Hali mbaya kiwanda cha makaratasi 'mufindi paper mills'

laigwenan

JF-Expert Member
Apr 13, 2012
325
79
Kiwanda kikubwa kuliko vyote Afrika mashariki na kati na pengine cha pili Afrika kwa uzalishaji wa makaratasi 'MUFINDI PAPER MILLS' Kilichopo Mgololo wilaya ya Mufindi na mkoa wa Iringa Kimefungwa kwa muda usio julikana na vibarua 3100 kupewa likizo ya bila malipo huku wafanyakazi 503 wa kiwanda hicho kulipwa nusu mshahara.

Akiwa tangazia wafanya kazi wake Mkurugenzi mkuu wa kiwanda anaye fahamika kwa jina la MUHINDI amesema kiwanda kinakosa uwezo wa kuzalisha na kujiendesha kwa faida baada ya serekali kupandisha bei ya Magogo ambayo ndiyo malighafi kuu kwa kiwanda,alisema kabla ya kupandisha bei serekali ilipaswa kufanya Tafiti na kujiridhisha kabla ya kutoa uamuzi huu hivyo serekali ilikurupuka na kutumia ubabe katika maamuzi yake na wadau hawakushirikishwa na kwa kua soko la bidhaa zao lipo nje ya inchi kiwanda kinashindwa kushindana na viwanda vingine kwa kuwa wanalazimika kupandisha bei ya bidhaa zao huku wengine wakishusha bei! hivyo hakuna njia nyingine zaidi ya kukifunga kiwanda mpaka hapo watakapo fikia muafaka na serekali, na kuiomba serekali ipunguze ubabe!

Ikumbukwe kuwa Shamba la Miti la Sao hill lilianzishwa na JK Nyerere kwa minajili ya kuhudumia kiwanda hichi cha Makaratasi na pia kuzalisha Nguzo za umeme hapa inchini ambapo kiwanda cha Twico Mufindi kilipewa kazi ya kutengeneza Nguzo za umeme lakini Wizara ya Mali asili na utalii kupitia Shamba la miti la Sao hill lime acha kazi yake kuu na kujikita na shughuli za kugawa vibali kwa wachana mbao binafsi ambamo Inasadikika Rushwa ni sehemu ya Mtaji ya wafanya biashara hawa wa mbao.

Sasa kiwanda kimefungwa vibarua na wafanya kazi wanakosa mishahara sijui tunakwenda wapi na sera ya CCM ya maisha bora kwa kila Mtanzania.

My Take:eeeh! Mwenyezi Mungu ninaomba kura yangu iwe salama mwaka 2015.
 
Serikali iache ubabe? Rais wa zamani wa Marekani, Thomas Jafferson anatuambia hivi: "EXPERIENCE HAS SHOWN THAT EVEN UNDER THE BEST FORMS OF GOVERNMENT, THOSE ENTRUSTED WITH POWER HAVE, IN TIME, AND BY SLOW OPERATIONS, PERVERTED IT INTO TYRANNY".
 
Sio hicho kilichonunuliwa miaka michache na Kenya? Hata kile cha maziwa cha Arusha vile vile walinunua watu wa Mwai Kibaki katika mkakati wa kudhibiti viwanda vyote EAC, kinachotoka ni maziwa kuleta kwa magari makubwa toka kiwanda cha Kenya na kujazwa kwenye store za kiwanda chetu na kuuzwa tz, la Precision walivyoinunua na kuifanya Daladala ya kusomba international travellers wa Tz kwenda Hub Nairobi na kupanda KQ kwenda majuu, kisha nayo baada ya kuitoa damu wameitosa. Nilishuhudia mwenyewe propaganda Kenya kuwa usije ukapanda Precision kama hutaki kufa. Bora nje ya EAC tutapumua
 
What! Then you promise Tanzanians to have excellent education! Tell me colleagues, do we have other paper factories in Tanzania? Where are they located? My God! what about the employment of those people? education of their children and needs for their families?
 
Nakifahamu kiwanda hiki, kuna wakati nilikuwa mteja kwenda kununua karatasi pale na kupakia kwenye reli ya TAZARA hada Dar, kwa kweli ni kiwanda cha pekee na cha kujivunia kabisa hapa nchini Tanzania.

Mfano wake ni kama viwanda vingi vilivyoanzishwa katika mataifa makubwa kuibua kiwanda porini na kujenga makazi ya watu kuwa mji, leo nashika tama kusikia hali hiyo kwa vile sijagusa pale kwa muda mrefu kidogo sababu yakubadilisha mwelekeo wa shughuli niliyokuwa nafanya awali.

Uroho wa viongozi wetu ni pale wanapofikia kuua viwanda nchini kama ilivyotokea viwanda vya nguo, kuunganisha magari ya Scania Kibaha, viwanda vya kusindika nyama, viwanda vya korosho, makampuni ya usafirishaji mikoani nk. Hali hii tutafika wapi wakati tulishakuwa na kiwanda cha kujisifia na kutoka kifua mbele?
 
Mkuu kufungwa kwa kiwanda si hila mbaya ya selikari ila ni hao wahindi(rai group)wanawafanyisha kazi bila kuwalipa wafanyakazi mishahara mizuri.siku zote wahindi hupenda kuwachonganisha wafanyakazi na selikari ili wao wapate faida.vipi mkuu laki na nusu mlipata mwaka 2008?na mpetu bado ipo?
 
Me nikionaga hivi, roho inaniumaaa, naishia kusonya.

ila haya yote yana mwisho.

"when the night is getting darker, the morning light is near"
 
hivi hii nchi inataka iendeshwe kwa migomo? malori wagome, wanafunzi wagome, walimu wagome, madaktari nao ni........


imeonekana haitoshi wameamua kwenda sector ya viwandani.


kama ni kweli UBABE wa pinda unaf
anyiwa kazi watueleze rasmi. naamin wametuchoka sasa.
 
Mufindi Papers Limited inamilikiwa na kampuni ya Team Sale ya Kenya. Hawa jamaa wana viwanda vingi sana, wamenunua Mashamba ya iliyokuwa NAFCO ya Hanang, lakini uendeshaji wake naona unasuasua
 
Serikali iache ubabe? Rais wa zamani wa Marekani, Thomas Jafferson anatuambia hivi: "EXPERIENCE HAS SHOWN THAT EVEN UNDER THE BEST FORMS OF GOVERNMENT, THOSE ENTRUSTED WITH POWER HAVE, IN TIME, AND BY SLOW OPERATIONS, PERVERTED IT INTO TYRANNY".
ulisha sema zamani sasa ni mwendo wa sheria haki na usawa vinginevyo ni ubabe ngoja nikuambie kuna ulazima gani wa kupandisha bei ya Magogo wakati vibali hutolewa bure? huo ni ubabe na unamwisho hii inchi si ya CCm peke yake
 
Sio hicho kilichonunuliwa miaka michache na Kenya? Hata kile cha maziwa cha Arusha vile vile walinunua watu wa Mwai Kibaki katika mkakati wa kudhibiti viwanda vyote EAC, kinachotoka ni maziwa kuleta kwa magari makubwa toka kiwanda cha Kenya na kujazwa kwenye store za kiwanda chetu na kuuzwa tz, la Precision walivyoinunua na kuifanya Daladala ya kusomba international travellers wa Tz kwenda Hub Nairobi na kupanda KQ kwenda majuu, kisha nayo baada ya kuitoa damu wameitosa. Nilishuhudia mwenyewe propaganda Kenya kuwa usije ukapanda Precision kama hutaki kufa. Bora nje ya EAC tutapumua
Ninasikiaga tu kuwa Mmoja wa Marais wastaafu ninao waheshimu zaidi humu duniani Mzee wa uwazi na ukweli B.Mkapa ni mwanahisa na mwenzie Moi ila hoja yangu ni kiwanda kufungwa na watu zaidi ya 3500 kubaki omba omba. Ni hicho tu
 
Mutakyamirwa My God! what about the employment of those people? education of their children and needs for their families?[/QUOTE said:
This is What CCM Calls 'MAISHA BORA KWA KILA MTANZANIA'
 
nakifahamu kiwanda hiki, kuna wakati nilikuwa mteja kwenda kununua karatasi pale na kupakia kwenye reli ya tazara hada dar, kwa kweli ni kiwanda cha pekee na cha kujivunia kabisa hapa nchini tanzania.

Mfano wake ni kama viwanda vingi vilivyoanzishwa katika mataifa makubwa kuibua kiwanda porini na kujenga makazi ya watu kuwa mji, leo nashika tama kusikia hali hiyo kwa vile sijagusa pale kwa muda mrefu kidogo sababu yakubadilisha mwelekeo wa shughuli niliyokuwa nafanya awali.

Uroho wa viongozi wetu ni pale wanapofikia kuua viwanda nchini kama ilivyotokea viwanda vya nguo, kuunganisha magari ya scania kibaha, viwanda vya kusindika nyama, viwanda vya korosho, makampuni ya usafirishaji mikoani nk. Hali hii tutafika wapi wakati tulishakuwa na kiwanda cha kujisifia na kutoka kifua mbele?
mungu ailaze peponi roho ya jk nyerere amina
 
me nikionaga hivi, roho inaniumaaa, naishia kusonya.

Ila haya yote yana mwisho.

"when the night is getting darker, the morning light is near"
hakikisha kura yako hai haribiki ,haipotei wala kuibiwa wakati huo mwombe mungu akuwezeshe kupiga kura 2015
 
Biashara huwa ina siri na mambo mengi sana ndani yake.
Hapa anayepata shida kuliko mtu mwingine yeyote ni mwenye rasilimali hizi na haswa mzawa/mwananchi wa sehemu hii.
Mimi nikiangalia uwezo wa nje wa kampuni hii( layman's side)tulio hapa tukiona haya malori-brand new na ya kisasa ndio yanatumiwa.Dunia hii hamna option nyingine ya karatasi ambazo kama huna hali ya hewa kama hii,hata uwe tajiri kiasi gani huwezi kuipata hiyo miti na magogo.
Hawa wananchi wa sehemu hii,umasikini walionao ni aibu kusikia watu wanatajirikia kwenye migongo yao.Hapa si suala la chama gani au policy zipi,lakini kuna mtu aliwahi kusikia mfanyabiashara anaisifia TRA?ongeza bei ya kitu,anawafundisha ndg zako yeye ni nani.
Watu 3,000 wakikasirika kwa njaa waliyopewa-fikiria.Mpaka naona hii kama hadithi.Kama ni kweli serikali na wenye kiwanda kubalianeni kwanza kwa faida ya wananchi,maana hizo mnazotaka kuongeza nazo zinatakiwa kurudi kwa watu hawa hawa wenye njaa.:tape:
 
Back
Top Bottom