Hakimu ajitoa kesi ya Mahalu

Rutashubanyuma

JF-Expert Member
Sep 24, 2010
219,470
911,173
Hakimu ajitoa kesi ya Mahalu

Imeandikwa na Regina Kumba; Tarehe: 28th March 2011 @ 22:55 Imesomwa na watu: 47; Jumla ya maoni: 0








HAKIMU aliyekuwa akisikiliza kesi ya uhujumu uchumi ya kuisababishia Serikali hasara ya zaidi ya Sh bilioni mbili inayomkabili aliyekuwa Balozi wa Tanzania nchini Italia, Profesa Costa Mahalu na Meneja Utawala na Fedha, Grace Martin, amejitoa kusikiliza kesi hiyo.

Hakimu huyo, Sivangilwa Mwangesi ametangaza uamuzi wake huo baada ya kuombwa na washtakiwa kufanya hivyo, kwa madai kuwa wanaamini hawatapata haki mbele yake.

Kesi hiyo itatajwa tena mbele ya Hakimu Mfawidhi wa Mahakama hiyo Aprili 28, na kupangiwa hakimu mwingine kwa ajili ya kusikilizwa.

Katika uamuzi wake, Hakimu Mwangesi alisema washtakiwa walikuwa na haki ya kufanya hivyo lakini walitakiwa kutoa sababu za msingi zinazoelezea mwenendo wa hakimu katika kesi na sio uamuzi wake wa kisheria.

Alisema ameamua kujitoa kwa sababu anaheshimu maono ya washtakiwa ingawa sababu zote zilizotolewa na wakili wa washtakiwa, Mabere Marando kwa niaba ya wateja wake, hazikuwa na msingi wowote.

Mwangesi alisema anashangaa kwa nini mawakili wa washtakiwa hao hawakuwasilisha ombi hilo mapema, kwa sababu inaonekana ni muda mrefu wamekuwa na hofu hiyo.

Machi 25 mwaka huu kesi hiyo ilipokwenda mahakamani hapo kwa ajili ya utetezi, wakili wa
washtakiwa Wakili Marando aliwasilisha ombi la wateja wake kutaka Hakimu Mwangesi ajitoe.

Marando alidai kuna wakati upande wa mashitaka waliiomba Mahakama iruhusu shahidi wao atoe ushahidi kwa njia ya video akiwa nchini Italia na Mahakama ikiwa Dar es Salaam, upande wa utetezi ukapinga na hakimu huyo akakubali pingamizi hilo.

Alidai Bunge lilipitisha Muswada kuruhusu ushahidi kwa njia ya video kuchukuliwa na mshitakiwa Mahalu akiwa kama mwanasheria, aliona kuwa uamuzi wa Mwangesi ulikuwa wa
makusudi.

Sababu nyingine ya kuomba hakimu huyo ajitoe, ni madai ya upande wa mashitaka kuwasilisha mahakamani mkataba wa mauzo uliokuwa ni kivuli, ambao ulipingwa na upande wa utetezi lakini hakimu huyo akapokea nyaraka hiyo kama kielelezo.
 
KESI YA BALOZI MAHALU: Mkapa akunjua makucha


na Happiness Katabazi


amka2.gif
HATIMAYE utetezi wa Rais mstaafu Benjamin Mkapa katika kesi ya uhujumu uchumi inayomkabili aliyekuwa Balozi wa Tanzania nchini Italia, Profesa Costa Mahalu, umetua rasmi katika Mahakama ya Hakimu Mkazi, Kisutu jijini Dar es Salaam.
Mkapa ambaye ni shahidi wa pili wa kesi hiyo alitoa utetezi huo ambao unaweza kuandika historia mpya katika mwenendo wa kesi nchini, kupitia kiapo chake ambacho kimewasilishwa mahakamani na wakili wa mshtakiwa huyo, Mabere Marando.
Katika moja ya vipengele 13 vya kiapo hicho, pasipo kutaja jina, maelezo ya kiongozi huyo mstaafu yanamgusa Rais Jakaya Kikwete ambaye wakati Mkapa akiwa madarakani alikuwa ni Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa.
Hiyo inakuwa ni mara ya kwanza kwa rais mstaafu, kutoa utetezi mahakamani kwa kesi inayomgusa mmoja wa waliokuwa wateule wake wakati akiwa madarakani.
Kesi hiyo Namba 1/2007 ambayo Mahalu anashtakiwa pamoja na Grace Martin inasikilizwa na Hakimu Mkuu Mfawidhi wa Mahakama hiyo, Ilivin Mugeta.
Katika kesi hiyo, Mahalu na Martin wanatuhumiwa kwa wizi wa shilingi bilioni tatu katika ununuzi wa jengo la ubalozi mjini Rome.
Katika hati ya kiapo chake cha Machi 31 mwaka huu, ambayo imeandaliwa kwa mujibu wa Sheria ya Usajili wa Nyaraka (The Registration of Documents Act, Cap. 117 of 2002), Mkapa anaeleza kuwa kila kilichofanywa na Mahalu kilikuwa sahihi na kilikuwa na baraka ya serikali aliyokuwa akiingoza toka mwaka 1995-2005.
Ushahidi huo wa rais Mkapa ambao Tanzania Daima inayo nakala yake, umeorodhesha maelezo yake yaliyoainishwa katika vipengele 13.
Mkapa katika utetezi wake huo anadai kuwa mchakato mzima wa ununuzi wa jengo hilo la ubalozi lililoko katika mtaa wa Vialle Cortina d'Ampezzo 185 mjini Rome ulizingatia sera ya serikali ya upatikanaji au ujenzi wa majengo ya kudumu ya ofisi na makazi na kwamba ulizingatia maslahi ya taifa.
Hati hiyo ya kiapo ambayo tayari wakili Marando amesema ameishaiwasilisha pia Ofisi ya Mkurugenzi wa Mashtaka (DPP) Eliezer Feleshi, inaanza kwa kusema, "Mimi Benjamin Mkapa, mtu mzima, Mkristo, mkazi wa Dar es Salaam, ninaapa kama ifuatavyo, 'nilikuwa Rais mtendaji wa serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa vipindi viliwili mwaka 1995-2005 na nina uhakika wa yote haya nitakayosema ndani ya kiapo hiki.'
Katika kiapo hicho Mkapa anadai pia kuwa alifahamishwa na watendaji wa serikali aliyokuwa akiingoza jinsi mchakato uliofanyika na ripoti za uthamini wa serikali zilizotumika katika kufikia hatua ya kununua jengo hilo la ubalozi.
Anadai kuwa tathmini ya jengo hilo ambalo Mahalu anadaiwa kufanya udanganyifu na wizi kwa kulipa fedha kinyume na ilivyotajwa katika mkataba ambayo ilifanywa na serikali ya awamu ya tatu kupitia wizara mbili tofauti, Wizara ya Ujenzi na Wizara ya Ardhi na Maendeleo Mijini.
Anaendelea kudai kuwa, anatambua kuwa ripoti ya serikali ya uthamini wa jengo hilo iliandaliwa na Wizara ya Ujenzi kwa kiwango cha dola za Marekani milioni tatu na Wizara ya Ardhi kwa thamani ya euro milioni 5.5.
Kwa mujibu wa ripoti hiyo kupitia mchakato wa ununuzi wa jengo hilo ulikuwa wa aina mbili, mmoja ni rasmi na mwingine wa kibiashara na kuongeza kuwa kwa mujibu wa taratibu ya serikali ya Italia na kuwa hilo lilifanyika kwa baraka za serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.
"Utaratibu kama huo wa mikataba miwili ushawahi kufanywa na serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania pale ambapo ilionekana haja kwa kuzingatia maslahi ya taifa kwanza....na kuwa ni mimi ndiye niliyezindua jengo hilo la ubalozi Februari 23 mwaka 2003," anadai Mkapa.
Shahidi huyo wa Mahalu anadai pia kuwa kwa mujibu wa kiapo chake anakumbuka vyema taarifa ya serikali iliyotolewa bungeni Agosti 3 mwaka 2004 iliyosema na kuthibitisha kuwa taratibu zote zinazohusiana na manunuzi ya jengo kwa mujibu wa maelekezo ya serikali, zilifuatwa na kwamba muuzaji wa jengo hiilo alilipwa fedha zote.
Kumbukumbu ambazo gazeti hili linazo zinaonyesha kwamba, Agosti 3, 2004, Kikwete alitoa maelezo bungeni kuhusu utata uliokuwapo awali kuhusu ununuzi wa jengo hilo la ubalozi.
Kikwete katika maelezo yake hayo ambayo yako pia katika kumbukumbu rasmi za Bunge (Hansard) anaeleza, "Mheshimiwa Naibu Spika mwaka 2001/02 wizara ilinunua jengo la ubalozi counsel katika ubalozi wa Rome katika jitihada za kuondokana na tatizo la kupanga majumba ya watu huko nje na pia kupunguza gharama za kuendelea kulipa pango la nyumba kila mwaka.
"Ununuzi wa jengo hili ulifuata taratibu zote za manunuzi ya majengo ya serikali kwa kuzishirikisha wizara za ujenzi, ardhi na maendeleo ya makazi pamoja na Wizara ya Fedha.
"...Jengo lilifanyiwa tathmini na wataalamu wetu na kukubaliana na ununuzi wa Euro 3,098,781.40 tarehe 6 Machi 2002 fedha za awamu ya kwanza katika ubalozi wa Rome zilipelekwa nazo zilikuwa shilingi 700,000,000 tarehe 28 Juni 2002 zilipelekwa shilingi 120, 000,000.
"Mwishoni mwa tarehe 26 Agosti mwaka 2002 zilipelekwa shilingi 1,000,000,000 jumla ya fedha zilizokuwa zimepelekwa zikafikia shilingi 2,900,000,000 na baada ya hapo ubalozi wetu ulitekeleza taratibu zote za ununuzi wa jengo na kumlipa mwenye nyuma kiasi hicho cha fedha," alieleza Kikwete.
Akimwelezea Mahalu katika utetezi wake, Mkapa alidai katika kipindi chote alichokuwa rais wa nchi alifanya kazi na mshtakiwa huyo katika nyadhifa mbalimbali za utumishi wa umma na kwamba mshtakiwa huyo ni mtu wa tabia njema, mkweli, mwaminifu na mchapaji kazi.
Mkapa anahitimisha utetezi wake kwa kueleza kuwa, kutokana na mwenendo huo wa kutukuka, Rais wa Italia alimpatia moja ya tuzo za heshima yenye hadhi ya juu kabisa ya taifa hilo Profesa Mahalu, muda mrefu baada ya balozi huyo kuwa ameshaondoka nchini humo.
Akizungumza na waandishi wa habari baada ya kuwasilisha mahakamani ushahidi huo wa Mkapa jana, wakili Marando alisema mteja wake anakusudia kupeleka jumla ya mashahidi 10.
Mashahidi hao ni mteja wake (Mahalu), Mkapa, Rais Jakaya Kikwete, kwani wakati akinunua jengo hilo ndiye alikuwa Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa ambaye ndiye alimpa mteja wake nguvu ya kisheria ya kuendelea na ununuzi wa jengo hilo, aliyekuwa waziri wa Ujenzi wa John Magufuli na mashahidi wengine na aliyekuwa Waziri wa Fedha, Basil Mramba ambaye pia anakabiliwa na kesi ya matumizi mabaya ya ofisi ya umma na kuisababishia serikali hasara ya sh bil. 11.7.
Kuwasilishwa kwa hati ya kiapo cha Mkapa mahakamani hapo, kumekuja baada ya Hakimu Mkuu Mfawidhi Ilvin Mugeta kusema kuwa yeye ndiye amejipangia kusikiliza utetezi wa washtakiwa hao Aprili 28 mwaka huu.
Hatua ya Hakimu Mugeta kusikiliza utetezi huo inakuja baada ya Machi 28 mwaka huu, Jaji Sivangilwa Mwangesi ambaye ndiye aliyekuwa akisikiliza kesi hiyo tangu awali kujitoa baada ya mawakili wa washtakiwa kuwasilisha sababu sita za kumwomba ajitoe kwa sababu kukosa imani naye Machi 25 mwaka huu.
Mapema mwaka 2007, Jamhuri kupitia mawakili wake toka Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (TAKUKURU), Ben Lincoln na Ponsian Lukosi iliwafikisha mahakamani hapo kwa mara ya kwanza washtakiwa hao kwa makosa ya uhujumu uchumi, wizi wa zaidi ya euro milioni mbili wakati wakisimamia ununuzi wa jengo la ubalozi mjini Rome nchini Italia.



h.sep3.gif


juu
blank.gif

blank.gif
blank.gif
Habari Mpya | Matangazo | Bei zetu | Wasiliana nasi | Tuma habari | Webmaster
Copyright 2011 © FreeMedia Ltd.
Wasomaji
counter
hit counter


© free media limited 2011
mtaa wa Mkwepu na Makunganya, jengo la Bilicanas, gorofa ya kwanza, SLP 15261, Dar es salaam, Tanzania
simu +255-22-2126233
 
Marando: Tunamtaka Rais mahakamani Send to a friend Monday, 30 May 2011 21:30

PROFESA MAHALU KUANZA UTETEZI LEO
James Magai na Tausi Ally

WAKILI Mabere Marando anayemtetea Profesa Costa Mahalu aliyekuwa na Balozi wa Tanzania nchini Italia, amesema ataiomba mahakama imlazimishe Rais Jakaya Kikwete kufika mahakamani kumtetea mteja mteja wake iwapo hatakubali kwenda kutoa ushahidi baada ya kuombwa kufanya hivyo kwa barua.Marando ametoa kauli hiyo wakati Profesa Mahalu na mwenzake Grace Martin wakianza kujitetea leo.

Mbali na utetezi wao binafsi, wanatarajia pia kuwa na mashahidi kadhaa wa kuwatetea akiwamo Rais Mstaafu wa Awamu ya Tatu, Benjamin Mkapa pamoja na Rais Kikwete.Tayari Rais Mkapa amewasilisha mahakamani hapo hati yake ya kiapo akimtetea Profesa Mahalu na mwenzake kuhusiana na tuhuma zinazowakabili huku akibainisha kuwa yuko tayari kufika mahakamani iwapo italazimu.

Lakini hadi jana, Rais Kikwete alikuwa hajajibu barua aliyoandikiwa na Wakili Marando kwa niaba ya wateja wake wakimwomba akubali wa kufika mahakamani kuwatetea au kuwasilisha kiapo chake ambacho kitatumika kama ushahidi wa utetezi dhidi yao.

Marando alisema jana kuwa Rais Kikwete alikuwa hajajibu barua hiyo, lakini akasema ikiwa Profesa Mahalu atamaliza kujitetea pamoja na mashahidi wengine kabla Rais Kikwete hajakubali, wataiomba mahakama imkumbushe.

"Kama atakaidi hata baada ya mahakama kumwandikia, basi tutaomba kesi hiyo iahirishwe hadi mwaka 2016 (wakati atakapokuwa amemaliza muda wake wa urais) ili imlazimishe kuja kutoa ushahidi huo," alisema Marando.

Mei 3, mwaka huu Wakili Marando alimwandikia barua Rais Kikwete yenye kumbukumbu namba MM/PCRM/2011/1 kupitia kwa Katibu Mkuu Kiongozi, Philemon Luhanjo, akibainisha kuwa ni miongoni mwa mashahidi muhimu ambao wateja wao wamewaagiza wamwite.

Barua hiyo inabainisha kuwa umuhimu wa Rais Kikwete katika ushahidi huo wa utetezi unatokana na ukweli kwamba nyumba hiyo ya Ubalozi wa Italia ilinunuliwa wakati akiwa Waziri wa Mambo ya Nje na kwamba alikuwa na taarifa zote kuhusu mchakato wa ununuzi wake.

Mchakato huo, kwa mujibu wa barua hiyo ni pamoja na nguvu ya kisheria aliyopewa mteja wao ambayo ilisainiwa na Rais Kikwete wakati huo akiwa Waziri Septemba 24, 2004 pamoja na hotuba yake aliyoitoa Bungeni Agosti 3, 2004 akithibitisha kuwa ununuzi wa jengo hilo haukuwa na mushkeli wowote.

Pia barua hiyo inaweka wazi kuwa kuna barua nyingi tu ambazo Profesa Mahalu alimwandikia Kikwete akiwa waziri, pamoja na katibu mkuu wa wizara hiyo, ambazo anapaswa kuzitambua mahakamani wakati wa utetezi.

"Kwa hiyo tunaomba kwa unyenyekevu kabisa, uweke barua yetu hii mbele ya Mh. Rais wa Jamhuri ya Muungano Tanzania; aisome na akueleze utujibu kama hana pingamizi kuja kueleza ukweli mahakamani. Kama muda wake hauruhusu, kulingana na ratiba zake za kitaifa, tunaomba aturuhusu tumwandalie kiapo (affidavit) kitakachoeleza yaliyotekea ili tukiwasilishe mahakamani badala ya kumwita yeye mahakamani", inasisitiza barua hiyo na kuongeza kuwa hakuna kifungu cha Katiba kinachozuia Rais kuitwa kutoa ushahidi mahakamani.

Katika kiapo chake alichokiwasilisha mahakamani, Mkapa anamtetea Mahalu na akidai kuwa amefanya naye kazi kwa muda mrefu na anamjua kuwa ni mtu mwaminifu, mtiifu na mchakapakazi. Mkapa alieleza katika hati yake hiyo kuwa mchakato wa ununuzi wa jengo hilo ulifanyika wakati wa uongozi wake na kwamba alikuwa akijua kila kilichokuwa kikiendelea kuhusiana na ununuzi huo na kwamba ulifanyika kwa mujibu wa sheria.

Alifafanua kuwa mpango wa ununuzi wa jengo hilo ulikuwa ni utekelezaji wa sera ya serikali wa kuwa na majengo yake ya kudumu katika kila ubalozi kwa kununua au kujenga ikiwa ni njia ya kupunguza gharama za upangaji. Aliongeza kuwa serikali yake ilimpa Profesa Mahalu mamlaka yote kupitia nguvu ya kisheria ya kusimamia na kutekeleza mchakato wa ununuzi wa jengo.

Mkapa alisisitiza kuwa kupitia utaratibu wa serikali, alikuwa akijua kuwa taarifa ya uthamini wa jengo hilo iliyofanywa na Wizara ya Ujenzi ilikuwa ni Dola za Marekani 3.0 milioni wakati Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, ilikadiriwa Euro 5.5 milioni: "Kupitia utaratibu wa serikali nilifahamu kuwa jengo hilo lilinunuliwa kwa gharama ya Dola za Marekani 3.0milioni sawa na Euro 3,098,741.40," alisema Mkapa.

Pia Mkapa alisisitiza kuwa alikuwa na bado anatambua taarifa ya serikali bungeni ya Agosti 3, 2004 iliyoeleza na kuthibitisha kuwa taratibu zote za ununuzi wa jengo hilo zilifuatwa kwa mujibu wa maelekezo ya serikali na kwamba dalali alilipwa kikamilifu.

"Kwa kipindi chote ambacho nimefanya kazi na Balozi Mahalu katika nafasi mbalimbali za utumishi wa serikali ameonyesha tabia thabiti na za dhati, uaminifu, utiifu, uchapakazi na ubora," alisema Mkapa.

Alisema kuwa sifa hizo zilimfanya atunukiwe na Rais wa Italia, Tuzo ya Heshima ya Juu wakati wa kuadhimisha Siku ya Taifa hilo, muda mrefu baada ya kuwa ameondoka nchini humo.

Profesa Mahalu na mwenzake, Martin aliyekuwa Ofisa Utawala wa ubalozi huo wanakabiliwa na mashtaka hayo katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu, Dar es Salaam wakidaiwa kuhujumu uchumi kwa kuisababishia Serikali hasara ya Euro 2,065,827.60. Wanadaiwa kusababisha hasara hiyo kupitia mchakato wa ununuzi wa jengo la ubalozi huo, wakati wa utumishi wao.

Kutokana na mashtaka hayo, leo wanadiplomasia hao wanaanza kujitetea baada ya mahakama hiyo kuwaona kuwa wana kesi ya kujibu.Mahalu na Martin wanadaiwa kula njama na kutenda makosa hayo katika tarehe tofauti na katika maeneo tofauti huko Italia, likiwamo la kumpotosha mwajiri wao katika hati ya matumizi.

Miongoni mwa mashtaka hayo ni kwamba Septemba 23, 2002 huko Rome, washtakiwa wakiwa waajiriwa wa Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, walisaini vocha yenye namba D2/9/23/9/02 ikionyesha kuwa bei ya ununuzi wa jengo la ubalozi ni Euro 3,098,741.58, maelezo ambayo yalikuwa ni ya uongo na yenye nia ya kumdanganya mwajiri wao.
 
Kesi hii ya Mahalu is nothing but corruption. Kesi inaendelea on and on. At the end of the Court day,tunaona watuhumiwa wanatabasamu,advocates wanatabasamu,kila mtu anatabasamu. Obviously some in the legal proffession are working in collusion with criminals to steal from the country. Nadhani tatizo lipo katika Jeshi,yaani JWTZ,wanajeshi hawahusiki,wako neutral,sasa inakuwa very difficult to deal with the few corrupt judges who are troubling us. I am not talking about a coup detat to solve this problem,tatizo la corruption Tanzania siyo kubwa sana. Lakini kama mafisadi wanaandamwa,wameiba hela za wananchi,they must have no place to turn to,absolutely no place to turn to,they must just go down.
 
Mahalu awataja Mkapa, JK mahakamani Kisutu Send to a friend
Friday, 05 August 2011 08:53
0digg

Nora Damian
ALIYEKUWA Balozi wa Tanzania nchini Italia, Profesa Costa Mahalu ameieleza Mahakama kuwa alimtaarifu Rais Mstaafu, Benjamin Mkapa kuhusu hali ya ofisi ya ubalozi ilivyokuwa mbaya.

Mahalu na aliyekuwa Ofisa Utawala wa ubalozi huo, Grace Martin, wanakabiliwa na kesi ya kuhujumu uchumi na kuisababishia Serikali, hasara ya zaidi ya Sh2bilioni wakati wa ununuzi wa jengo la ofisi za ubalozi wa Tanzania mjini Rome, Italia.

Jana katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu, Mahalu alitumia zaidi ya saa tatu kujitetea huku baadhi ya utetezi wake ukitawaliwa na kukataliwa kwa baadhi ya nyaraka alizoziwalisha kama ushahidi.

Akiongozwa na wakili wake, Mabere Marando, Mahalu alidai kuwa mwaka 2001 wakati Mkapa alipokwenda Brussels nchini Ubelgiji, alionana naye na kumtaarifu kuhusu hali ya ofisi za ubalozi huo kuwa mbaya.

"Mwezi Mei mwaka 2001, nilitaarifiwa kuwa Mkapa atakwenda Ubelgiji na mimi nilimwomba Katibu Mkuu wangu, Balozi Kibelo aniruhusu nikamweleze juu ya matatizo yaliyokuwa kwenye ofisi yetu,"alidai Mahalu na kuongeza:

"Nilionana na Rais Mkapa na aliniambia anafahamu suala hilo kwa kuwa ofisi za ubalozi huo, zilikuwa zimefungwa kwa muda mrefu hivyo aliniambia atajitahidi kupata fedha za kujenga ama kununua jengo lenye hadhi za ofisi za ubalozi."

Mkapa ni mmoja wa mashahidi wa upande wa utetezi ambaye tayari aliwasilisha utetezi wake wa maandishi ulioandaliwa kwa njia ya kiapo kumtetea Profesa Mahalu.
Kwa mujibu wa kiapo chake kilichowasilishwa mahakamani hapo, Mkapa anadai kuwa jengo la ofisi ya ubalozi mjini Rome, lilinunuliwa wakati ambao yeye akiwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.

Alidai kwamba ununuzi wa jengo hilo ulifanyika kwa mujibu wa sera ya Serikali ya kumiliki au kujenga ofisi za kudumu na makazi kwa mabalozi nje ya Tanzania ikiwa ni njia mojawapo ya kupunguza gharama kwa Serikali.

Maelezo zaidi ya Mahalu
Mahalu alidai kuwa baada ya kuonana na Mkapa, alimjulisha Balozi Kibelo juu ya mazungumzo yao na kwamba alimuahidi kuwa atalifuatilia na kulipeleka katika bajeti ya wizara husika.
Alidai kuwa masuala yote ya fedha yalikuwa yakiletwa kwake, lakini alikuwa hayashughulikii moja kwa moja kwa sababu chini yake kulikuwa na mhasibu.

Aliendelea kudai kuwa Desemba 2001, Rais Jakaya Kikwete wakati huo akiwa Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, alikwenda nchini Italia na kwamba aliiona hali ya ofisi za ubalozi huo zilivyokuwa.

"Rais Kikwete alikuja na aliona ofisi zilivyokuwa kwani japo alikuwa mfupi kuliko mimi, alishindwa kukaa kwenye meza iliyokuwa pale ofisini,"alidai Mahalu na kuongeza kuwa: "Aliahidi kwamba tutapata ofisi nyingine itakayokuwa na hadhi na mwonekano mzuri".

Balozi Mahalu alidai kuwa mwaka huo huo, Rais wa Zanzibar, Dk Ally Mohamed Shein ambaye wakati huo alikuwa Makamu wa Rais naye alikwenda nchini Italia na aliona ofisi za ubalozi huo zilivyokuwa.

"Dk Shein alisikitishwa sana na hali ile na aliahidi kwamba akirudi nyumbani, ataongea na viongozi kuhakikisha tunapata jengo kubwa lenye hadhi ya kibalozi,"alidai.
Alidai kuwa Juni, 2001 alipigiwa simu na Katibu Mkuu wake na kujulishwa kuwa maombi ya wizara ya kutengewa fedha za ununuzi wa jengo jijini Rome yatakubalika bungeni kwa kuwa wizarani yalikuwa yameshapitishwa.

"Niliagizwa kwamba nijipange na maafisa wangu kwa kuangalia majengo yanayofaa yenye hadhi ya kuwa ofisi za ubalozi, nami nilifanya hivyo,"alidai.
Alidai kuwa namna ofisi za ubalozi huo zilivyokuwa, alikuwa hawezi hata kuwaalika mabalozi wengine ama hata kuandaa mkutano.

Alidai kuwa ubalozi huo ulikuwa umefungwa tangu mwaka 1994 na kwamba vifaa vyote vya masuala ya ubalozi likiwemo jengo, vilirudishwa kwa mwenyewe.

Alidai kuwa ilibaki ofisi ndogo ya kilimo iliyokuwa katika jengo dogo.
"Nilianzia kazi kwenye ofisi ndogo iliyokuwa na square metre (mita za mraba) kati ya 88 na 100,"alidai.

Profesa Mahalu alidai katika ofisi hiyo kulikuwa na meza ya miguu mitatu, kiti cha balozi ambacho hata hivyo, kilikuwa kibovu, kochi lililokuwa limevunjika na simu.

Alidai kuwa maafisa wake wengine walikuwa wanakaa kwenye vyumba vya kulala na kwamba jiko lilikuwa linatumika kama sehemu ya mapokezi ambayo katibu muhtasi na dereva wake walikaa hapo."Choo kilikuwa kimoja tu na kilikuwa kibovu wakati mwingine kikiharibika tulikuwa tunashindwa kukaa,"alidai.

Alidai kuwa baada ya kuona hali hiyo aliamua kununua samani za ofisi kwa fedha zake mwenyewe, lakini hata hivyo hazikuingia zote kutokana na udogo wa ofisi hiyo.

Vielelezo

Mahalu pia alionyesha mahakamani hapo vielelezo viwili vya barua moja, ikiwemo ile ya shukrani aliyoandikiwa na Katibu Mkuu wa Wizara ya Sayansi, Teknolojia na Elimu ya Juu wa wakati huo marehemu Abdallah Ngororo ambayo Mahakama iliikataa kwa kuwa ni nakala.

Wakili wa Serikali Ponsiano Lukosi alipinga kupokelewa kwa barua hiyo kwa madai kuwa hawana uthibitisho kama imetolewa wizarani kwa sababu ni nakala ya barua.

Katika uamuzi wake Hakimu Mfawidhi wa Mahakama hiyo Ilvin Mgeta, alisema kuna haja ya kuthibitisha kielelezo hicho kama barua halisi ilipotea au uletwe ushahidi wa kuthibitisha kwamba ilitolewa na ofisi ya umma.

Kielelezo kingine alichowasilisha Mahalu ni barua yake aliyomwandikia Balozi Kibelo ya Juni 4 mwaka 2001, akimshukuru kwa kushughulikia suala la ofisi za ubalozi huo ambayo ilipokelewa na mahakama kama ushahidi.
Kesi hiyo imeahirishwa hadi Agosti 26 itakapoendelea kusikilizwa.
 
ninashindwa kuamini ya kuwa kweli professa mahalu ni mwanasheria kwa ushahidi wake usiyo na kichwa wala miguu..........................anachojivunia ni yeye kuongelea jinsi wakubwa walivyoafiki umuhimu wa ofisi bila ya kuelezea ni sababu zipi zilimfanya aingie mkataba wa ununuzi wa mamilioni ya dola ofisi nje ya utaratibu wa kisheria ya manunuzi.............................maana hapo ndipo kesi ilipo...........................ushahidi wa Mkapa wala haumsaidi kwa sababu unazungumzia umuhimu wa kuwa na ofisi yenye hadhi lakini hauwezi kuondoa makosa ya ufisadi hata chembe.........................ila kwa Mahalu kitakachoweza kumsaidia ni kwani yeye tu.......................where is the permanent secretary Philemon Luhanjo in all these............and whee is sungura mjanja JK?
 
Back
Top Bottom