Mungi
JF Gold Member
- Sep 23, 2010
- 16,975
- 9,566
Polisi wanapiga mabomu ya machozi. Kuna gari limepigwa bomu mpaka limefumuka
===================================
UPDATES KUTOKA KWA MEMBERS WENGINE
===================================
===================================
UPDATES KUTOKA KWA MEMBERS WENGINE
===================================
Polisi wameanza kupiga mabomu wakati wabunge wa CHADEMA walipoanza kuhutubia maelfu kwa maelfu ya wafuasi wake. Hali ni mbaya sana hata watu wametelekeza magari na pikipiki zao, wabunge wote nao wamekimbia na mbaya zaidi wanapiga mabomu kila mahali.
Hali ni tete, mabomu yanarindima sana hali ni tete magari ya mevunjwa gari la Lissu laharibiwa, pikipiki zinavunjwa na polisi bila sababu. Hali tete, tegemeeni msiba mwingine
Wametumia risasi za moto kupiga watu, gari la Tundu Lissu limevunjwa vioo na jeshi la polisi. Wameumiza watu wengi sana! Hali ni mbaya sana!
Kufuatana na mgogoro wa serikali na wananchi wa Arusha, barabara inayounganisha kalolen na polisi central mpaka pale benki kuu arusha pamefungwa na inaonekana kuna pilikapilika nyingi central zinazoashiria hali si shwari Huku upande walipo wanaCHADEMA kukirindima mabomu...
Tahadhari wanaJF, msipite barabara hiyo kuanzia muda huu saa kumi na nusu ya tar 18 June 2013.
Kwa kweli hali ni ya hatari na wabunge kadhaa wa Chadema wameshikiliwa, polisi wanatumia nguvu kubwa kupita kiasi. Baadhi ya vyombo vya usafiri vilivyoachwa eneo la tukio polisi wanaviharibu kadiri wawezavyo. Usafiri wa abiria katika barabara ya Moshi-Arusha umesitishwa na hakuna gari zinazopita latika barabara hiyo. Majeruhi ni wengi na wamepelekwa hospitali.
Mabomu yalilipuliwa baada ya naibu mwenyekiti kuhitimisha kwa kuwaomba wananchi waliojikusanya eneo la Soweto waende ktk hospitali ya Mount Meru kwa ajili ya kwenda kuwaaga marehemu. Awali palitokea mabishano kati ya polisi na viongozi wa Chadema kuhusu mkusanyiko uliokuwapo hapo. Polisi walisema AICC wamekataa uwanja wao wa Soweto usitumike ktk shughuli yoyote. Bado vyombo vilivyoachwa uwanjani na wananchi vinaendelea kuharibiwa na polisi na baadhi ya wananchi wamejificha ktk fensi na baadhi ya nyumba zilizopo ktk uwanja huu.
WAKATI hali ikizidi kuwa mbaya jijini Arusha kufuatia mapambano ya raia na Jeshi la Polisi,Mbunge wa Arusha Mjini Godbless Lema amelazimika kukimbilia kwa wachoma nyama ya Nguruwe, (kiti moto).
Lema ambaye alinusurika kupigwa na bomu lilorushwa na Askari wa Jeshi la Polisi na kuharibu gari lake alikuwa akijaribu kuwatuliza wananchi walioanza kukusanyika katika vikundu, wakijadii amri ya Serikali ya kukataza miili ya watu waliofariki Dunia katika shambulio la kigaidi isiagwe katika viwanja hivyo.
Kabla ya Lema kupigwa mabomu na kukimbilia kwa wachoma nyama ya nguruwe hao alikuwa akisema, "jaribuni kuvumilia tunajaribu kuwasiliana Serikali ya Mkoa, ili watupe kibali ya kuleta miili ya wapendwa wetu hapa, kuweni wastaarabu kwa sababu mbele yetu kuna wanausalama ambao wanalinda amani,ingawa kufa ni kufa tu, wenzetu wamesha kufa na sisi ipo siku tutakufa, lakini kila anayetangulia lazima tumzike kwa heshma zote"alisema Lema kabla ya kupigwa bomu na Polisi.
Kauli hiyo ilizidi kiwachefua Polisi ambao walishatangaza amri ya watu kutawanyika katika viwanja hivyo, kwa ajili kuweka hali ya usalama wa eneo hilo ambapo walisema kwamba hakutakuwa na suala la kuaga maiili ya watu hao katika eneo hilo.
Niko SELIAN HOSPITAL majeruhi ni wengi sana. Kijana mmoja utumbo uko nje na wengine wana majeraha ya risasi wamevunjwa mikono wengine miguu! This is TANZANIA !