Hakuna laana kubwa kama kuichagua CCM

Pdidy

JF-Expert Member
Nov 22, 2007
50,893
21,979
Kama kuna laana kubwa watanzania itaendelea kuwasakama mpaka mwisho na hakuna matatizo yatakayowaisha hata aje kuhutubia papa Benedicto ni laana ya kuichagua CCM madarakani.

Najua wapo wasioamini lakini ukweli halisi ni huo kwamba haya matatizo yote mnayoendelea kupiga kelele mara unyanyasaji,ufisadi,albino ni kutokana na laana za ya kuichagua CCM.

Kama kweli unataka kuondoa laana ya mkosi kwenye familia yako usichague kabisa CCM vinginevyo ndoa zenu zitaota mbawa bila kujua chanzo nini nini kumbe jibu unalo.

 
Asante sweetbaby, Hakika umenikosha leo. Wambie wajue kuwa hiki ni chama uozo kabisa kheri ya chadema mara elfu. CCM ni mzoga kila pakiwa hapakosekani mafisi. Mwisho wakre ndio huu. watanzania amkeni kumekucha.
 
At least we are missing threads of this type, watu wanahangaika usiku na mchana mara EL, geuka huku CHENGE, kidogo RA, mara JK....Mkapa,,,, name it

Jumla ya yote hayo NI CCM WOTE ....waondoke thats all,

focus iwe kuijenga Tanzania mpya, kutayarisha vyama vizuri vyenye mawazo mapya ya kizalendo sio hivi tulivyo navyo sasa!

Tuwakomalie hawa wapinzani wabadilike wasijali matumbo yao wala kuanzisha NGO

CCM donda ndugu, haliponi jamani
 
Kama kuna laana kubwa watanzania itaendelea kuwaskama mpaka mwisho
na hakuna matatizo yatakayowaisha hata aje kuhutubia papa benedicto ni laana ya kuichagua ccm madarakani...yaah najua wapo wasioamini lakini ukweli halisi ni huo kwamba haya matatizo yote mnayoendelea kupiga kelele mara unyanyasaji...ufisadi....albino....ni kutokana na laanza ya kuichagua CCM....kama kweli unataka kuondoa laana ya mksoi kwenye familia yako usichague kabisa ccm....vinginevyo ndoza zenu zitaota mbawa bila kujua chanzo nini nini kumbe jibu unalo

IDD MUBARAK

Wishful thinking!
Wanaosema wengi lakini it is mere lip service.Na waliojitokeza wakipenyezewa rupia maneno ya utata kibao.
 
wapiga kura wanatuangusha sana, ila kwasababu wasio piga ni wengi kuliko wanaopiga, lazima tufanye mikakati mizito kuwawin hawa waliovumjika moyo kufikia kususa kupiga kura maana wengi wao ni waelewa, wanahitaji somo kidogo tu.
Mungu tutie nguvu tuweze kukabiliana na hawa CCM Wezi wa kura.
 
wapiga kura wanatuangusha sana, ila kwasababu wasio piga ni wengi kuliko wanaopiga, lazima tufanye mikakati mizito kuwawin hawa waliovumjika moyo kufikia kususa kupiga kura maana wengi wao ni waelewa, wanahitaji somo kidogo tu.
Mungu tutie nguvu tuweze kukabiliana na hawa CCM Wezi wa kura.
Nguvumali, wapiga kura ni wananchi wengi masikini wasiojua kusoma na kuandika , kwanza kwenye kupiga kura wanaletewa mtu wa kuwasaidia kuzipiga hizo kura na sahihi zao ni vidole gumba! what do u expext??hapa hapa Dar kwa mfano wananchi wengi wameridhika na maisha waliyonayo mtu akiwa na mia hamsini ya kula andazi linalouzwa barabarani tandika ameridhika!! unafikiri tutaiondoa ccm madarakani?? kwa kifupi wananchi wako stagnant hawajui kukasirika, in short tunaudhi kuliko maelezo!! angalia uchaguzi wa mitaa uliopita utakubaliana na mimi, mbali na kashfa zote ccm ilizokuwa nazo za ufisadi bado wameshinda kwa kishindo???! saa nyingine nakasirika kuwa mtanzania. yaani sisi wenyewe ni laana na ndiyo maana tutaipitisha ccm tena.
Binafsi naamini hakuna chama kilicho tayari kwa kushika dola hata hao chadema wenyewe ila kutoa fundisho kwa ccm ni muhimu, yaani kuwanyima kura ili wajirekebishe.
Lakini bado nasema watanzania wengi hawajui kusoma hivyo tusitegemee critical thinking ya mambo,wakija kudanganywa na miradi ya visima na barabara za kokoto wakati wa kukaribia uchaguzi wanasahau kwamba wana tanzanite arusha, urenium mbeya, gesi, makaa ya mawe, dhahabu, almasi...........ambavyo ni sababu tosha ya wao kutokuwa masikini kama viongozi wengesimamia vizuri.
Mungu ibariki Afrika, Mungu ibariki Tanzania.
 
wapiga kura wanatuangusha sana, ila kwasababu wasio piga ni wengi kuliko wanaopiga, lazima tufanye mikakati mizito kuwawin hawa waliovumjika moyo kufikia kususa kupiga kura maana wengi wao ni waelewa, wanahitaji somo kidogo tu.
Mungu tutie nguvu tuweze kukabiliana na hawa CCM Wezi wa kura.

Uko sahihi Nguvumali. Ushindi wa CCM unachangiwa pia na wasiopiga kura.

Toka nimetua hapa bongo, kama mwaka hivi sasa, ninajaribu sana kudodosa wabongo. Wengi wao wamechoshwa na CCM. Hawajasema kama upinzani hauko tayari, ila kwamba hata wakiwachagua upinzani, CCM wataiba hizo kura. Hiyo ndio sababu yao kuu. Mimi binafsi siiamini sana.

Watanzania chagueni upinzani badala ya CCM. Angalia signature yangu hapo chiini.
 
Watanzania vilaza watamchagua Kikwete aendeleze ubabaishaji ikulu kwa awamu nyingine - Tafakari
huo ni ujumbe maridhawa
 
Watanzania vilaza watamchagua Kikwete aendeleze ubabaishaji ikulu kwa awamu nyingine - Tafakari
huo ni ujumbe maridhawa
Ndugu vipi tena umekata tamaa au? na siasa za chadema

JK hana urais kama tume itakuwa huru..i can assure you...watanzania tuungane tulinde kura zisiibiwe kutakuwa na mabadiliko makubwa sana 2010

lakini makubwa zaidi 2015 the end of CCM.
 
Nguvumali, wapiga kura ni wananchi wengi masikini wasiojua kusoma na kuandika , kwanza kwenye kupiga kura wanaletewa mtu wa kuwasaidia kuzipiga hizo kura na sahihi zao ni vidole gumba! what do u expext??hapa hapa Dar kwa mfano wananchi wengi wameridhika na maisha waliyonayo mtu akiwa na mia hamsini ya kula andazi linalouzwa barabarani tandika ameridhika!! unafikiri tutaiondoa ccm madarakani?? kwa kifupi wananchi wako stagnant hawajui kukasirika, in short tunaudhi kuliko maelezo!! angalia uchaguzi wa mitaa uliopita utakubaliana na mimi, mbali na kashfa zote ccm ilizokuwa nazo za ufisadi bado wameshinda kwa kishindo???! saa nyingine nakasirika kuwa mtanzania. yaani sisi wenyewe ni laana na ndiyo maana tutaipitisha ccm tena.
Binafsi naamini hakuna chama kilicho tayari kwa kushika dola hata hao chadema wenyewe ila kutoa fundisho kwa ccm ni muhimu, yaani kuwanyima kura ili wajirekebishe.
Lakini bado nasema watanzania wengi hawajui kusoma hivyo tusitegemee critical thinking ya mambo,wakija kudanganywa na miradi ya visima na barabara za kokoto wakati wa kukaribia uchaguzi wanasahau kwamba wana tanzanite arusha, urenium mbeya, gesi, makaa ya mawe, dhahabu, almasi...........ambavyo ni sababu tosha ya wao kutokuwa masikini kama viongozi wengesimamia vizuri.
Mungu ibariki Afrika, Mungu ibariki Tanzania.
wapiga kura wanatuangusha sana, ila kwasababu wasio piga ni wengi kuliko wanaopiga, lazima tufanye mikakati mizito kuwawin hawa waliovumjika moyo kufikia kususa kupiga kura maana wengi wao ni waelewa, wanahitaji somo kidogo tu.
Mungu tutie nguvu tuweze kukabiliana na hawa CCM Wezi wa kura.





CCM haifai tena kupewa nafasi ya kushika dola tatizo wasomi wengi wanaganga njaa, heri wananchi wasiojua kusoma na kuandika maana siku wakijua watabadilika.

wasomi wanajua ubaya wa CCM lakini kusema ukweli kuhusu hilo ni mwiko. Zaidi tunaona wengi wanahangaika kujiunga na CCM ili mambo yao yanyoke.

Wananchi wengi kutokana na uelewa wao mdogo wamedaganyika sana na propaganda za CCM.

Mabadiliko yanakuja
 
Kila mtu anataka mabadiliko. Sio siri CCM kina wezi, ingawa ni wachache lakini ndio wenye influence kwenye chama, na ndio wenye nguvu, lakini swali linakuja nani aje badala ya CCM?

So fara upinzani wanaonekana kuwa bado hawajajipanga. Na inaonekana tayari mafisadi wameanza kutumia janja ya kuwatingisha na kuwanunua, tumeshaanza kusikia migogoro chadema, NCCR ndio imekufa, CUF bado ina nguvu zanzibar bara ni kama haina kitu.

Bado kuna asilimia kubwa ya watu wanaweza kuwapigia kura mafisadi kwa kuhongwa pilau, khanga, sukari au hata bia. Kuna wengine bado wakataa kuwapigia kura opposition kwa kuwa tu opposition ni opposition.
 
Nguvumali, wapiga kura ni wananchi wengi masikini wasiojua kusoma na kuandika , kwanza kwenye kupiga kura wanaletewa mtu wa kuwasaidia kuzipiga hizo kura na sahihi zao ni vidole gumba! what do u expext??hapa hapa Dar kwa mfano wananchi wengi wameridhika na maisha waliyonayo mtu akiwa na mia hamsini ya kula andazi linalouzwa barabarani tandika ameridhika!! unafikiri tutaiondoa ccm madarakani?? kwa kifupi wananchi wako stagnant hawajui kukasirika, in short tunaudhi kuliko maelezo!! angalia uchaguzi wa mitaa uliopita utakubaliana na mimi, mbali na kashfa zote ccm ilizokuwa nazo za ufisadi bado wameshinda kwa kishindo???! saa nyingine nakasirika kuwa mtanzania. yaani sisi wenyewe ni laana na ndiyo maana tutaipitisha ccm tena.
Binafsi naamini hakuna chama kilicho tayari kwa kushika dola hata hao chadema wenyewe ila kutoa fundisho kwa ccm ni muhimu, yaani kuwanyima kura ili wajirekebishe.
Lakini bado nasema watanzania wengi hawajui kusoma hivyo tusitegemee critical thinking ya mambo,wakija kudanganywa na miradi ya visima na barabara za kokoto wakati wa kukaribia uchaguzi wanasahau kwamba wana tanzanite arusha, urenium mbeya, gesi, makaa ya mawe, dhahabu, almasi...........ambavyo ni sababu tosha ya wao kutokuwa masikini kama viongozi wengesimamia vizuri.
Mungu ibariki Afrika, Mungu ibariki Tanzania.
Sisi tulio vijijini tunatarajia nyie mlio dsm mtuonyeshe njia maana magazeti mnasoma, na wengi ni wasomi; lakini nimeshangaa takwimu za waliojiandikisha na kupiga kura dsm katika uchaguzi wa serikali za mitaa. Hivi kweli mnatarajia mageuzi yaanzie vijijini? Mmetuangusha. Katika kata yangu tumepata wenyeviti wa vijiji 2 wa CUF na ccm mmoja, kata ya jirani tumepata vijiji 2 Chedema na ccm kimoja. Tungepata hivyo dsm tungekuwa tunazungumza mengine.
Mijini mmekata tamaa, mageuzi atayaongoza nani kutokea kijijini? Wakeup!
 
lakini swali linakuja nani aje badala ya CCM?
Hizi fikra ndiyo sikubaliani nazo. Hivi unadhani hakuna anayeweza kuongoza ila CCM tu? Hata wewe unaweza ali mradi dhamira yako iwe ni kuwatumikia wananchi. Nakuhakikishia ukiwa na dhamira safi utaona wananchi wanakuunga mkono na kila kitu kitaenda vizuri.
Unafikiri kwa nini watu wanakwepa kodi? Ni kwa sababu hawana uhakika kodi zao zinatumiwaje!
Kwa nini watu wanapiga kelele za ufisadi na kutowaamini viongozi wao? Ni kwa sababu viongozi wamewageuka wananchi na kuanza kuwatafuna!

Wewe ukijiepusha na mambo hayo, utaweza kutuongoza tu. Nchi hii ni tajiri sana, huhitaji miujiza kuwatoa wananchi katika umaskini!!!!
 
Kama kuna laana kubwa watanzania itaendelea kuwaskama mpaka mwisho
na hakuna matatizo yatakayowaisha hata aje kuhutubia papa benedicto ni laana ya kuichagua ccm madarakani...yaah najua wapo wasioamini lakini ukweli halisi ni huo kwamba haya matatizo yote mnayoendelea kupiga kelele mara unyanyasaji...ufisadi....albino....ni kutokana na laanza ya kuichagua CCM....kama kweli unataka kuondoa laana ya mksoi kwenye familia yako usichague kabisa ccm....vinginevyo ndoza zenu zitaota mbawa bila kujua chanzo nini nini kumbe jibu unalo

IDD MUBARAK

Wewe wakikusikia House negro wa kibogo utakiona
 
wapiga kura wanatuangusha sana, ila kwasababu wasio piga ni wengi kuliko wanaopiga, lazima tufanye mikakati mizito kuwawin hawa waliovumjika moyo kufikia kususa kupiga kura maana wengi wao ni waelewa, wanahitaji somo kidogo tu.
Mungu tutie nguvu tuweze kukabiliana na hawa CCM Wezi wa kura.

Nakubaliana na wewe 100 kwa 100. kazi kweli ipo wasiopiga kura wako wengi sana, kuna dada mmoja nilimpa lifti akaniambia kuwa hapigi kura tena kwani hana imani na system. Nilichofanya nilihakikisha kuwa nampa lifti kila siku halafu nikawa nampa somo, juzi kaniambia kuwa atapiga kura
 
Kukiwa na tume huru ni rahisi CCM kuondoka Zanzibar na Zanzibar kupata maendeleo lakini sio Bara! Ukitathmini matokeo ya chaguzi za serikali za mitaa, utatambua kuwa CCM inachukiwa JF tu sio na wananchi ambao imewafanya maskini wa kutupwa! Wabara mtaendelea kuumia mpaka mtakapotambua CCM ndio wanaofanya mahoheha wa kutupwa mpaka wakina mama wazazi wodini Temeke walale sakafu na wamlize Naomi Campbell!
 
Ccm ni chama chenye laana hivyo kukichagua ni kuchagua laana miaka 53 nchi imeliwa imebaki mifupa, watanzania wanaishi kwenye umasikini uliopindukia pamoja na nchi kuwa na rasilimali nyingi ambazo zingetumika kunufaisha wananchi husika.
Huduma za kijamii ni mbovu
Elimu ambayo ingetumika kumkomboa mwananchi wameiua makusudi ili waendelee kututawala
Rushwa imekithiri masikini hana haki hata watoto wa masikini wameishia kuwa walimu maana kwingine hupati kazi bila rushwa na kujuana,
Kibaya zaidi deni la Taifa linapaa hivi hiyo mikopo inafanya kazi au mnakopa mje kulipana posho
NAKULILIA NCHI YANGU.
 
Back
Top Bottom