Denis denny
JF-Expert Member
- Oct 7, 2012
- 5,780
- 7,835
Tehee katika fursa za kufanya umeiona hiyo ya vinyago..unapozungumzia kitu jaribu kuangalia na mazingira kwa kuwaelekeza vijana kuwa mazingira fulani ukifanya kitu fulani kitakutoa usiishie tu kusema kijana piga kazi kwa nadharia mana itakuwa ni blah blah kama stori za kwenye vitabuUkikaa na kuandika mtandaoni muda mrefu na maneno mengi unaingiza sh ngapi? Sisi vijana siku hizi tu wavivu sana, tunasingizia kila kitu, hatutaki kufanya kazi, hatutaki kulima, maofisini ni kuchati na rushwa kwa kwenda mbele.
Umeajiriwa juzi leo unataka umiliki gari nyumba nzuri, huku maofisini ni Facebook, whatsapp, badoo na Instagram.
Kila kukicha tunalalamika hakuna fulsa, hakuna ajira, huku wageni wakizidi kujinyakulia maeneo na rasilimali zetu.
Wageni wanachukua maeneo wanalima wanatajilika sie tunalalamikia serikali, vijana tuamke tufanye kazi, tuache uvivu.
Tutengeneze hata vinyago tuuze tumekalili ni kazi ya wamakonde, kulima wasukuma.
Kijana wa Tanzania amka fanya kazi kwa maendeleo ya kwako, familia yako, jamii yako na Tanzania yako