Ccm ni chama chenye laana hivyo kukichagua ni kuchagua laana miaka 53 nchi imeliwa imebaki mifupa, watanzania wanaishi kwenye umasikini uliopindukia pamoja na nchi kuwa na rasilimali nyingi ambazo zingetumika kunufaisha wananchi husika.
Huduma za kijamii ni mbovu
Elimu ambayo ingetumika kumkomboa mwananchi wameiua makusudi ili waendelee kututawala
Rushwa imekithiri masikini hana haki hata watoto wa masikini wameishia kuwa walimu maana kwingine hupati kazi bila rushwa na kujuana,
Kibaya zaidi deni la Taifa linapaa hivi hiyo mikopo inafanya kazi au mnakopa mje kulipana posho
NAKULILIA NCHI YANGU.
kama kuna laana kubwa watanzania itaendelea kuwasakama mpaka mwisho na hakuna matatizo yatakayowaisha hata aje kuhutubia papa benedicto ni laana ya kuichagua ccm madarakani.
Najua wapo wasioamini lakini ukweli halisi ni huo kwamba haya matatizo yote mnayoendelea kupiga kelele mara unyanyasaji,ufisadi,albino ni kutokana na laana za ya kuichagua ccm.
Kama kweli unataka kuondoa laana ya mkosi kwenye familia yako usichague kabisa ccm vinginevyo ndoa zenu zitaota mbawa bila kujua chanzo nini nini kumbe jibu unalo.
si rahisi kuingoa ccm kama watu kama wa chalinze watazidi kuwepo nchini
Escrow ni moja ya scandel inayopiganiwa kuzimwa na watawala kwa nguvu na akili zao zote.
-aisee inauma sana na inakera pia,chadema simama imara soon utakabidhiwa nchi hii iliyo megwa kila mahala:
Mara ooh! Huu ni mgodi wa ritz1,ooh!mara geta ni vichi kamato,ooh!buzwagi ni ya mkuu wa kaya!
-ndio maana vijana kina zitto wamejikatia tamaa na kuamua kuwa mafisadi tu.
-lakini sinto kata tamaa hadi siku ya ukombozi itimie.
Ni mimi.
vijana wengi wajiandikishe kwenye daftari la wapiga kura na wapate elimu ya ukomavu katika kulinda kura kama walivyo watu Arushakwahiyo tufanyeje mkuu ? Tunaomba ushauri wako .
nakubaliana na wewe kwa mengine. ila hilo la kusema wameua elimu ni uongo, elimu haijawahi kuwa hai tanzania tangia uhuru. kwa lugha ingine mzee mchonga hakuwekeza kwenye elimu hata kidogo.
Magamba ni kuachana nao 2015 tu kama tunahitaji maendeleo
vijana wengi wajiandikishe kwenye daftari la wapiga kura na wapate elimu ya ukomavu katika kulinda kura kama walivyo watu Arusha
vijana wengi wajiandikishe kwenye daftari la wapiga kura na wapate elimu ya ukomavu katika kulinda kura kama walivyo watu Arusha
kila mtu katika nchi hii ameichoka ccm , linasubiriwa daftari tu .
Mkuu hata mimi nimeichoka CCM.
mkuu ni aibu. kuna kitu hata watu hawakifikirii. mfano mzuri kujua kusoma na kuandika sio kwamba umefuta ujinga. kwa sababu hakukusaidii chochote. huna knowledge yoyote. hujui kilimo kinakuwaji wala biashara nk. is just unajua kuunganisha herufi. nadhani tunahitaji mtazamo mpana sana wa haya mambo.Mtu ukimuuliza umemaliza shule anasema ndiyo, Huku ni darasa la 7 tuu!