivi.
Hivyo, nalitumia jukwaa hili kuomba mamlaka na wahusika wakiwamo Mabwana na Bibi Afya kupita na kusimamia usafi katika maeneo yote ya uuzaji wa chakula nchi ili kulinda afya za Watanzania kwa kuepusha magonjwa ya kipindupindu na homa za matumbo.
Pia nawashauri wanunuaji wa chakula kutumia nafasi zao kusisitiza usafi wa mazingira katika maeneo wanayonunulia vyakula.
Picha: Sehemu ya chakula Mwenge Stendi
Picha: Sehemu ya chakula Kawe Stendi
Picha hizo juu nimezipiga leo Asubuhi (11/05/2023) maeneo ya Mwenge na Kawe.
Nawasilisha.